Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Hapa kwa Partey hapa🤠🤠...fanya kama hyo jamaa alishauzwa..ni mchezaji nnayemkubali kuliko wte pale Arsenal ila tyri imeshakuwa flat tyre tena yenye kipara....hyu Hana msaaada wwte kwasasa...usajili ujao tulete Fofana mtu kazi pale kati
 
Na hii ina expose weakness ya Arteta, kwahiyo 65M kwa ajili ya kushinda mipira ya hewani tu?

Trossard kaingia na instant impact, ni mara Mia LCM achieve Zinchenko huko LB achieve Kiwior. Huyu Havertz is bullshit.
Hiki tunachokipigia kelele kila siku kua Zinny acheze LCM na Arteta hana hata wazo hilo ndo hiki hiki mashabiki wengi wa Liverpool wanatamani klopp amuweke TAA kwenye kiungo na klopp hana hata muda huo ni kwanza sisi tunawaza zaid kuliko wao au ni kua impact kwenye nafasi zao wanazocheza ni kubwa kuliko ambapo tunapowafililia sisi kwenye nafasi za kiungo?
 
Unataka kujua kwanini Jana Zinchenko hakuwa anaingia ndani kama ilivyozoeleka kwa Arsenal ( Inverted FB ) kuwa karibu na kiungo wa ulinzi Declan Rice ?

Well, sababu sio Jorginho , kwamba uwepo wa namba 6 wawili Jorginho na Rice ndio ulifanya Zinny asiwe na sababu yoyote ya kuingia ndani kuwa kama kiungo ... la hasha , bali sababu ilikuwa :- MUUNDO WA PRESSING WA LIVERPOOL ( 4-1-4-1 ) . Kivipi ?

Hapo maana yake Liverpool watakuwa wanakabia juu kwa kutumia wachezaji watano ( Straika na viungo washambuliaji wanne nyuma yake ) : sasa kwanini huu muundo ufanye Arteta abadilishe build up structure yake ?

Muundo wao Arsenal mara nyingi ni 3-2 ( mabeki watatu wa nyuma White Saliba na Gabriel ) huku mbele yao ni Rice na Zinny ) kama wangefanya hivi maana yake ingekuwa 5v5 kwasababu Arsenal nyuma wangekuwa watano kitu ambacho ni risk .

KWAHIYO : Arteta akaamua kubadilisha build up structure yake kutoka 3-2 kuwa 4-2 ( White Saliba Gabriel na Zinny ) huku mbele yao ni Rice na Jorginho kwahiyo hapo inakuwa 6v5 , faida ya mchezaji mmoja ( hapo wanakuwa wametengeneza overload ) . Angalia goli la kwanza la Arsenal .

NOTE

Kwenye huo muundo juu walikuwa na namba 10 wawili Kai na Odegaard lakini sio mstari mmoja bali Kai alikuwa pembeni juu kidogo ya Odegaard ... kwanini ? Ili kushambulia space baina ya TAA na Konate .!

AMBANGILE
 
Sasa ukute mashabiki MAANDAZI wa JF wanavyomtukana Arteta! Utasema ni makocha nguli hapa duniani. Pumbafu kabisa.
 
Na hata Goli la kwanza lilipatikana Kwa sababu hiyo, kaangalie ile buildup ,
 
Mnanishangaza sana mnaosema Kai ana physique
Ile incident yake na mac allister kama angekaza kidogo tu angeweza fanya chochote

NB Jana kacheza vizuri ila kwa price tag ile bado tunamdai
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…