EMILE SMITH ROWE, CROYDON'S KELVIN DE BRUYNE
Mitaa ya Magomeni ilituletea Mohamed Hussein Zimbwe Jr asante Magomeni, mitaa ya Kirumba huko Mwanza ilituletea Kelvin Patrick Yondani, thank you Mwanza Mwanza! Mitaa ya Ifakara Morogoro ikatuletea Farhan Jr, Asanteni pia Ifakara
Kuna Mtaalamu na Afisa wa zamani Kabisa wa soka pale FIFA anaitwa Jerome Valcke aliwahi kusema "The street is the best way of becoming a good Footballer" akiamini vumbi la mtaani, kuta za nyumba ndio zinazalisha wanasoka bora sana
Mie nani nibishe? Kama utahitaji kubishana basi dunia hujaijua wewe, nikusafirishe mpaka London Uingereza kwenye nchi ya Malkia Elizabeth anaepumzika kwenye kasri lake la Buckingham akiendelea kutazama nani atachukua kiti chake siku akiondoka
Ila mimi nakushusha mpaka Kusini mwa Jiji la London, ni mitaa hii ilituletea Callum Hodson Odoi, haikutosha ikatupa Jadon Sancho, haikutosha ilitupa David Beckham 'The English Prince' kisha Wilfreid Zaha na sasa imetupatia EMILE SMITH ROWE
Kwenye eneo hilo la Kusini mwa London kuna mtaa unaitwa CROYDON, ndipo hapo panaitwa Magomeni Usalama kama kwa Herry Mzozo, ndipo hapo nyumbani kwa fundi Emile Smith Rowe, wenyewe wanamwita CROYDON KELVIN DE BRUYNE
Ilikuwa jioni moja ya 2015 kama sikosei, Skauti mmoja wa Arsenal katika pitapita zake kichwani akiwa na stress nyingi sana, akiwaza Arsenal ya Mafundi kama Robert Pires, Arsenal ya Vava Voom Thierry Henry El Mimo au The Non flying Dutchman Dennis Bergamp
Katikati ya mawazo yake aliwaona watoto wakipiga mpira mtaani, alimshuhudia mtoto mmoja mwenye nywele nyeupe, hajavaa guards mguuni na amekunja socks zake, anapangua ukuta atakavyoz anafunga, anasharehesha na anaburudisha, hakuhitaji kumtazama mara mbili zaidi ya kuonana ma wazazi wake
Miaka mingi imepita sasa, De Bruyne kutoka South London anayasherehesha majukwaa ya Emirates, mchezaji mkubwa aliepatikana kwa pesa ndogo tu, amekuwa utambi kwenye mafuta ya taa, amekuwa reflector kwenye gari iliyoharibika
The Magician ESR, the very own English KDB