Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Watu wanalalamika online

Kwanini timu za EPL zipo pamoja.

Same na Germany.

Barca anacheza tena na Benfica.

Inasemekana hii set up ni ili Madrid akutane na Liver.

Wanaamini ni set up
 
Niliwaambia Liverpool tutamkamata February, hesabu zangu bado zipo valid

Liverpool upcoming games
Man city vs Liverpool
Liverpool vs Newcastle

Arsenal upcoming games
Arsenal vs westham
N. Forest vs Arsenal

UEFA or EPL moja letu
Bora wewe umebaki. Hamisi amehamia unyumbuni mazima.
 
Partey pia ni moto wa mkaa. Huwa anachukua muda kukaa kwenye rhythm na akikaa anawaka muda mrefu. Ila pia ni mwepesi wa kupata injuries za kumkalisha nje muda mrefu. Atakupa mechi 2-3 mbovu ila baada ya haop atakupa hata 10 kali, kama akiweza kukaa fit. Kwa hilo muweke kundi moja na kina Jesus.
 
Watu wanalalamika online

Kwanini timu za EPL zipo pamoja.

Same na Germany.

Barca anacheza tena na Benfica.

Inasemekana hii set up ni ili Madrid akutane na Liver.

Wanaamini ni set up
Wanapanic tu. Huu mfumo mpya hauna seeding kwa timu za association moja. Kinachokutanisha timu ni nafasi walizomaliza kwenye league phase pamoja na waliotoana kwenye play-off. Timu zikifanikiwa kupita league phase, hakuna cha kukwepesha timu za association moja. Ni wa 9 atakutana na wa 17, wa 10 na wa 18, wa 11 na wa 19, nakadahalika. Ndiyo maana PSG alikutana na Brest. Baada ya hapo pia bahati nasibu iko clear.

Binafsi nimeuona ni mfumo mzuri ila unahitaji bahati nzuri na consistency kwa sana kutoka kwa washiriki. Points 9 au 10 hazitoshi tena kukuvusha kama enzi za groups. Sasa unahitaji zaidi ya points 15 kuingia top 8 na si chini ya 10 kubaki top 24. Yaani kidogo tu unaweza jikuta uko nje ya top 8 au nje ya michuano kirahisi mno.
 
Niliwaambia Liverpool tutamkamata February, hesabu zangu bado zipo valid

Liverpool upcoming games
Man city vs Liverpool
Liverpool vs Newcastle

Arsenal upcoming games
Arsenal vs westham
N. Forest vs Arsenal

UEFA or EPL moja letu
Acha kutukumbusha mambo ya mwaka juzi na jana.
arsenal ndoo
haaland kiatu
onana golden gloves
 
Huyu mtoto fala kweli.
 
Huyu mtoto fala kweli.
Alikuwa anacheza mechi 5 msimu mzima anarudi kwny meza ya matibabu.....kala Pesa ya bure sana ya Arsenal halafu anategemea tumkubali kwa undava alotufanyia baada ya kuona kapona kabisa na akatutosa....ilitakiwa tupangwe na wale Feyernood tukutane naye azomewe mwanzo mwsho
 
Huyu bwege na Ashley Cole mimi sitawasamehe aslani.
 
Punguzeni hasira ndugu zangu, mtaishia kujipa maradhi ya moyo pasi na sababu zozote za msingi.
RVP amewatumikia kwa zaidi ya miaka 8 pasi na kunufaika na kombe lolote la maana kutokana na ubahili pamoja mentality yenu.
Kipindi hicho Arsenyo ilijikita zaidi katika kutengeneza faida kwa kukuza na kuwauza wachezaji, Arsenyo ya kipindi hicho mafanikio yake ilikuwa ni kuingia top 4, sasa utamlaumu vipi mchezaji kama RVP mwenye hadhi ya kubeba tuzo ya Ballon d'or kwa wakati huo baada ya kuamua kwenda kutafuta changamoto sehemu nyingine zitakazo timiza ndoto yake?
Kwa shabiki yoyote wa Arsenyo mwenye uelewa ilitakiwa amshukuru sana RVP kwa kuwapambania kwa moyo wake wote, tena kwa kipindi kirefu cha miaka 8 bila ya kuchoka.
Nyinyi mlitaka RVP aishi maisha yake yote hapo Arsenyo?
RVP alikua anaipambania timu kwa uwezo wake wote lakini Arsenyau ndio iliyokua inamuangusha, matokeo yake alikua anaambulia tu tuzo binafsi za mfungaji bora pasi na kubeba kombe kwa misimu yote aliyokaa hapo Unyanini.
Ndoto zake akaja kuzitimiza alipohamia kiumeni.
 
Na mnashuka daraja msimu huu🤠🤠🤠....mechi mlizobakisha zote ni vichomi kwenu....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…