Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Hii City ndiyo wanafiki walikua wanatuchonganisha nayo.

Aliishindwa Ferguson, Wenger, Klopp, Mourinho wanakuja kumsakizia Arteta hata kudeal na pressure hajamaster na kikosi kipo nusu.

Kwa position aliyekua arsenal ingekuwa newcastle,brighton, man utd, hata brentford saivii wangekua wanajiandaa na sherehe za ubingwa lakini uliza arsenal na mashabiki wake saivi sio arteta sio hamis sio aroon wote wameshika tama wako kama vituko hata mbele ya relegated soton
. Wanajiuliza hivi hawa arsenal ndo timu iliyochaguliwa kua kituko cha epl ama
 
Labyrinth 84 endelea kupiga spana hizi Kima zisizojielewa.
Tunavyowaambia kila siku humu kua Arsenyani sio timu, hii ni Academy ya kukuza watoto, halafu wakishaanza kukomaa wanaenda zao sasa kutafuta timu za kucheza hawataki kuelewa.
 
Go back to school brother, watoto km nyie huwa napiga block tu.
 
Go back to school brother, watoto km nyie huwa napiga block tu.

arsenal is for boys only!! Hakuna mtu mzima anashabikia arsenal.. kumuita arteta genius ni kulikosea heshima neno lenyewe though so far kwa timu ilipokuepo mpaka hapo ilipo! Arteta hadaiwii chochote!
Block za nini lete facts nitajie game 4 arteta alizokuja na approach tofauti mimi nikutajie game 10 pep alizokuja na different approach!! … i have been an arsenal fan for 20 years dont call me a child! Lete hoja na si viroja
 
Nyie wenye mmejipata msimu mzima mmetoka patupu kweli fans wa arsenyani mmedata sio bure.

Mafanikio yenu mwaka huu ni kwenda uefa tu nako mnaenda kutia aibu mnataishia makundi kwa wachezaji wenu wa mafungu mafungu.
Hii ni project brother, ndio kwanza tupo phase 3/ 5. Sisi kazi yetu kuwafunza Mpira nyie manyumbu. as long as Mikel Arteta yupo hapa basi Mtaujua tu.
 
Unaangalia mechi ya brighton muda huu au unajifurahisha?

Nitarudia tena.

Jitahidini kuangalia mechi.
 
Nilikua nawaambia juzi kwamba Brighton anaonyesha classic symptoms za mid table team

Angalia mechi yake kuanzia Notingham mpaka leo.

Anafungwa na Nottingham.

Anaenda kumfunga nyumbu.

Anaenda kufungwa 5 na Everton.

Anaenda kumfunga Arsenal.

Sasa hivi anaongozwa nne na Newcastle.
 
Kwa asiyeelewa anaweza niuliza kwanini nasemea sana hii mid table attitude ya Brighton. Ni kwakua timu za hivi zikiwa zinashuka daraja unakua haujui it takes just one wrong step for all else to fail

Soton wanashuka daraja msimu huu, timu ambayo ilikua inaweza shtua kwa matokeo na wrong step kwao ilikua nini? Waliacha aggressive defending. Just that imetosha kuwashusha.

Timu za hivi hua hazina firm footing in the league. Angalia Leicester. So Brighton itauza wachezaji na ikilemaa mpaka kocha ataondoka ishu itakuja pesa watakazopata zitawafanya wawe giants? No.

So misimu miwili mbele Brighton akiwa anashika mkia haitakiwi kukushtua. Dalili ni hizi unazoona hapa.
 
Arsenyani na Brighton zote zinaonyesha classic symptoms za mid table teams.
Brighton yeye anakomaa na timu kubwa anaishia kugongwa na timu ndogo, Arsenyau nae misimu yote ukiacha huu anaenda vice-versa anakomaa na timu ndogo halafu anagongwa na timu kubwa, miaka zaidi ya 8 akashindwa hata kunusa top4.
Arsenyo na Brighton zote ni dugu moja (mid table teams) tofauti yao ni vile Arsenyeto msimu huu amebahatika kuingia kwenye top 4.
 
Kawa nominated coach of the season kukosa ubingwa kwanini iwe maneno mengi kwa arteta kikosi kimoja pep hata akibadilika ana watu wa kucheza kila formation anayotaka kwa quality ile ile..
Na mpendea arteta anajifunza na kubadilika na kutafuta solution hivyo naimani nae bado na Wala Mimi hanidai namsubiri tu nione apraoch yake ya usajili kwendea champions ligi ndio ntaanza pia kumjaji nategemea robo au nusu ya champions ligi kwetu itakua achieve kubwa msimu ujao then misimu unaofuata kufuta kila kombe mbele yetu tutakua na timu ya maana na kikosi imara after next season

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Naiombea kushuka kabisa daraja Kama kilichowakuta soton hawa bright misimu miwili wanavuruga matokeo yetu muhim sijui kwann

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Nyie mpira haumjui nakwambia arseml kua pale sio bahati subiri next step step uone saivi Ni clearance ya kikosi inafanyika kinasukwa kitu cha CL nusu fainali hii hapa Kama sio kuchukua kabisa pl tunafunga na point 97 ,98 ataemaliza juu yetu bingwa maana kila msimu ndio zitakua point zetu hizo Kama saivi tumepiga 80+ hivyo endelea kula mtori...

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Msitegemee kabisa msimu ujao mambo yatawaendea vizuri kama msimu huu.
Ilikua ni one season wonder, Ucl mnaenda kuchomolewa kwenye makundi kisha mnarudi tena Europa halafu msimu ujao kama kawaida yenu hio top 4 mtaishia kuisikia tu.
 
Xhaka anaweza kuondoka mwisho wa msimu huu. Nimependa jinsi safari yake na Arsenal imepita milima na mabonde na Sasa anaondoka Kwa amani na upendo mwingi kutoka Kwa mashabiki
arteta now atakuwa anakuna kichwa kumpata mchezaji atakaye timiza majukumu walau nusu
tu ya alivokuwa xhaka..

kwa wacheza waliopo ni ama abadili namna ya uchezaji eneo la kati la uwanja ama akubali tu
kuingia sokoni tna.. mana fabio sio wa kumtegmea kucheza eneo la xhaka.
 
Hii ni project brother, ndio kwanza tupo phase 3/ 5. Sisi kazi yetu kuwafunza Mpira nyie manyumbu. as long as Mikel Arteta yupo hapa basi Mtaujua tu.
Mnatufunza mpira gani mlikula OT chuma 3_1 kwa moja tukisema mmeishiwa akili mnaona tumewakashifu.
 
Arsenyani ni takataka na uchafu yani timu inajisifia kucheza mpira miaka nenda Rudi lakini hata ka ueropa hakuna hafu tukisema ni kikundi Cha wauni mnanuna.

Nyie tushawaambia hapa nyie ni under dog Sasa under dog na mpira mzuri wapi na wapi nyie mnatakiwa kupata kocha Aina ya Mourinho ili muweze kuonja hata radha ya ueropa

Hii ni game ya jana kati ya Roma vs Leverkusen

Roma ajapiga hata shot moja langoni kwa adui lakini huyo yupo zake fainali.

Mourinho alishasemaga hivi na mnukuu.

Attacking wins you games, but defending wins you titles. JM
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…