Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kai ananikumbusha mimi nilivyokuwa shule nilikuwa mpole sana mpaka sikuweza kufikiriwa kuhusishwa na vitendo vyovyote visivyo sawa vya wanafunzi.

Kuna siku mwalimu mmoja aliniudhi nikarivenji kwa kumuaribia mali yake flani. Baadae nikakutana nae akiwa amesikitika sana na akaanza kunieleza jinsi kuna mwanafunzi ameharibu mali yake, mimi namsikiliza tu. Akaniambia kabisa "Halafu HENRY14, namjua kabisa ni nani amefanya hivyo, na nitakachomfanya, maji ataita mma". Mimi nikampa pole pale nikamuaga nikasepa zangu.

Huwezi kudhani kama Kai ana kauhuni uwanjani.
 
Kai anacheza rafu sana ,halafu mpole sana, VVD na Konate wanamjua vzr alichowafanya

Kai off the ball ni mzuri zaidi kuliko hata akiwa na mpira

Anafanya movement nyingi sana za kuwatoa watu mchezoni

Pia sio Abiria uwanjani ,anacheza false 9 lakini bila mpira anarudi katikati kabisa, Arsenal wakiwa na mpira ,sekunde yupo mbele ,


Wachezaji kama huyu ambao sio abiria uwanjani ngumu kuwanyima nafasi


Arsenal inavyocheza haihitaji mchezaji abiria kama kina mactominay, rashford,Bruno


Ndio maana hakuna mchezaji wa manjesta hata mmoja anayeingia hata benchi la Arsenal
 
Na hii ndo modern football inavyotaka...Mwalimu anachokutuma unakifanya🤠🤠..hawezi kuwa na quality kama ya Henry au Van Persie au Ozil...lakini ukimwambia nataka wale mabeki 2 wa pale kati wasiwe na siku nzuri basi watakuwa na siku mbaya siku hiyo🤠🤠....unapofanya chaos unatengeneza room of error kwa timu pinzani mara nyingi na hiyo Ina create nafasi kwa timu yako....angalia magoli mengi ya Arsenal msimu huu...kama hajahusika kwny kufunga au kutoa assist basi either mpira ulipita kwake au kuna room of error aliilazimisha kwa timu pinzani....na hiki ndo kinamfanya awe panga pangua hakosekani uwanjani
 
Ki

Kifupi ubovu wa kai unafichwa na matokeo ya arsenal.
Kai ana matatizo mengi kuliko mazuri yake.
Nadhani uko sahihi pia. Tunabebana. Nataka mengi zaidi kutoka kwa Kai. Na siku hizi nawadai zaidi Martinelli, Saka, Trossard, Jesus na Odegaard. Naamini wako gia #3 na wanaweza kwenda #4 na #5.
 
Ww Sasa naona una kakampeni Kako🤠🤠...wachezaji Wana miili ya kawaida kama sisi ila Wana mazoezi sana..Sasa huku kuwadai kwako unataka wacheze kama Shaolin soccer sio🤓🤓...watazidi ku improve as long as wapo pale jino kwa jino na mandevu Klopp....yaani huu mbinyo tunaoutoa na pressing anayofanya Odegaard especially kama jana na yy bdo unamsakama....nimekushindwa mkuu
Nadhani uko sahihi pia. Tunabebana. Nataka mengi zaidi kutoka kwa Kai. Na siku hizi nawadai zaidi Martinelli, Saka, Trossard, Jesus na Odegaard. Naamini wako gia #3 na wanaweza kwenda #4 na #5.
 
Saka is too good. Mechi zake 3 mpaka 5 za mwisho huenda sio Saka yule tunayemjua, maybe anatupa 65% ya kiwango chake.

Lakini hiyo 65% ndo same na 100% ya baadhi ya wachezaji wa timu fulani fulani hivi
 
hahahahaha hapana bro. Mimi si nawaona uwanjani...najua wanaweza kufanya mambo.
Labda nimemiss tu kupiga watu 5-0 na 6-0. Jana Brighton alipaswa kula angalau 5.
 
De Zerbi "The penalty was clear..."

Angekuwa yule fraud mwenye Kipara, angeleta blaah blaah kama zote
 
De Zerbi "The penalty was clear..."

Angekuwa yule fraud mwenye Kipara, angeleta blaah blaah kama zote View attachment 2956176
Utasikia

"hata ile mechi ya Arsenal ilibidi tushinde"

"Hatuna majeruhi kama Arsenal"

"Garnacho hakua offiside pale Emirates"

Hapo anacheza na timu zingine kabisa.
 

To make stats clear:
11 matches;
38 goals scored
04 goals conceded
07 clean sheets
01 goal conceded away from home
3.5 average goals per game

On top of the premier league table, ladies and gentlemen this is Asenali!!
 
Kuwashabikia man u Leo nikutafuta magonjwa ya moyo yasiyo na lazima, Mabeki wao waliofit ni Maguire na kambwala , Wana abiria sio chini ya wanne ,

Plus mbinu za Erik Ten hag, kila baada ya dk 1 wanapelekewa moto

Kama unataka kumuona Prof. Janabi ,shabikia Manjesta leo
 
Msimu jana tulimaliza ligi na points 84, GD 45.

Msimu huu mpaka sasa tuna points 71, GD 51.

Tukishinda mechi zote zilizobakia tutamaliza na points 92.

Pamoja na kuchelewa kuwasha moto msimu huu ukichangiwa na dhulma za marefa na kushuka form kidogo, naweza kusema kuna mambo mazuri msimu huu yametokea ya kufanya tuseme tunazidi kupanda.

Tukimaliza na points nyingi zaidi ya msimu jana itakuwa poa sana. Tukibeba kombe itakuwa poa zaidi. Ila tusishindwe kutambua kuwa tunapanda na tunapaswa kuendelea kukomaa na kupanda zaidi.
 
Njia yetu ya UCL ni ngumu nusu fainal ,


Binafsi hata kabla makundi hayajapangwa nimekuwa namuomba Madrid huyu nammudu vzr sana


Mancity vs Arsenal ni mechi ya mbinu na commitment kubwa , hutakiwi kusinzia hata dakika moja


Tukifika Fainal basi kazi imeisha ,

Fainal tutakutana na PSG ,Barca au Atletico Madrid


Mziki upo nusu ambapo naona kabisa Mancity anaenda kumla kichwa Madrid

Kama Madrid atapita basi nacheza Wembley mapema sana
 
Timu zote zinawaza zitakabiliana vipi na sisi. Wale wakupaki basi wanajua sisi ni wafungaji bora na tutawatoboa tu. Wale vinara wa mashambulizi wanajua sisi ni wazuiaji bora na kutufunga itakuwa mtihani. Man City na Tottenham ndio nawaona wanaweza kutupa shida tukiwa kwenye form nzuri. Wengine naona watatuweza tukiwa tumeamka vibaya siku hiyo.
The lowest xG conceded in the Premier League in 2024:

1. Arsenal - 4.98
2. Manchester City - 12.28
3. Liverpool - 13.56

The Gunners are in a league of their own. View attachment 2956196
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…