Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Grupu jepesi Sana lile , PSG,AC MILAN wapo hoi bin taaban, BVB kule Bundesliga wanajipigia tu

Halafu mtu anakwambia eti kundi la kifo


UCL timu nyingi zimebaki majina

Naungana na zege la nyasi ,Mikel aongeze beki wa Kati mwenye uwezo wakucheza pemben na kiungo mmoja anayeweza kucheza LCM na DM, mrefu pande la mtu


UCL Kama nilivyosema ,timu nyingi Ni dhaifu

Sarri kocha wa Lazio kasema yeye anataka mterezo na kaomba mapema apewe Barcelona



Lazio manager Maurizio Sarri:

“I’d like to face Barcelona at UCL round of 16, honestly”.


Ninachoomba Mancity wanitolee ,Hawa wengine watanieleza vzr

Why mancity ,sipend kucheza na timu inayotaka na yenyewe imiliki mpira ,mechi mbili za mwaka huu zote zimeenda Kama 50/50

Lakini Hawa wengine watake wasitake watapakishwa basi kilazima

TUKUTANE WEMBLEY MWEZI MAY


 

Ukitazama hapo unaona Arsenal ina superior goal difference (12) kuzidi team zote kwenye hatua ya makundi kwa msimu wa 2023/2024.

Pamoja na kutokuwa na natural striker tumefunga magoli 16, magoli mawili pungufu kwa City mwenye goal 18. Tumeruhusu magoli 4 tu katika mechi 6 huku mawili yakitokea against Lens kwenye mechi moja.

Pamoja na injuries za defence unit (Partey na Jurrien) bado team inaonesha kuwa na good balance when it comes to attacking and defence.
 

Nadhani uko sahihi. Kinachotokea pale ni coincidence kati ya ‘mlipuko’ wa fedha za tajiri mpya na kuyumba kwa viwango vya team kama Chelsea na Liverpool last season.

Eddie Howe bado hana experience ya kutosha kusumbua Uefa, lakini hata wachezaji walionao wengi hawana experience kwenye Uefa.

Wakimaintain misimu kadhaa huku wakiendelea kujiimarisha kwa kuwa na structure na philosophy ya club wanaweza kuanza kuingia kwenye ‘elite clubs’ ila so far, binafsi nawaona kama ‘wapita njia’ ndio maana hata huwa siwajadili, wakionesha seriousness over time, then we can talk. Don’t feel embarrassed @Nyukasto, chance for discussion is open.
 


Sawa Mkuu, umeeleweka.

Ila upande wa Martinelli pamoja na kuwa na wachezaji wengi i.e Trossard, ESR, Reiss, Jesus pia anacheza kule.

Lakini kwa maoni yangu hatuna perfect sub ya Martinelli ule upande, yule dogo anakupa energy level ya juu sana na ndio maana asipokuwepo Zinny anastruggle na ikibidi Arteta hampangi kabisa.

Martinelli ana mchango mkubwa sana kwenye kukaba tukiloose possession, na speed yake ni key kwetu kuzuia counter. Ukimchek several times anatuokoa na counter attack sana.

Martinelli game tunazopigwa sana counter ule upande utaona hamalizi game atatolewa sababu anakuwa exhausted kwa kuzuia counter na bado adrive ule upande.

Hawa wengine wote wanafaa tukiwa na mpira, na bado miongoni mwao hakuna mwenye kumatch pace ya Martinelli hata mmoja with and without the ball.
 
Nyukasto hawez kupata nafas ya UCL tena kwasasa ,anamtoa Nani pale top 4

Kwasasa wapambanie kucheza Europa conference league
 
Sarri muhuni sana
 
Binafsi naamini huyu shabiki wa Newcastle ndio yule computerarsenal, na huyu inaonekana ni shabiki wa Man united, anachofanya ni kuvuruga hali ya hewa humu kwani inamfanya ajisikie raha, ndio maana anatafuta kila namna ya kuikosoa arsenal, hii inamfanya ajisikie vizuri sababu kuukubali ukweli arsenal inafanya vizuri ni maumivu makali kwa shabiki yoyote wa manunu.

