Arsenal (The Gunners) | Special Thread

FOOTBALL YA ARSENAL NI MIXA BASKETBALL


Najua unajiuliza sana hii Nini?

Kwanini wachezaji wa Arsenal Wamekuwa na aina hii ya ushangiliaji kama wanatumbukiza mpira kwenye kikapu?

Mpira wa miguu ni kuhusu UBUNIFU.Makocha mnasoma wote mnapata License A au Pro License.Lakini kinachoweza kuwatofautisha ni UBUNIFU.

Na hapa MIKEL ARTETA ameuleta mchezo wa Mpira wa kikapu kwenye kiwanja chake Cha mazoezi

Ukienda pale London Colney "Uwanja wa Mazoezi wa Arsenal" ukisema kuhusu "Basketball rule" Kila mchezaji anaelewa unaongelea nini.

Nahodha Martin Odegaard aliulizwa kuhusu ushangiliaji huu wa Basketball
anasema "Ni kitu huwa tunamzungumza sana kwenye Mazungumzo ya team.Tuna Kanuni tunazifanya ni kama zile tu Basketball

Basketball rule ni nini? Kwenye Basketball ni kuhusu kashambulia sana ndo msingi.Kutengeneza mazingira ya goli kufunga ni Muunganiko wa ufundi binafsi na team.

Kwanini Mchezo wa Mpira wa Kikapu? Na sio tennis na michezo mingine? Anasema ni kwasababu Basketball Kuna vitu Vingi inafanana na Football

Kwa mfano ambacho Basketball na Football wanashea ni "Transitions na turn overs.Na ili transition ifanikiwe Kuna vitu 4 lazima vifanyike kwa usahihi

Kwanza ni kuwa na nidhamu ya eneo.Lazima uwe kwe eneo Sahihi ili tujue wapi tunakuwekea mpira.Pili , Compactness yani kuwa kwenye umbali Sahihi ili iwe rahisi kusafirisha mpira.Tatu, Organization,yani lazima kuwe na Muundo kuwezesha shambulizi.Nne,maandalizi ya nini Cha kufanya kama shambulizi likifeli.

Na kwenye basketball mara nyingi transition ikitokea lazima mpira umalizkie kwenye kikapu.Hii utaona Arsenal wakishapora mpira wanaondoka Kwa Kasi na lazima shambulizi limazike kwa Shuti Golini.

Kitu kingine ambacho Basketball na Football wanashea ni michezo ya Uvamizi (Invasion) .Yani inahusisha team moja kuvamia goli la timu pinzani na kufunga Goli au vikapu , Lakini pia kumzuia pinzani asifunge magoli au vikapu zaidi yako katika muda fulani wa mchezo.

Mikel Arteta amediriki Kujiunga kwenye group la Whatsapp la makocha wa Mpira wa kikapu nchini Marekani NBA ili Kupata uelewa zaidi wa namna makocha wanaziandaa team zao

THIS IS FOOTBALL MADE IN ARSENAL


wilson oruma
 
Gunners Bado kuna mtu ana wasi wasi na Eddie ENKETTIAH kuziba pengo la Gabriel Jesus??.

Mie kusema Kweli sijui wasi wasi wenyewe unatoka Wapi

Lakini pengine ni kawaida ya Mashabiki.Msimu uliopita walinuna wakati Lacazette anawekwa nje anaanza Eddie Enkettiah

Eddie Enkettiah akafunga goli 5 kwenye Mechi 7 wakasahau na wakaanza kuimba jina lake.


Akaongozewa Mktaba wakafaurahi kinoma, Saivi amepewa nafasi anaonyesha kwanini aliongzewa Mktaba.



Halafu kuna option za ESR kucheza False 9 au Gabi Martinelli kucheza kama 9 kama ikishindikana ambayo ni asilimia kidogo, Kuna ongezeko la Trossard ambaye anapiga Miguu yote,amejaa Skills za hatari.

