Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kumbuka pia jinsi hayo magoli yalivyofungwa.

La kwanza, mpemba Rashidi alipiga move kali na shuti amazing la nje ya box akapata goli.... against the run of play. Na kama sikosei, Chidi ndiye alikuwa mchezaji aliye mbele zaidi Kwa Manyumbu, huku wengine wamepaki basi Kwa hofu kubwa wakijiandaa kujilinda na shambulio tulilokuwa tunawapelekea, hivyo hakuwa na msaada. Tukapoteza mpira, mpemba akafanya yake. Lilikuwa goli Bora sana Kwa kweli.

La pili ndilo lilifungiwa ndani ya box. Na lenyewe pia lilikuwa la kimiujiza miujiza hivi. Yaani Kona imepigwa, ikawa cleared kidogo tu ndani ya box, tukaanza kujipanga kupiga counter moja hatari sana, mara akatokea Martinez na diving header ya mpira ulio kima Cha mbuzi, mpira ukarudi juu na ku-loop. Golini Gabriel almanusra auokoe ila ukamchuna kichwa kidogo na kuingia wavuni. Bahati juu ya bahati.

Nakumbuka pia goli la Saka lilitokea nje ya box. Hata shangilia yake ya kukimbilia corner flag kuweka kidole kichwani, aliifanya kumjibu Rashidi ambaye awali alishangilia hivyo goli lake.

Naona hizi takwimu zinatuonyesha tu kuwa sisi tulikuwa hodari Kwa kutawala mashambilizi na yalitufikisha sana ndani ya box ila nyie mlikuwa vizuri kuyazuia na kupona chupu chupu. Nyie hamkutawala sana mashambuilizi hivyo hamkuingia sana ndani ya box ila mlipata magoli mawili mazuri sana ya kubahatisha.
 

Edu na Vinai wawe wakali kidogo kwenye mauzo. Najua Edu alisema tuko tayari kuvunja hata mikataba Ili wachezaji tusiowataka na wasiotaka kuendelea kuitumikia timu wapunguzwe wengine waje. Ila 35 + 15 naona tunajipunja. Weka 45 + 5. Weka buy-back na sell-on clauses.
 
Halafu unaweza Kuta hiyo add ons yenyewe masharti yake ni magumu kwelikweli...unaweza Kuta inasema afikishe goli kiasi flani kwa misimu kadhaa hta wakti mwingine na ubingwa juu....yaani add ons huwa siyo hela ya kuhesabia kbsa
 
Halafu unaweza Kuta hiyo add ons yenyewe masharti yake ni magumu kwelikweli...unaweza Kuta inasema afikishe goli kiasi flani kwa misimu kadhaa hta wakti mwingine na ubingwa juu....yaani add ons huwa siyo hela ya kuhesabia kbsa
Tumekuwa na shida kubwa kwenye kuuza kuliko kununua
 
Man united watakuwa na mid brutal saana this season ukiangalia wana
casemiro
Fernandez
Mainoo
Erikson
Na sophian amrabat.
Mid nzuri na itawasaidia sana kwenye big matches kama za city,liver na arsenal.Tatizo la mid yao ni kukosa akili tu ila nawaona wakiwa washindani kweli.

Secondly wamerudi kusajili wachezaji wa man united philosophy.Mara nyingi wanatumia akili 20% na nguvu 80%.
Arteta tuletee mid moja muuaji na awe anaweza kucheza lone 6
 
Wataje wachache unaopenda kuwaona wakinunuliwa
Aisee namhitaji mnooo caisedo.rice hajaondoa nafasi ya zubimendi au lavia. Sadly ndani ya team kwenye academy sijaona a potential product kwenye eneo la DM wakucheza lone 6

LCM na RCM tunao wengi mno ila wote wana offer kitu kilekile.angalau trossard akichezeshwa double pivot ya 8 anaoffer flexibility kubwa.
 
Caisedo price tag kubwa...£100 million...Chelsea mpk leo wanavutana na Brighton...Zubimendi nahisi ana kitu kinaitwa home sickness bado hajakuwa tyri kucheza nje ya spain...Lavia naye inaonekana price tag yke kubwa maana hata Liver wanamhitaji sana ila wanaona bei ni ya kupigwa kwhyo wana bargain...Rice anachezeshwa LCM lakini kiuhalisia ni DM...mi naona eneo lenye uhitaji ni RW ila viungo so far somehow tuko sawa...ila with arsenal kitu chchte kinaweza tokea maana hata kipa tumeshtukizwa....kwhyo U never know
 
Inter kafanyiwa umafia ,Sasa njia nyeupe waje kwa Balogun

(
) Gianluca Scamacca to Atalanta is a DONE DEAL in a deal worth €25m fixed fee, €5m easy add ons; 10% sell on clause also included.
#Atalanta

(via @FabrizioRomano)
 
Safi....ukilialia watu wanachukua....Inter na Juve wanajifanya wanaijua hela sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…