Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Villa jana kimewakuta kilichotukuta kwenye defeats zetu za msimu huu na hata dhidi yao.

Chances zinatengenezwa, scorer hakuna.
ilifika kipindi xG yetu tukawa tunazidiwa na Luton ,nafasi nyingi ,magoli hatufungi

Kwasasa tunaongoza kwenye defence na kutengeneza nafasi ,tuna xG kubwa , tupo top ,

Next Burney ,jumanne Porto

Hizi mech za Sasa hasa mwez huu tushinde zote ,Wala sio ngumu,

Kuingia April ,Imani tutakuwa tupo full squad ,

Partey anatarajiwa kuwepo vs Porto

Tomiyasu
Zinny
Vieira
Smith rowe
Jorginho
Timber
Jesus

Wote wanatarajiwa kuwa fit mwez ujao ,

Mikel anasema anahitaji wachezaji fit mechi za mwisho ,
 
ETH anatamba anasema kwasasa anampiga yeyote


Amecheza na villa lakin anadai alistahili kuifunga Arsenal na Liverpool


Huyu kocha manjesta fans wanadai simpendagi ,kaangalieni stats za hizo mechi

Hata hiyo ya villa kabahatika ,siokwamba aliukamata mchezo ,lakini cheki anavyotamba

Utofauti wa Flano na ETH ni upi
 
Huyu dogo anapendwa sio na mashabiki tu,hadi wachezaji walikuwa wanamwambia Mikel amuingize akacheze



️ “Bring Ethan Nwaneri in!”,

Arsenal players on the bench were whispering in the second half.

Mikel Arteta:

“They really wanted me to bring Ethan in”,

said via @jamesbenge.
 
Kwenye mahojiano na waandishi wa habari baada ya mchezo kumalizika Mikel Arteta alinukuliwa akisema wachezaji waliokua "bench" walitaka Ethan aingie...kupitia IG Ramsdale anaonekana kumtag @FrelloJorginho kama mchezaji aliyeomba Ethan aingie

@FrelloJorginho
 
Huyu ndiyo maana hua nasubiri afungwe.

Maneno mengi mno.

Hiyo game hizo stats ulizoona ndiyo ukweli ulivyokua, hakuna kitu wameonewa.

Ila the fact that analala anatuota speaks volume
 
Kuachana ukiwa unamaanisha kumuuza au tuache aendelee kukua taratibu huku tukiwa tunampa mechi chache sana....fafanua
Nilimaanisha kumuuza mapema akiwa anahitajika na timu zingine. Najua bado dogo ana 16, sasa sijajua kama atarefuka sana zaidi ya hapo ndani ya miaka 2-3. Nia ni ili tumsahau mazima tufocus na wachezaji wenye miili mikubwa, watakaoweza kustahimili mikiki mikiki ya ligi.

Wachezaji wenye miili midogo kama Wilshere, Carlos Vela, Fabio Vieira, kwa kiasi fulani hata Cedric, wanakuwa targetted sana. Wengine wanajikuta majeruhi mara kwa mara. Kusurvive baadhi ya wachezaji walibidi wawe tough kiasi na skills nyingi, kama Mtakatifu Cazorla.

Nilikuwa na wasiwasi wa hivi kwa Saka pia alivyoanza, ila jamaa sasa amejijenga physically na amerefuka kiasi.
 
Jana alikuwa anatembea na Kudus tu mwanzo mwisho🤠🤠🤠....mpk ikafika kipindi nikawa najiuliza Kudus bdo yupo uwanjani
Huyu jamaa alikua na debut mbovu mno.

Ila baada ya pale ni mechi moja ama mbili ndiyo niliona ana makosa
a
 
Mkuu yule dogo ana kitu miguuni....kanatakiwa kapige gym sana katitie...kakiwa na nguvu ya kutosha basi inatosha...kazi chafu watafanya kina Rice na mtakatifu Kiwior🤠🤠🤠
 
Mkuu yule dogo ana kitu miguuni....kanatakiwa kapige gym sana katitie...kakiwa na nguvu ya kutosha basi inatosha...kazi chafu watafanya kina Rice na mtakatifu Kiwior🤠🤠🤠
Kiwior sikujua kama ni mkatili vile. Nadhani kuishi na kina Benny Blanco na Gabriel kumembadilisha. Na yeye pia bado kijana anakuwa.

