Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Naangalia mazoezi ya mancity hapa wanajiandaa na game jumanne sijui wanacheza na nani lakini mazoezi makali sana. Rodri amekimbia kilimota 50.
Nawashauri msitarajie chochote

Kila mtu ashinde mechi zake.
Nakutakia kila la kheri na Aston Villa. Nona hasira na Villa sana nataka muwapige hata mkono ila uwezo wa kuwafunga sidhani kama mnao. Hivyo kisasi tutalipiza wenyewe msimu kesho.

Kwa leo, kila la kheri.
 

Yaani sisi tutafute pa kujificha kisa hatujawapiga kono la nyani? Nyie huenda FA cup ndiyo njia pekee ya kuingia mashindano ya Ulaya. Bila hivyo nafasi ya 8 inawahusu. Halafu eti sisi tukajifiche. 😄😄😄😄
 
Mnajisifu kuwafunga goli 1 United isiyokuwa na CB na AM ya McTalantaless!
Nawaombea mbebe ndoo msimu huu maana baada ya hapa hata europa hamtagusa tena.
Narudia kusema tena, huu ulikuwa upepo kama wa leicester city na ndio umepita hivyo.
 
Vocha sisi hatutaki tunachotaka sisi ni nyie mkose kombe tu hamis aendelee kujificha huko huko vichakani🤣🤣

Acha record ya Ferguson ivunjwe tu ila nyie wakora kombe msibebe tu.
 
Yaani sisi tutafute pa kujificha kisa hatujawapiga kono la nyani? Nyie huenda FA cup ndiyo njia pekee ya kuingia mashindano ya Ulaya. Bila hivyo nafasi ya 8 inawahusu. Halafu eti sisi tukajifiche.
Mkuu ukishaamua kushabikia Arsenyani automatically unakua na mentality za kinyaninyani, wapi mimi nimesema mtafute pa kujificha kisa hamjatupiga kono la nyani?

Nimesema Arsenyodo mkimaliza msimu mikono mitupu halafu Utd tukibahatisha kuchukua kombe la FA mtafute sayari ya kwenda ujificha.
(elewa kwanza neno kubahatisha) maana kiuhalisia na hizi beki zetu za kina Kambwala hatuna uwezo wa kumfunga City
 
Mnajisifu kuwafunga goli 1 United isiyokuwa na CB na AM ya McTalantaless!
Nawaombea mbebe ndoo msimu huu maana baada ya hapa hata europa hamtagusa tena.
Narudia kusema tena, huu ulikuwa upepo kama wa leicester city na ndio umepita hivyo.
Mkuu fuentte jambo la kwanza kabisa waombe radhi leicester city kwa kuwafananisha na vitu vya kijinga kijinga.
Jambo la pili hawa sio wa kuwaombea wapate hata kombe la uji, kama unawahurumia sana ni bora uwaombee wapate hata mimba lakini sio kombe.
Hebu vuta picha hawa Kima wanaongoza kwa clean shit na GD tu lakini humu hatupumui sasa wakibeba na kombe si watatupiga marufuku hata kuvuta Oxygen kabisa hawa?
Potelea mbali ni bora Epl ionekane ni Farmers League kwa City kujimilikisha hilo kombe mpaka pale timu nyingine zitakapokua tayari kuchuana na Kipara, lakini sio kwa hii misukule ya London kubeba kombe la ligi
 
Nimekuwa shabiki wa arsenal kwa zaidi ya miaka 25
Nimeangalia mech zenye tension kubwa na kawaida
Nimeona generation za wachezaji wengi na waliotarajiwa mengi
Nimeona ushindani wa makocha wengi ndani ya epl na mifumo mingi

Ila kwa sasa guys ligi imebadilika saaana.
Mechi moja unayopoteza August inaweza ikakuhukumu may
Ni kama kocha na wachezaji wanatakiwa kuwa full perfect with no room for errors and correction
Ukitazama quality ya makocha walioko epl kwa sasa unauona ugumu wa kubeba ligi


Kwa mara ya kwanza jana nimeangalia mech yetu kwa tension ya hali ya juu mno.

Kwenye somo la uokoaji hasa kwenye ajali za majini mtu unafundishwa kwamba hakuna kitu hatari kama kumuokoa mtu anayetaka kuzama.anaweza kukung'ang'ania na mkafa wote.

Jana united walikuwa wanatoa aura ya mtu anayezama na ameona mtu wa kutaka kumuokoa.wali give it all
Kocha alikuwa anataka kuproove kitu
Wachezaji walikuwa wanataka kuproove kitu
Hata mashabiki walikuwa wanataka kuproove kitu
Thanks united
 
Saka amechoka,anahitaji msaada wa a strong back up,tena awe ana style tofauti na ya saka

Tunahitaji namba sita mwingine partey na jorginho hawaaminiki

Tunahitaji mbadala wa odegard,a driving typical RCM with pace,dribbling skills,passer,long short merchant,physically tough,awe ni holder wa mpira haswahaswa na mwisho na muhimu mno awe na atributes za ulinzi.ode kuna muda anapwaya na anakata pumzi

Tunahitaji sriker wa magoli,awe na attributes kidogo za link up play ila alijue goli vizuri na ningependa awe awe above 25

Tunahitaji legend mmoja wa invisible au mwingine yoyote akae bench la ufundi na awajenge madogo kwenye mech za tension kubwa na ndo maana timu imesita kumuacha jorgy
 
