Charles_watts kutoka Goal.com kuhusu Ethan Nwaneri:
“Ethan Nwaneri, Arsenal walipambana sana abaki msimu huu wa joto, Walifanikiwa kumbakisha.
Arsenal imeweza kumfanya akubali mkataba mpya na mkataba wa kikazi(professional contract) mara tu atakapofikisha miaka 17 na atasaini hilo."
"Hizo zitakuwa habari njema kwa Arsenal kwa sababu alionyesha kwa Vijana wa U21 haswa kwa nini alifunga hat-trick akiwa na umri wa miaka 16, sio mafanikio mabaya kama vile Arsenal walivyoifunga Leicester. Nadhani maendeleo ya Nwaneri msimu huu yatakuwa ya kuvutia sana.
Arsenal wana mipango mikubwa kwa ajili yake.” wanamuona akifika mbali .
Mikel Arteta anamuona akienda mbali sana, alimpa nafasi kama kijana wa miaka 15 msimu uliopita vs Brentford, na hiyo inaonyesha jinsi anavyomkubali.
Kama nilivyosema, Arsenal walipigana sana kumbakisha kwa sababu kwa muda mrefu, ilizingatiwa kuwa alikuwa anaondoka.
"Maajenti wengi ambao nilizungumza nao walikuwa na hakika kabisa kwamba hayupo na alikuwa anaenda kusaini Manchester City au Chelsea.
Lakini Arsenal waliweza kubadili fikra zake, wakarudisha nyuma mawazo yake kwa Arsenal na kukamilisha dili hili.”
(YT kupitia HITC).