Ninachomiss kwa Kiwior ni zile long balls zake cross-field . Wakati anakuja tulicheki sana clips zake za pass kutoka beki hadi kwa strikers na wingers tukasema 'kwa distribution hii, wapinzani watakoma'.
 
Mkuu yule dogo ana kitu miguuni....kanatakiwa kapige gym sana katitie...kakiwa na nguvu ya kutosha basi inatosha...kazi chafu watafanya kina Rice na mtakatifu Kiwior🤠🤠🤠
Tumpe muda. Nimegoogle urefu wake nikaona 1.65m. Diego Maradona alikuwa 1.65m. Ethan bado anakuwa labda atajazia jazia. Na game ya sasa inahitaji ukomaee.
 
Tumpe muda. Nimegoogle urefu wake nikaona 1.65m. Diego Maradona alikuwa 1.65m. Ethan bado anakuwa labda atajazia jazia. Na game ya sasa inahitaji ukomaee.
Yule dogo ana kau Jack Wilshere ndani yake na u Cazorla hivi...katakata sawa...na nadhani Arteta anampa gemu moja moja kumuonesha kwmba ana future kwny klabu...maana mijizi Chelkenge na Man City ilitaka kumuiba kwa kumpa mshahara wa kufuru bwana mdgo🤠🤠🤠....Arteta akamtuliza
 
Kiwior ni LCB , ila kama unavyojua Arteta anamtumia LB, Tena alikuwa anamtumia LB wa kuinvert akawa anazingua

Arteta akagundua hatakiwi kumchezesha LB ya kuinvert Bali acheze LB ya kustick nyuma ,ndio maana anacheza vzr


Mechi ya Liverpool,na ya Jana amecheza LB ya kukaa nyuma


Jana aliyekuwa ana invert to midfield ni White


Kiwior ni LCB hapo ndio utaziona hizo long balls ,bahati mbaya LCB yupo Magalhaes na huwezi kumtoa kirahisi .


Kutokana na Hali hiyo imebidi acheze LB, lakin asifanye invertion to midfield,
 
Hii ishu nimeona kuna shabiki kaisemea Reddit.

Sasa changamoto ni hiyo.

Akipiga anadeliver vizuri asipopiga uwepo wake ni advantage kwenye box. Mwisho tukakubaliana aendelee kupiga
Mwanzo nilikua naona mpigaji alikua Trousad akiwepo uwanjani sikua nashangaa asipokuwepo LT19, ila hivi karibuni LT19 namuona uwanjani na Pia Rice anaendelea kupiga, ila impact yake ni kubwa sehemu zote mbili game vs Nyumbu lile bao lilitokana na mpira wa aina iyo
 
Asivimbe kichwa, atapotea mapema, tushaona vipaji maridhawa kabisa, vikiimbwa ila matokeo yake sasa wakapotea kwa kupewa misifa mingi.
 
Asivimbe kichwa, atapotea mapema, tushaona vipaji maridhawa kabisa, vikiimbwa ila matokeo yake sasa wakapotea kwa kupewa misifa mingi.
Sio rahis kuvimba kichwa, uzuri wapo wachezaji anawaangalia tokea pale pale Arsenal wanawachukulia kama mfano , Smith Rowe,Saka,Nell, na Partino alisema anachukulia mfano wa Saliba kuamin ipo siku atalejea Arsenal na kua mchezaji wa muhimu.
 
Aisee hivi dogo umeomuona vizuri au unaongea tu huyo dogo hapa juzi City na Chelsea walitaka kufanya hujuma Arsenal ilibidi waingilie kati ndo akasajiri mkataba bonge la kiungo hilo.
 
Aisee hivi dogo umeomuona vizuri au unaongea tu huyo dogo hapa juzi City na Chelsea walitaka kufanya hujuma Arsenal ilibidi waingilie kati ndo akasajiri mkataba bonge la kiungo hilo.
Ndiyo maana nikasema tumpe muda na nikatoa mifano ya wengine wadogo wadogo waliopata tabu kwetu japo walikuwa na vipaji sana. Nilimsahau Eduardo pia. Wajinga walimvunja mguu kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…