Sasa hivi tumebakiwa na Europa tu. Siku tunatolewa Carabao nikaona kwahiyo timu inabakiwa na priorities mbili Fa na Europa. Ila ilitakiwa iwe funzo, juzi hivi nilisema tumeshinda kwa newcastle ila siyo timu ngumu kwa sasa kisha nikasema Sotonaliikamia gemu na timu ambayo haijatrain kwa wiki 3.
Tulitarajia game na timu inayotrain kila siku apange watu gani?
Jana shots nyingi zilikua blocked, forward iikua haioni hata inapiga wapi ilikua ni kushuti kisha mtu wa Soton anajitupa mbele ya mpira, ni kama kucheza Ultimate team kwenye FIFA 21 inawezekana unapiga zako shuti unajiona uko 1 v 1 ila beki uliyemuacha hatua nne nyuma unashtuka yuko mbele anablock hilo shuti it's weird.
Kipindi cha kwanza tumepoteza nafasi mbili au tatu za kuscore, kipindi cha pili tumepoteza nafasi mbili. Hii inatuambia nini? Hii inatuambia Balogun ni bora kuliko Nketiah, Nketiah anahitaji akakomazwe. Edu na wenzake ni miyeyusho wangeweza kuwachukua kwa mikopo ST wengi waliokua wanatolewa kwa mikopo, inatuambia kwamba Pepe anahitaji game time kwenye ligi.
Pia Willian anatakiwa aende sasa.
Kila timu hua na talisman wake, siyo lazima ila hua inatokea. Unakuta huyo mchezaji akiwepo timu ni ama ishinde au isuluhu hakuna option ya kufungwa. Kwa united ni Bruno, Liva alikua Henderson, chelsea wanafikiri talisman wao ni Ziyech, kwa Arsenal talisman ni Tierney.
Yaani huyu inabidi iwe iwavyo apangwe. A kind of player anasababisha wapinzani wasijisahau na Mungu anakuumbua kila ukimuweka nje. Ni komedi watu wa jf tunakubaliana timu inahitaji LB na AM ila wenye timu wameleta kipa, ama kweli cha mtu gogo.
Mwanampotevu alivyorudi wote tukashangilia kisha akatuchoma kwa bao pekee. Anyway hii haimaanishi kwamba kiwango chake nina mashaka nacho mipira get deflected kwa yeyote so he is still good. Jumanne tunaruka nao tena Soton kwenye epl, itakua ni komedi nyingine amabyo itabidi twende na uso serious.
Mimi naamini timu inayomiliki mpira inahitaji watu watatu au wanne wenye akili za runs na kutoa pasi kutafuta nafasi mbele regardless kama kuna AM au hakuna. Ndiyo maana Emile, Saka, Tierney na Partey wakiwepo unaweza ona game inakua ya kushambulia zaidi.
Anyway, kama itakupunguzia machungu ni kwamba Arsenal kaifunga Soton mara 24, kasuluhu naye mara 13. Soton kaifunga Arsenal mara 9 na jana ameifunga Arsenal kwa mara ya kwanza kwenye FA.