Huyu alishasema Leicester city na Brendan Rodgers ni bora kuliko Arsenal na Arteta, kuna kipindi kachafua sana server humu kwa hoja za Conte na Spurs dhidi yetu, leo jahazi limezama anatafuta unafuu kupitia Newcastle na Eddie howe kesho ataleta hoja za Aston villa na Unai, kesho kutwa tujiandae kwa fujo za RDZ na brighton yote ni kutafuta unafuu.
Conclusion
Huyu Jamaa apuuzwe, ni mpumbafu.
 
🤣🤣🤣....Computerarsenal unamuonea tu...yule huwa ana criticize lakini kwny uhalisia huwa anakubali....ila hyu wa Nyukesto yy huwa anaandaa mafaili yake ya kujipooza na stats kibao ilhali Kila anacholeta hmu ni pumba tu akisaidiwa na Security guard Flano🤠🤠🤠..yule muangalieni tu na tutaenda naye hvyohvyo
 
Tukicheza kwa nidhamu na kuheshimu wapinzani wetu basi semi final hii hapa, afu huko lolote litokee tu. Wababe wakusumbuana nasi ni watatu, Man City, Bayern & Madrid.
 
Nakubaliana na wewe ,ila sio Computer arsenal

Huyu anadai alikimbilia Newcastle sababu alidai msimu wataongoza ligi

Ni mdogo kiumri ana akili za kitoto ,niliwahi jadiliana nae Sana ,nilipogundua Ni mtoto nikamkataa mazima

Akili yake ilikuwa inamtuma sababu Newcastle imenunuliwa na waarabu Basi itakuwa Kama Mancity ,asijue mpira haupo hivo

Cha ajabu Sasa Newcastle hiyo kwasasa haiwezi kunusa hata top 6 ,aliongea Sana na kuponda Arsenal kuwa tunaenda UCL kushiriki tu ,tulipopigwa na Lens ndipo akazidi zaidi,

Nilisema Newcastle Ni timu ya Vibe tu na fujo tu ,

Sasa hivi anaona aibu akija humu atasubiri sapoti ya watafuta furaha kina flano na yule Mkohoti

 
Huwa sisomi anachoandika huyu jamaa wa Newcastle, ila kwa kuwa ni kinganganizi kuandika humu that's why namuona kama computer and i entirely believe ni computer na inawezakuwa ni flano au yule mwenzie wa unyumbuni lkn all in all ni shabiki la manunu
 
Tukicheza kwa nidhamu na kuheshimu wapinzani wetu basi semi final hii hapa, afu huko lolote litokee tu. Wababe wakusumbuana nasi ni watatu, Man City, Bayern & Madrid.
Yah uzuri kuzuia tunaweza na kufunga tunaweza,Hakuna goli la ugenini,


Kila mechi ya kwanza tupige intensity ya juu tutafute mtaji wa goli 2+

Mechi ya 2 kufunga duka
 
Huwa sisomi anachoandika huyu jamaa wa Newcastle, ila kwa kuwa ni kinganganizi kuandika humu that's why namuona kama computer and i entirely believe ni computer na inawezakuwa ni flano au yule mwenzie wa unyumbuni lkn all in all ni shabiki la manunu
Kwasasa Kama wameshikwa Ganzi

Alikuwepo yule wa Chelsea ,Mkohoti ,timu yake inagombea kushuka daraja

Flano ,timu yake inasubiri miujiza

Huyu wa Nyukasto yeye alikuwa anaamini wataongoza ligi na kufuzu 16round

Na walikuwa wanasapotiana na kufanya kejeli


Kwasasa kila mtu kashika njia yake ,


 
Hii picha sio kwamba Bruno anasononeka kutokufika final ila anawaza ni lini atapata nafasi ya kucheza michuano km hii tena. Anafika mbali na kufikiria kwanini hakusajiliwa na timu kama Arsenal ili apate fursa ya uhakika kucheza Uefa na kulichukua kombe pia😁
 
