Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Pep alikua anajibu swali kutofautisha uchezaji wa City na Wa Arsenal akasema City wanapitia katikati wakati Arsenal tunapitia pembeni na kweli tukiangalia timu yetu baada ya maneni yale timu kama zimetujulia zinakaa nyuma zinatuacha hasi kwenye final third wanakaba nafasi za pembeni mambo yanakua magumu kiukweli mechi ya kesho tubadilike tuliona mechi ya FA, AKE alikua anatembea na Saka angalau odegard akuwepo kwani wote huwa wanaenda pembeni waki alternate na kukabika inakua ngumu ila tusubiri tuone yote kwa yote Arsenal tutashinda mechi ya kesho
 
Mechi ya kesho tunashinda! Japo itakuwa mechi ngumu sana!
 
Arsenal ndoo
Halaand kiatu..

Mda utaongea
 
Nimeangalia mechi zenu tatu zilizopita Martinel amefail, Saka amefail. Saka anajiona star hakabi anasimama kule pembeni anasubiri apelekewe mipira, shida ni timu haina namba 7 mwingine makini ambapo Saka akizingua anatolewa faster kwa hiyo anarelax anajua hamna cha kumfanya. Tafuteni option nyingine. Kwani hamna hata watoto wa academy huko muwapandishe!!
 
Duuuhuu,, mku hivi pale man u,, nani atamuweka saka njee kwenye ile position

Et unasema saka hakabi,, fullback both, wingback both,
 
Arsenal atamaliza ligi akiwa na point 92.. atapoteza mechi nne na kutoka sare mechi tano. Mpaka sasa ameshapoteza mbili na sare tatu. Amebakisha sare mbili na kupoteza mbili.

Sasa kama kuna timu itaweza kuzidi hizo point basi itapewa ubingwa. Timu zinazoweza kusababisha arsenal akafungwa au sare ni Man City ugenini, fulham na liverpool zote za ugenini na brighton nyumbani.

Mashabiki wa arsenal waendelee kutembea kifua mbele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…