Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Wana magolikipa timamu

Ni arse8 tu ndio ana Golikipa anayepandwa na wazimu uwanjani

Achilia mbali wale nyumbu ambao kipa wao hana mikono
Kipa wa arsenal tunaemtambua ni Raya ambae ata kiungo anacheza kwa kiwango kilekile
 
Haina noma, ngoja tuendeleze hii dozi, heshima yetu tutachukua kinguvu
Kumbuka bado hatupo Ile form ya msimu uliopita
Form ya kupokonywa ubingwa na kuambulia patupu.

Wasindikizaji FC...
Oneni timu ya Dunia liver inavyobeba makombe yote.
 
Leandro ananikumbisha enzi zangu, kasoro tu ye anatumia vyema miguu yote, mie mguu wa kulia ndio nilikiwa nautumia, mguu wa kushoto ni wa kuoandia kitandank, namba nyingi nilikuwa nacheza kwa ufasaha mkubwa mnoo, namba yangu pendwa ilikuwa ni winga wa kushoto na namba 10, ila winger ya kulia nacheza, namba 9 nabonda japo sienjoy kusema ukweli. Namba 8 ndio mama yangu nikicheza namba 8, unashangaa, kuna game tulienda kubonda sehemu namba 6 yetu tegemezi ikaumia, nikamuomba mwalimu nicheze hapo, kulikuwa na winger wa akiba(sio tegemezi) akala wiger yangu, niliupiga mwingi siku hiyo, anayofanya partey ndio yalikuwa mambo yangu, mwalimu akabaki kinywa wazi. Pengo la namba 6 halikuwepo nikaupiga mwingi game inaisha mwalimu wa wapinzani ananiomba niwe naenda kupiga nao mazoezi.

Ndio maana mie mchezaji asiye mnyumbulifu, mchezaji mgumu mgumu tu, yupo kama tren alipoelekea ndio huko huko.. Simpendi hata kidoogo kwa kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…