Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ligi ya Ukraine
 
Kutoka ligi dhaifu ya Ukraine kuja kucheza ligi ngumu EPL na kuperfom kuna changamoto kidogo,,,, thou inawezekana pia

Kuna baadhi ya wachezaji watahitaji muda wa kuadapt na wengine hawahitaji muda wakifika tu wanakiwasha!

Hii ligi Ni competitive sana, wengi tumeona wakuja kutoka huko farmer's league na kuchemka vibaya mno !

Mudryk Ni mchezaji mzuri Sana, ana skills za kutosha, stats zake Ni nzuri pia ! Shida Ni moja tu Moto anaouwasha kule ataweza kuuwasha the same/above akija EPL ?

Usajili Ni kamari, wacha tuone, maana mzigo mnaoutoa Ni mkubwa 70m plus adds on, na hapo mmesubmit tu, shaktar hawajakubali,,,, wanawatega muongeze !!!
 
Watu washaanza rivals kuumia, "mudryk anacheza ukraine, mudryk bla blah"

Mchezaji amecheza UCL mpira unaonekana, mchezaji mzuri ni profile yaani anafit vipi kwa system inayotumika, ukiona mchezaji anazingatiwa ligi aliyotoka kinachoangaliwa ni his tactical education from youth development, wala si kwamba huna kipaji, kipaji kinaonekana either unatoka Kenya au Congo. Mudryk uwezo anao biggest concern ni kwmb amekuwa profiled kuendana system tunayotumia,? Mikel Arteta hajawahi sajili mchezaji wa €70m tangu amejiunga Arsenal, ni mmoja tu alimuhitaji Vlahovic kwa bei zaidi ya hiyo. Mudryk nasikia amekuwa developed as #8 kwenye level za chini. Yupo explosive ni transition threat. Binafsi napenda kasi na elite ball control cuz napenda soka fluid na goli za chapchap.
 
Je Kuna wachezaji mbadala ya Mudryk au wa nafasi zingine tunaowasaka dirisha hili? Naona kama tunamfukuzia mtu mmoja tu na wenyewe wana kaza mpaka nadhani mwishowe hatutasajili mchezaji yeyote.
Mudryk is a deal done, hofu yangu ni replacement ya Partey huyu ndo mwenye timu yake anahitaji mtu wa kucover nafasi yake
 
Naamini Rice anakuja nxt summer, ningewaza locatelli lkn sidhani km tunaweza kurudi nyuma.
Viungo wavunja kuni ,siwapendi ,napenda DM Kama Partey ,Rodri , Gorginho , FDJ ,

Nipe ubora wa Rice kwa mpira hasa huu tunaocheza ambao unahitaji DM awe na accuracy kubwa Sana ya upigaji pass kuliko kufanya tackling
 
Kwenye transfer market zipo aina mbili direct/indirect contact na ndiyo maana kwa Mudryk , Arsenal wanafanya indirect contact transfer market. Lakini pia Arsenal wanaangalia vigezo vingi hawajaingia kichwa kwenye huo usajili.

Mchezaji mwenyewe ameamua timu anayotaka kucheza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…