Msimu ujao mnamaliza wa 15 hakyanani🤠🤠...kama mentality ya timu yenu ndo hii kwmba mmetufunga ila wachezaji Fulani hawakuwepo hakyanani mna Hali ngumu huko mbele....labda muuze kikosi kizima kitu ambacho hakiwezekani....tabu ipo palepale
 
Nakubaliana na wewe, Partey jana alikuwa below Average, so is Saka. Ollise asingekuwa na injuries, ningeshauri aje kumpa challenge Saka
 
Vocha sisi hatutaki tunachotaka sisi ni nyie mkose kombe tu hamis aendelee kujificha huko huko vichakani🤣🤣

Acha record ya Ferguson ivunjwe tu ila nyie wakora kombe msibebe tu.
Hahaha............tafadhali tuombeeni tubebe hili Kombe, tuna muda mrefu hatujanyanyua hilo Kombe


Ila Vocha zenu bado ninazo, endeleeni kutuombea
 
Wewe kinachookuuma ni sisi kutowafunga kono la nyani. Hizo ndoto za hata kubahatisha kumpiga City sijui unazipatia wapi.

Labda nikusaidie kuota:

City atashinda Premier League.
Sasa tuseme Pep hana hasira yoyote ya kukosa Champions League. Hana hasira yoyote ya kukosa Kalagabaho. Yeye awe amefurahi kabisa na kushinda EPL pekee na asitake kabisa kushinda FA pia.

Kwa hali hiyo, naona mnaweza kubahatisha hilo FA, ila usidhani tunahaja ya kujificha popote.

Kiukweli, kama mnataka kucheza Ulaya msimu kesho, kushinda FA ndiyo njia pekee mliyonayo. Newcastle hawatawabembeleza kama sisi. Chelsea hawatawaacha muwapite...
 
sisi mashabiki wa arsenal tunaombea spurs amkazie city ila kabla ya kuombea spurs amkazie city tumuombee liver amchape Aston villa ikitokea hvy nakwambia game ya kesho city ushindi wake mkubwa ni draw spurs watakaza sana washinde Kwan mechi ya mwsh crystal palace atacheza na Aston villa ambapo kutoboa ni ngumu ila ikitokea liver akafungwa spurs hatoingia top 4 na atamuachia city ashinde
 
Hakika mkuu, siku hizi hautaji tu kuwa bora hili uweze kuchukua ligi, bali yakupasa uwe na ubora ambao hauna makosa kabisa... yaani kama unafanya mistakes basi hakikisha wapinzani wako nao wawe wamefanya mistakes ambazo zina impacts sawa na kwako.

Zamani ilikuwa ukishinda mechi 25 tu kati ya mechi 38 basi wewe moja moja kwa moja una uhakika wa ubingwa, Manchester united amechukua ubingwa mara 20, na mara zote hizo hakuwahi kushinda mechi zaidi ya 26, hata points nyingi alizowahi kuzifikisha ni 85, lakini ndio timu yenye mafanikio zaidi kwenye EPL, sababu ilikuwa ni bora tu.

Msimu wa 2018/2019 Liverpool alishinda mechi 31 na alimaliza na points 97 lakini bado akaukosa ubingwa..... hii inaonesha ni jinsi gani unaweza ukawa bora lakini bado ukakosa ubingwa kwa sababu hauna perfection.

Jana Arsenal tumeshinda mechi ya 26 tangu msimu umeanza na hizi ndio mechi nyingi tulizowahi kushinda tangu tupande daraja, kwa mara ya mwisho kushinda mechi nyingi hivi ilikuwa ni msimu wa 2003/2004(invincible season) ambapo tulishinda mechi 25.

Unaweza ukaona kipara ameweka standards za hali ya juu mno hili kuchukua ubingwa, yaani unahitaji karibu kila timu uwe unajipigia tu na hasa round ya pili.

Kwakweli ni kazi sana, ila ninachojivunia kuna mabadiliko makubwa sana kulinganisha na misimu mingi iliyopita huko nyuma. Acha tuone kesho Spurs pengine labda anaweza akatupa ubingwa licha ya chuki kali aliyonayo dhidi yetu
 
Kudus akija Arsenal tutamkataa.
Kudus anacheza timu ambayo inategemea sana long balls na kuzishambulia spaces za mpinzani.
ARSENAL ina timu Nzuri sana ila haina WACHEZAJI wengi wazuri sana. Castr ARSENAL ilimuhitaji Mudryk ila ikaishia Mpata TROSSARD, Hajawa chaguo Baya na amekuwa na Mchango Mkubwa ila kama ARTETA angempata MUDRYK Yule Bwana angekuwa anaimbwa.

KUDUS ilikuwa Chaguo la kwanza kwa ARTETA. Stori yake ingefanana na MARTINELI. Leo hii MARTINELI anapambania Nafasi, SAKA amekuwa kama ana kura Turufu sababu hana Mpinzani wa kueleweka kwenye Nafasi yake.

Kama KUDUS angeenda ARSENAL angefanya Makubwa. AJAX wanacheza mpira wa kumiliki kwa hiyo isingempa Changamoto ARSENAL, Hapa ni kumpongeza namna ameweza ingia Poa timu inacheza tofauti kabisa na Alipotoka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…