Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ukweli mchungu, City ndio timu ya kuifunga kwa sasa. Experience ya city ni second to none, uwezo wa mchezaji mmoja mmoja ni next level, squad depth kwa kila position ni nzuri. Tuwe wakweli, tunahitaji kuifunga City ili tuonyeshe uwezo wetu na dhamira ya kuchukua epl.
 
Hongereni Gunners,,,,

Msimu huu wakuwazuia alikuwa aidha sisi ama city, sio mbaya tumegawana hizo alama sita! Kazi kwenu mpambane na citizens!

Saka, Yuko vzr Sana yule chalii, bad luck timu ya taifa hapati minutes za kutosha !

Zinchenko mtu pia,,,,

Kipa wenu ana mawenge mawenge,,,,

White Jana ulimi nje, rashy alimuendesha awezavyo, na ile yellow kocha akaona Bora amtoe ,,,

Martineli , bado aisee hakuwa threat kiivo, !

Partey pia hakuwa na game nzuri Jana,,,, goli letu la Kwanza lilianzia kwake, tungekuwa na Casemiro nadhani ingekua battle nzuri kwenye midfield !

!!!!! Mngempata Mudrky mmngetisha Sana aisee, Bora alienda Chelsea
 
Kuna huyu kiumbe hapa for short term plan na anauwasha kisawasawa nadhani uliona mwenyewe
 
Katika hao watu wanaojisahau Arteta na wachezaji nao wamo au?
 
Acheni kukufuru nyie viumbe,
Umfunge Man Utd zaidi ya goli 3 kwa kikosi gani hasa mlichonacho?
Hilo goli la 3 lenyewe refa aliamua kuwapa tu ili mpunguze maneno maneno, maana kabla ya mechi mlikua mmeshaanza kumtuhumu kua atawabeba united.
Sijui mpira ulisimuliwa offside ipo wapi,
zilikuwa Sita Eriksen kapunguza mbili Degea moja na mwakani ukija tena na kugonga kama nilivyo kugonga miaka mitano mfululizo.
 
Nilisema humu ,Ni finisher mzuri,

Chini ya wale watu 10 ,atafanya vzr tu,

Tatizo Eddie amecheza Sana Cups ,ligi alipata nafasi mechi 8 msimu uliopita mechi za mwishon akafunga goli 5, Lakini watu baaadhi hawakumuamini

Nketiah Ni finisher mzuri kuliko hata Jesus ,ila tu in terms of full package kazidiwa na Jesus.,maana Jesus Hadi leadership uwanjan na nje ya uwanja yupo vizuri , kwasasa kaumia Lakini anashinda dressing room anahamasisha.

Nketiah Ni finisher mzuri pia kuliko hata Darwin Nunez ,

Ni vile sababu hatujamnunua Ni mtoto wa academy
 
Inakera mtu akiwa hatumii logic halafu anajiona yupo sahihi
 
Mikel, na wachezaji wa Arsenal wakiulizwa maswala ya ubingwa, wanasema Wana focus game inayokuja

Upo sahihi

Huku mashabiki wa Arsenyani focus yao ni: -
Arsenal Ndoo
Haaland kiatu

Aaron Arsenal mpe basi japo pole ndugu yako allypipi maana ule mpira mliopiga kuanzia dakika ya 70 ilikua ni utatoa hutoi mpaka tukaamua kutoa ki roho safi tu.
Hii chini ni selfie aliyojipiga ndugu yangu allypipi baada ya dakika 90.
 
Hizi ninaona ni blah blah tu, liverpool ilibeba epl na ucl ikiwa na kikosi kimoja.
 
Sasa hivi kuna baadhi ya mashabiki wa Arsenal humu ndani mmeanza kua matured na kuanza kujielewa, tatizo kuna mashabiki wengi humu hua hawapendi kabisa kusikia jambo lolote negative kuhusu wachezaji, kocha na timu yote kwa ujumla.
Wao muda wote wanataka kusikia mambo matamu tu na shabiki anaejielewa akijaribu kuzungumza kuhusu uhalisia wa mambo anaanza kushambuliwa kwa matusi, kebehi na kejeli na kuonekana ni mamluki.
Ukienda kwenye majukwaa ya Chelsea, Man United na Liverpool unaona jinsi mashabiki wake walivyo huru kukosoa iwe ni mchezaji, kocha au timu kwa ujumla pasi na kushambuliwa na mashabiki wenzake.
 
Naona kuna baadhi ya mashabiki wanatumia muda mwingi kujitia wasiwasi kuhusu city mara April mara kikosi kipana..

Inabidi tuelewe huu ni mpira na kila kitu kinawezekana iwe kupoteza ama kushinda tunachopaswa sisi kama mashabiki na wapenzi wa arsenal ni kufurahi timu yetu kadili inavyopata matokeo haiwezekani muda huu wa furaha tujitie simanzi ambazo hazipo..

NB: kwakuwa city hana kibali cha kushinda mechi zote za ligi, Arsenal inaweza ikapoteza mechi zote vs city na bado ikawa bingwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…