makaveli10
JF-Expert Member
- Mar 27, 2013
- 35,749
- 103,684
Kwa sasa arsenal tunahitaji wachezaji walio bora, mchezaji ambae anaweza ingia kwenye kikosi chochote duniani..Kwa kiasi fulani, ndiyo. Ukiangalia hayo mambo amefanya huku akipambana na mambo ya kukosa wachezaji muhimu kwake, huku akijitahidi kupunguza wasio na manufaa (Ozil, Aubameyang, Tierney, Bellerin, Maitland-Niles...).
Yaani, kama makocha wote tu kwenye ligi, anafanya hayo huku akijitahidi kujenga timu inayomfaa kila msimu.
Mfano, unaona kawaleta Rice na Kai baada ya Xhaka kuondoka. Anajua ana mmoja wa makipa bora kabisa kwenye ligi, Ramsdale, lakini bado akamleta Raya, na Raya kadaka Golden Glove. Hii inaonesha kuwa dogo anataka kuimarisha kila sekta awezayo kadri awezavyo.
Kazi ipo kwenye kuleta wachezaji bora na bora zaidi kila msimu. Akifanya vizuri na kuendelea kuingia michuano ya Ulaya, atazidi kuvutia wachezaji wazuri.
Then linakuja suala la mbinu uwanjani. Ni wazi kwamba kwa mchezaji mmoja mmoja, Arteta hana akina Watkins, Doku, KdB, Olise, nk,. baadhi ambao wangeanza mbele ya wachezaji wake alionao , ila ukiangalia jinsi alivyowatumia alio nao, unaona ni kocha aliye vizuri kidogo kimbinu. Na factor ya mbinu ni muhimu maana ndiyo moja ya vitu vinavyotenganisha mafuta na maji kwenye hili game.
Saliba,ben white, partey, odeergad.. wanahitajika wengine wenye ubora mkubwa saana.
Mpaka kufikia hapa ubora wa mbinu za mwalimu ndio umetufikisha hapa, tunahitaji wachezaji bora zaidi, kuwa bora zaidi.


