Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Yaani kipindi kifupi pekee ambacho Arsenal kamnyanyasa Liverpool ni kile Cha 2002-2006 mfano Ile mechi Thierry Henry anawapunguza kina Carragher na kumzunguka Dudek mechi ya 4-2 msimu wa invisible
Na Ile ya Julio Baptista kufunga harttrick Anfield ushindi wa 6-3 kombe la Carling(Sasa Carabao) msimu wa 2005/06
Nje ya hapo ni vipigo vya paka kakomba mboga yaani 5-1,4-0 za kutosha ikiwemo Ile ya msimu wa 2013/14 ambapo ndani ya dk 20 scoreboard ilikuwa inasoma 4-0 kiasi Cha camera kumuonesha Colsieny anatoa machozi kwa mechi iliyoisha 5-1
 
Itakua kuna sehemu sikuelewi.

So ili rivalry ije unahisi nini kingekuepo kingeleta rivalry?

Nimeongelea magoli ya mchezaji mmoja siyo matokeo ya mechi
Nielewe Kama ifuatavyo..Ni hivi hiyo gentleman rivarly unayoisema inatokana na unyonge wa Arsenal kwa Liverpool,kwa sababu fierce rival huchangiwa na tension of game,not otherwise...Sasa kwa mfano hivi unajua kwa zaidi ya miaka 10 Arsenal haijashinda mechi Anfield,wakati Liverpool kushinda Emirates ni Jambo la kawaida Tena kwa idadi kubwa ya magoli..5-4,3-1,2-0 nk??
 
Lverpool na United hazina fierce rivalry?
 
Kwako rivalry inatokana na mechi moja moja?

Siyo bigger picture?
 
Kuna hii streaming site naona iko vizuri kwa quality kuliko livesports 088
 
Mpaka 2013 bado liver hakai meza moja na Arsenal.
 
Ukiwa ni mfuatiliaji mzuri wa mpira utagundua kwamba RIVERLY kati ya club na club inaundwa na vitu vingi nje ya matokeo ya uwanjani

Ila sababu kubwa zaidi ni HISTORIA ya vilabu husika.Namaanisha namna vilabu vilivyoundwa na kukua.
 
Itakua kuna sehemu sikuelewi.

So ili rivalry ije unahisi nini kingekuepo kingeleta rivalry?

Nimeongelea magoli ya mchezaji mmoja siyo matokeo ya mechi
Ninyi Kenge mlikuwa mnaTuombea tufungwe ,tumemnywa supu Aston villa huko
Tumerudi nafasi yetu ,pimbi ninyi mlikuwa mmekaimu tu ,mabosi WA London tumerudi
 
Mkuu ulipotea sana mpaka nikahisi tayari umeshatupa manyanga na kuamua kuungana na boss wako Masingeli.
Humu alibaki chawa mmoja tu wa kuitwa mkorea tena kachezea spana za kutosha mpaka ikabidi mwenyewe aombe radhi na kujitetea kua ni Masingeli ndie aliekua anamshikilia akili yake, anadai kipindi kile hata yeye mwenyewe alikua hajitambui vizuri alikua anajikuta tu ameshaandika comments za kumsupport na kumuunga mkono Masingeli bila ya ridhaa yake.
Anadai Masingeli huenda alimtumia kwa nguvu za giza pasi na hiari yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…