Kajunjumelle
JF-Expert Member
- Aug 13, 2024
- 220
- 241
Yaani kipindi kifupi pekee ambacho Arsenal kamnyanyasa Liverpool ni kile Cha 2002-2006 mfano Ile mechi Thierry Henry anawapunguza kina Carragher na kumzunguka Dudek mechi ya 4-2 msimu wa invisibleNilichoandika ni kweli kipindi hicho nipo deep na ushabiki wa mpira kulikua na shabiki wa liver alibisha kama wewe.
Kazi ikawa ni kuprove mara ngapi Arsenal kamaliza juu ya liver kabla ya 2017 au 2018, alivyoona ukweli akakaa kimya. Hauna haja ya kubisha kama memory yako inaishia hapo 2000 na hizo hat tricks.
Andrey Arshavin aliscore magoli manne dhidi ya liver, unajua kama kuna hichi kitu?
Elewa kitu hichi, kipindi tupo on fire liver ilikua hovyo (hichi ni kipindi chote baada ya transformation ya Wenger) liver imekua vizuri Arsenal tuko hovyo (miaka 3 baada ya Klopp kuja)
Hatujawahi kugombea mchezaji wala makocha wetu kutukanana. Hatujawahi kugombea crown kwa pamoja ukilingaisha na united. Wako juu tupo chini, tupo juu wako chini.
Na Ile ya Julio Baptista kufunga harttrick Anfield ushindi wa 6-3 kombe la Carling(Sasa Carabao) msimu wa 2005/06
Nje ya hapo ni vipigo vya paka kakomba mboga yaani 5-1,4-0 za kutosha ikiwemo Ile ya msimu wa 2013/14 ambapo ndani ya dk 20 scoreboard ilikuwa inasoma 4-0 kiasi Cha camera kumuonesha Colsieny anatoa machozi kwa mechi iliyoisha 5-1