Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ukweli Ni hivo
 
Burnley imekosa watu ila inacheza vizuri
Upuuzi mtupu. Timu inaweza kwenda mbele lakini inafanya ujinga wa ku recycle mpira kwenye half yao..

Tatizo lake Kompany anataka acheze mpira wa City, ndo inapokuja shida.

Nilizungumza muda mrefu tu, mpaka sasa timu zilizopanda ndio hizo hizo zitakazoshuka. Sio Luton, Sheffield wala hawa Burnley.. Labda waamue kubadilika.
 
Mbona Trossard nimemuona mazoezini
Kuna tetes Kuna injury,yule alivujisha injury ya Partey kabla ya mech na man u alishambuliwa Sana siku ile Maana Arsenal walificha waje waseme baada ya mechi ,akavujisha siku moja kabla na kwenye picha za mazoezi alionekana


Sasa Jana kasema Kuna injury imetokea ila hawez kusema atazua taharuki

Most wameunganisha dot wanasema Ni Trosaard

Session ya mwisho Kama hajaonekana, lakin Kuna baadh ya session kaonekana,Sasa hatuna uhakika Kama Ni kweli Ni session za Jana au juzi ,Maana kwa Partey ,Arsenal walionesha picha kabisa yupo mazoezini
 
Kama kaumia basi mchezaji wa kucheza eneo la pembeni ya uwanja tena akatoa impact kubwa ni Nelson hao wengine Arteta asilazimishe lazimishe tu
Nelson namkubali kwa sub aisee, asubiri jumatano CARABAO Cup,

Kwann asianze Jesus Kama LW , Kai Kama CF ,
 
ID yako ya Aaron ndiyo imekaa kiuchambuzi nguli hii ya MC hamis imejaa mipasho
Hamtaki kukubali ukweli

Against Burney mnakuwa dominated hivi ,mnasubiri magoli ya kuvizia ,

Mtakuwa na Msimu mrefu Sana

Hata hapa tatizo ni Grazzer?

Arsenal ikifikiwa kuwa dominated na kina Luton, Burney, wolves Basi pale EMIRATES kocha hatakaa kwa amani

Muulize Unai Emery alipotuletea Mpira Kama wa 7hag


Hivi mnawezaje wenzetu kuangalia Mpira Kama huo na bado mnamtetea kocha wakati Ni wazi kabisa uwezo wake mdogo kufundisha modern football

 
Haiwezekani kila siku nasema nketiah na jesus ni daraja tofauti kabisa, nketiah afikie huko ajitoe na ajitume kimazoezi na kujifunza kwa kiwango alichofanya cr7 kuusaka ubora wake.
 
Kama dirisha la January watampata Toney na winger kama Mbuemo hawashuki.

Na kweli mpira anaoucheza ni very modern ila hana watu wa kumpa anachotaka
 
Watakaoamua ushindi leo ni defense.

Katika timu zilizo nafasi ya 1 hadi ya 4 ni Arsenal pekee ndiye tumefunga magoli machache. Spurs imetupita pia kwenye magoli ya kufunga na kufungwa na Spurs haina centre forward.

Hii ndiyo kusema Ange amefaulu kuyagawa magoli na mid yao mpaka forward inaweza kuscore. Spurs ipo kwenye form nzuri, timu inacheza kwa kudominate game na kocha wao siyo mbaya.

Jinsi yeyote atakavyodefend ndivyo ataamua ushindi uende kwa nani. Bahati na miujiza weka pembeni. Nketiah ni clinical finisher ila link up play yake siyo kubwa, Arteta anaweza muanzisha huyu ili asubiri wakina Romero miguu ichoke ili kuingiza Jesus, Vieira, Tomi n.k.

Game itakua physical. Kai akiwepo at least waliopo wamuangalie akianza zile instinctively run wampelekee mipira, Trossard na Rice wakae naye karibu kumpokelea mipira.
 
Ligi imeanza tumecheza na wapaki Basi

Leo tunaocheza nao Ni kama PSV walifunguka zaidi


Ukitaka kufunguka kwa Arsenal hii Kila la kheri

Spurs wanafunguka ,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…