Herzogg
JF-Expert Member
- Apr 17, 2024
- 4,573
- 1,389
Nakumbuka msimu uliopita zilikua zimebaki mechi 5 kama sikosei, arsenal na liva walikua wanatuacha point 2 Arsenal akiwa kikeleni.Wazee wa conspiracy theory, yaani hii timu kuanzia kocha, wachezaji mpaka mashabiki wake hua wanaishi kwa imagination's.
Mtu anakaa anajitungia kastori kake mwenyewe halafu anaanza kujiaminisha na kuwaaminisha wenzake.
Humu kila siku tunaongea Arsenyau shida yao kubwa ni mentality, siku watakayo achana na maisha ya ndoto wakaishi kwenye uhalisia wa mambo ulivyo watabeba mpaka kombe la dunia.
Sasa hayo Makosa 115 yaliwazuia nini Arsenyo kuchukua ubingwa msimu wa 2022/2023 hali yakua mmeongoza ligi kwa siku 258 na zimebakia mechi 6 ligi kumalizika Arsenyo inaongoza ligi kwa point8 dhidi ya City?
Hayo Makosa 115 yamezuia nini kubeba kombe msimu ulioisha mpaka City akawa overtake na kumaliza ligi kwa tofauti ya points chache na nyinyi?
Wikiendi moja wote wakapigwa 2-0 na mid table teams huku sie tukashinda tukakaa kileleni mpaka ligi kuisha.
Halafu unakuja kuletewa habari za Michael oliver this, Michael oliver that π
Liva alichukua ndoo mbele ya hii hii city ya pep inayohisiwa kuhonga marefa, why?
Sababu wale wahuni walikua na uwezo, sasa hawa ndugu zetu kujaribu hii misimu miwili unaletewa habari za "FA hawataki tubebe kombe" π€£π€£π€£π€£
Jenga timu yenye uwezo, kombe unachukua haijalishi kahongwa refa ama ball boy.