Kwangu Kimbinu na Kiufundi Eddie Enkettiah ni perfect replacement ya Gabriel Jesus

Anaweza kuunganisha team vizuri (Link up play)


Ni focal point mzuri


Ni outlet mzuri tu


Ni mzuri Kwenye 1v 1


Ni mpambanaji mzuri tu


Ni mmaliziaji mzuri tu


What else GABI JESUS anafanya EDDIE ENKETIAH hawezi?

Kitu Bora ni kusajili watu wa kuboresha Lile eneo la Kiungo ,

 
LUCA MODRIC PLAYING CENTER BACK??

Is that you William Saliba?

Binafsi nilifahamu Kwamba William Saliba ni beki mzuri, Lakini kwamba ni mzuri kiasi hiki? No ananishangaza Kila siku

Uwezo wa SALIBA akiwa na mpira mguuni ni Dunia.Utulivu wake na Mali mguuni ni Kila kitu.Kwenye eneo ambalo Mabeki wengi wanapaniki Saliba kama yupo kwenye FRIJI


Ana uwezo mkubwa kwenye kusogeza team juu (Progressive).Saliba anaweza kugeuka na mpira kwenye Upande wowote ule (Turning on the ball)

Dominant

Powerful

Slick

Calm

Quick

Clever


HE'S GOT IT ALL AKIWA NA MIAKA 21 TU
 
Mikel Arteta on Why alimchamgua Martin ODEGAARD kama Nahodha wa Arsenal?

MIKEL ARTETA "Kwasababu yeye ndo anaweza kutafsiri kwa usahihi kile ambacho nataka kitokee uwanjani"

Unaweza kurudia tena kusoma hayo Maneno ya MIKEL ARTETA? Fanya hivyo kwa afya yako.

Mikel Arteta pia ndo alimchagulia Martin ODEGAARD jezi namba 8 ambayo alikuwa anaivaa yeye alipokuwa Nahodha wa Arsenal chini ya babu Wenger.
 
Kumbe unataarifa kwamba Saka ni chezaji kubwa duniani🤣🤣🤣, itakuwa anakuumiza sana hadi unazusha taarifa za kuhitajika Madrid, unadhani katokea America ya Kusini? Tuliza kipira ndugu
 
Kumbe unataarifa kwamba Saka ni chezaji kubwa duniani
, itakuwa anakuumiza sana hadi unazusha taarifa za kuhitajika Madrid, unadhani katokea America ya Kusini? Tuliza kipira ndugu
Huyo jamaa hajui lini timu yake itarejea, Summer walitumia €300m akatamba , now wapo 10th, so lazima awe anaumia
Toka Arteta anaanza hii project huyo jamaa amekuwa akibeza , Juzi Arsenal hatuwezi kumtaka Caicedo,
Gafla ikatumwa bid ya £60m , anasema tunachofanya Ni mbwembwe kutengeneza A & B teams ,
Arsenal walimpeleka Arteta kwa Pep akajifunze vingi ikiwepo Depth of squad ,

Moja ya Depth ya kikosi Ni kuwa na mchezaji anayecheza nafasi zaidi ya 1, tumeliona Hilo kwa Arsenal ,tuna wachezaji karibu 6 wanacheza nafasi zaidi ya 1
 
Ni suala la muda tu ataelewa, mwache akaze shingo.
 
| @FabrizioRomano:


“Brighton insist they want to keep Caicedo, so it’s not an easy one. Arsenal are pushing on Caicedo deal also on player side.” #afc
Hili deal la Caicedo ni kama Chelsea tumetulia hivi yani tangu tupeleke offer ya kwanza tetes zikawa zimeishia hapo.

Now naona tu tetes za Enzo zikirudi tena
 
Partey mnyumbulifu saana, mali inakuja anatizama kwenye side mirror, anafamya kama anapasia, anageuka kwa adui, anacheza one, two, anapiga through ball.. Mie napenda kiungo mnyumbulifu.
 
Kwangu bado Gabriel jesus ni bora zaidi. Naombea arudi haraka, nadhani kukosekana kwake kunamfanya hata martinelli asicheze vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…