Arsenal (The Gunners) | Special Thread

ulaya ulaya ni ulaya, mwenye uwezo ndio atakae funga kesho.
 
Mchezaji akitoka Ajax ligi ambayo dominant ni Ajax, Feyenoord na zingine mbili uwezekano wa kupigwa ni mkubwa.

Antony na Malacia ni mfano wa haraka kwa nyinyi United.

Nionyeshe wachezaji wabaya wa Arsenal ambao kwa Arsenal ni starters na unaamini hawana mchango wowote
 
Niliwahi shauri kwa mzaha ila kuna ukweli ndani yake.
Makocha wa epl hasa top six wameshaonjeshwa uji wa moto wa kipara.
Hawa kina arteta na wenzake wakae chini wamwite kipara,wamshukuru kwa uwepo wake ndani ya ligi kwa miaka 8 kisha kwa heshima wamwambie apeleke kimbunga chake SERIE A au LA LIGA

Kipara mwenye enough fund source ataendelea kuinyanyasa ligi 😂😂😂

Ikishindikana wachangishane mkwanja wampe aende akale pensheni huko,jamaa na waarabu wake wanajua hadi wanakera
 
Vinahitajika vilabu angalau vitano vyenye consistency ya kipara.
Kipara anaimarisha kikosi every season. Ananunua mchezaji 100M na hamtumii na wala siyo kesi kwakua timu inaleta matokeo mezani.

Nataka abaki hapo hapo kipindi hichi ambacho matumizi yanaanza kubanwa
 
Hili ni jambo ambalo kila mtu analisubiri kwa hamu kubwa
Tunataka kuona kipara bila pesa ya kumwaga anaweza fanya anachofanya?

Tactically hatuna wasiwasi nae,ila ngoja tuone akiminywa swala la technical recruitment je ataendelea kufanya tunachoona leo?
Jamaa absolutely ni gifted ila pesa ya mwarabu imempa upper hand kwenye title races
 
Ili mchukue ubingwa mnahitaji kocha wa kueleweka mwenye mentality za ki utu uzima sio premature kama Arteta.
Tafuteni Attacking mid wa maana Odegaard anachangamsha kijiji tu.
Saka sio mchezaji wa kuwapa kombe la maana huyu anatakiwa kuwa bench warmer. Kwa kifupi nyie kenge mna world class mmoja tu Declan Rice wengine wote ni magarasa
 
We jamaa ni fala tabaka la juu kabisa. Mwenye mentality ya ubingwa ni Klopp au sio?
Ambaye since 2015 mpaka sasa, msimu wa 9 ana EPL moja.

Klopp akiwa Liverpool

2015/16 Hola
16/17 Hola
17/18 Hola
18/19 Hola
19/20 Ndo hapa kapata kombe la Corona
20/21 Hola
21/22 Hola
22/23 Hola
23/24 Hola

Huyu Klopp, wakati anakuja Liverpool ilibidi asubiri miaka minne ndo apate kombe lake la kwanza la ligi. Baada ya hapo kaendelea kusugua. Na wengi wa mashabiki wa Liver mliufyata kimya.

Klopp anakuja Liverpool akiwa ni kocha mzoefu kabisa, kashacheza mpaka fainali ya UCL.

Miaka 9, EPL moja
 
Hiyo comment ya CASTR, kwamba KUDUS tungemkataa Emirates, niliisoma jana nikawa sijamuelewa kabisa. Umefafanua vizuri kilichopo kichwani mwangu.
 
Naamini ataadopt fasta na kuonesha ubora zaidi ya saka.

Kila nikimtizama saka, natamani tupate bora zaidi ya saka, arsenal ya msimu ujao inabidi ibadilike, nafasi ya saka unahitajika ubora wa mo salah yule wa misimu kadhaa hapo nyuma.

Kwenye ulinzi tumetulia, ila sasa safu ya ushambuliaji inabidi iongeze ukatili sana.
Kiungo atafutwe mtu wa kuziba pengo la partey chap kwa haraka.
 
ARSENAL ni TIMU NZURI SANA ila haina Wachezaji Wengi wazuri sana. Mchango wa Mchezaji ndo Unapelekea kutengeneza timu Nzuri! Unaona kikosi cha ARTETA Ni wachache sana wanaweza kuwa STARTERS katika timu zao za TAIFA hasa Mataifa makubwa Kisoka.

Nadhani umemaanisha Ligi ya Uholanzi, UTD & ARSENAL Ni wanufaika wakubwa toka Hii ligi. Mchezaji kupigwa ni Suala la Mifumuko ya Bei na Kukosa watu Makini wa Mpira.

Hoja ni KUDUS, Kama ARSENAL Ingempata Hali ya SAKA Ingekuwa kama Martinelli na Trossard. Wachezaji wa Kiingereza wako na Tabia ya Kujisikia wasipopata Ushindani na SAKA + PALMER wameshaingia kwenye kundi hilo.
 
Kuna kiazi kimoja kipo mbele kuipa ushauri timu iliyo nafasi ya pili anaacha kujishauri yeye yupo matopeni huko hata ashinde mechi alizobakisha hafikii points zetu
 
Unahisi Arsenal inamhitaji Kudus kuliko United?
 
Xhaka kashacheza LB

Fabio akiwa liva kashaceza CB.

Kimmich kacheza CB.

Alaba anafika Bayern ni DM ila akawekwa CB.

Kama hauelewi maana ya DM ni Defensive Midfielder means anajua kila kitu kwenye standing tackles, interceptions, ball carrying, sliding tackles n.k.

Ikatokea huna beki the next option unayokua nayo ni DM. Timu nyingi zimechezesha DMs kama mabeki nyumbu hua nasema hawajui mpira so kwao wanahisi ni jambo la ajabu.

Kuna beki wanachezea mpira vizuri mpaka wanapelekwa kua viungo mfano Kimmich, Alaba na kuna kipindi mashabiki wa liva walisuggest Trent awekwe kama CM. Ni sawa na sisi tulivyotamani White apelekwe Midfield.

Muwe mnaelewa kwanini kwangu ni ngumu kuongea mpira na mashabiki wa kenge na nyumbu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…