Yah uzuri kuzuia tunaweza na kufunga tunaweza,Hakuna goli la ugenini,


Kila mechi ya kwanza tupige intensity ya juu tutafute mtaji wa goli 2+

Mechi ya 2 kufunga duka
Madrid wenye individual brilliance, bayern & city, naamini tukishikilia bomba na defense ya timber, tomi, saliba, gabriel, partey & rice tutatoa upinzani mkali sana. Kama tutafika final tutegemee kuona final moja kali mno ambayo haijaokea hivi karibuni
 
Kwanini Sasa walikuwa na mdomo na kelele Kama group Lao Lilikuwa gumu

Hilo group halikuwa gumu ,majina ndio yaliwatisha

PSG ,AC Milan wapo kawaida ,BVB hata kule Germany ana struggle na ndiye katop Group


Newcastle uwezo wao mdogo
Ww jamaa mda mwengine unajitoa akili hilo ndo lilikuwa group la kifo halafu ww unasema halikuwa jepesi
Ac Milan bingwa mara 7
Dortmund ana misimu karibu 6 anafika hatua ya 16 na ashafika hadi final
Psg kila mwaka yupo Uefa na alishacheza hadi final
Newcastle ndio timu pekee kibonde kwenye hilo group ulitemegea angefika wapi
 
Hizo historia ,hazichezi ,ingekuwa hivo Barcelona last season asingeenda Europa ,msimu huu wenyewe ilibaki kidogo wampeleke Europa

Hilo kundi unalosema Gumu ,AC Milan kaenda Europa ,BVB ndiye kavuka

Hilo kundi Newcastle alikuwa kilaza tu ,

Timu ilijizatiti haishindw kupita hilo kundi,

Huu ujinga wakucheza na historia ndio umemponza manjesta wamemshikisha mkia kund Lina Copenhagen na Galatasaray ambayo imeokota wachezaji reject


PSG hata kwenye Ligi yake wanamkimbiza Sana, BVB Hana makali hayo ,BVB alichofanya kwenye Hilo kundi kamtumia Newcastle Kama ngazi kakomba points 6 ,kaokoteza na kwa wengine akafuzu mapema , ila sio kwamba BVB Ni Bora Sana

PSG , AC MILAN,Barcelona zimebaki majina tu


Maurizio Sarri kasema anaomba apewe Barcelona awahi robo fainal, wewe unatuambia habari za historia
 
Sisi tunachofanya ni kutunza hizi risiti halafu baadae tuje kukumbusha maana mpira wa mdomoni haujawahi kuwa mgumu bali uwanjani
Tusubiri February hapo wala sio mbali uone hizo timu nyepesi zitakapo badilika ndo utaelewa kwann ile ni Uefa
 
Sisi tunachofanya ni kutunza hizi risiti halafu baadae tuje kukumbusha maana mpira wa mdomoni haujawahi kuwa mgumu bali uwanjani
Tusubiri February hapo wala sio mbali uone hizo timu nyepesi zitakapo badilika ndo utaelewa kwann ile ni Uefa
Mbona mliposema hatutafuzu hamzifukui


Yaan unakaa kabisa unasema lile grupu lilikuwa gumu

BVB alichofanya kashinda mechi 3 tu na draw 2 kaongoza kundi

Kabeba points 6 kwa Newcastle mliyekuwa mnasema atafuzu

UCL zaman ulikuwa unamkuta Ac Milan dume,Bayern Munich dume, Madrid dume, Barcelona ya Messi , Porto , Juve ya wanaume kweli kweli, Intermilan ya kina Zaneti , Hapo sijawataja watukutu kina Benfica, Sporting Lisbon , Galatasaray,


Ndio unataka kufananisha na UCL hii ya sasa ambayo Madrid ,GK wake Kepa arizabalaga, AC Milan hii imepelekwa Europa, Barcelona hii watu wanaigombania kucheza nayo round 16,


Yule Bayern aliyecheza na Manjesta anapewa nafas ya kulibeba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…