Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Msaidizi (chakula) ya bosi
 
Wanaume tumepangwa na Porto, nyie mpo na Praha 😂😂😂 Kweli mpira ni akili
 
Mara ya mwisho Slavia Praha kufungwa ni tarehe 10/12/2020 Arsenal mara ya mwisho kufungwa ni jana tarehe 18/03/2021. Walifungwa na Bayer Leverkusen Europa, wiki nyuma Slavia alikua amempiga Leverkusen moja kwa bila.

Slavia amemtoa Leicester kwenye mashindano, Slavia pia ndiye kakomesha hii run ya Rangers kutofungwa kwa mechi zote tangu msimu uanze. Hatuna historia nao ndefu, mwaka 2007 tukiwa Europa hatua ya makundi tulimfunga Slavia 7 kwa bila kisha second leg tukatoka naye suluhu ya bila bila.

Slavia ya 2007 ungemwambia shabiki wake kwamba kuna msimu utafika hawatofungwa na wataitoa Europa timu iliyo ndani ya top four Epl asingekuelewa but here we are. So ingawa inatakiwa ionekane game nyepesi ila hii siyo Arsenal ile hii ni Arsenal ambayo ina presha, haina wapeleka mipira mbele na watengeneza chansi wa kutosha.

So tuna kazi ndefu kiasi chake, gemu zetu mbili za Europa zilizopita zimeonyesha jinsi gani bado Arsenal ina shida kucheza kama kikosi, swala ambalo Slavia hawana tatizo nalo. Tutakutana nao 08/04/2021 hapa kati kati tuna kesi za EPL tunahitaji kubadilika haraka kama tunataka tuongeze chansi yetu ya kuongeza step towards glory.
 
BILD - Hertha Berlin hawana tena mpango na Matteo Guendouzi, hawatamtumia tena kwa msimu huu na mazungumzo ya kumuongeza mkataba mpya wa mkopo yamevunjika hii ni kutokana na utovu wa nidhamu aliokua nao Matteo hasa tabia ya kujionyesha na ujuaji. Ataondoka Hertha mwisho wa msimu huu huku akiangalia uwezekano wa kujiunga na timu za EPL.

 

Huyu dogo maisha ya soka yatamshinda akiendelea hivi.
 
Nadhani hata kocha ameshaliona hilo na atalifanyia kazi.
 

We subiri kunyolewa hacha blablaaaa .
 
Hivi huko praise team we ni sauti ya ngapi? Mara ya mwisho kukutana umekufa tatu ila hapa unauliza kama unaogopwa.
Ngoja tukutane tena ndio utajua praise team niko sauti ya ngapi.. Kile kipindi cha Lampard kila mtu anajipigia utafananisha na huyu mtu anayejielewa anafanya nini?

Hivi unaamini kabisa hata tukikutana kesho una hata ubavu wa kupata on target hata moja? Nakupa challenge hebu jitahidi utoke mid table hapo ndio tuanze kuongea haya vizuri.
 
Sasa kama unajua ulipigwa tatu hili swali si la kipraise team hili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…