Interlacustrine R
JF-Expert Member
- Jan 22, 2022
- 8,069
- 15,754
Dunia haiko hivyo Ndugu, usishangae kesho ungali hai Arsenal FC ikatoka nyuma na kuwapita Man City tena mbali sana kirekodi kwa kubeba kombe hilo hilo la UEFA CL.
Mbona Man City yenyewe mwaka huu 2023 haikupata ushindani kiviile maana klabu kubwa nyingi sana zimeshuka kiuwezo zikiwemo Buyern Munich & Chelsea FC sababu ya kukosa umakini wa bodi kuamua kukaa na Makocha bora kwa muda mrefu baada ya mabadiliko ya ghafla kabla hata ya wiki 2 kupambana hatua za robo fainali na Real Madrid na Man City?
Pia tambua Man City imemgharimu zaidi ya miaka 7 tangu 2016 pamoja na kuwa na Kocha bora na uwekezaji mzuri kifedha kusajili Wachezaji bora kila mwaka na kufanya vizuri kwenye EPL & FA.
Pesa + Kocha bora na Wachezaji wazuri + Bahati (Upepo) = Makombe/Mafanikio.
Imagine 2006 Arsenal FC ilimtangulia Chelsea FC kucheza fainali za UEFA CL na haikubeba hilo kombe ilihali Chelsea FC ilikuja nyuma ya Arsenal FC kucheza fainali za UEFA CL 2012 & 2021 na zote ikabeba.
Nani alijua Chelsea FC itabeba hayo makombe mara 2 hizo kulingana na kikosi cha Wachezaji iliyokuwa nao dhidi ya timu pinzani za Buyern Munich & Man City?
Je Barcelona FC ya akina Xavi, Iniester, Puyol, Messi ilivyokuwa moto na kubeba UEFA zaidi ya mara 3 tokea 2006, nani alitegemea Real Madrid itabeba zaidi ya mara 5 tokea 2013?
Jifunze kuwa na akiba za maneno (future life is unpredictable/uncertainty).
Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app