Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Castr, ushindi wa Arsenal ni wa bahati...kinyume cha bahati ni mipango

Unless uniambie plan yenu ilikuwa ni kupata bahati
 
Lbd km tunatofautiana kutafsili neno bahati kwenye soka. Neno bahati kwenye soka huja tu pale timu moja inapokuwa inafanya makosa mengi lkn timu pinzani inashindwa kutumia nafasi za hayo makosa kuscore.

Mfano kwa mechi ya jana kama arsenal wangefanya makosa mengi na city wakakosa nafasi za wazi hapo tungesema arsenal walikuwa na bahati lkn badala yake city hawakupata clear chance to score. Kwa maana hiyo hatuwezi sema arsenal alikuwa na bahati kwa kutofutwa na city. Nadhani unaweza kuwa umenielewa kiongozi
 
Arsenal tunanufaika sana na kasi ya Pepe na Auba kwnye kupress, na mara nyingi makosa yanafanywa na Opponent kama CF atakuwa dogo Nketiah anaspeed pia
 
Castr, komenti yako kuhusu plan ya Arsenal, hapa umelalamika kukosa plan
Boss tena hili nitalisimamia ni kweli game na Liva hakukua na plan ya ushindi. Tofauti na jana.

Magoli tuliyoscore jana tungescore same goals kwa Liva ningekukubalia kua tumepaki basi ila techs zimetupa points.

Ila jana magoli yetu yalikua planned. Cross na through pass zimetupa magoli ukiachia hivyo kuna through pass Auba alihisi ni off side akashut as a last resort, Pepe alipigiwa through pass ukamgonga kisiginoni akijiandaa kusprint, whereby angefanikiwa angebaki yeye na kipa, pia Auba alimpa Pepe pasi nje ya 6 ila Pepe akachelewa kuufuata.

So jana tulikua na vision kuliko game ya Liva. Kwa Liva magoli yote yalikua mtu katoa pasi hovyo na Laca akapokea. Ndiyo nikauliza bila vile kulikua na plan nyingine iliyoonekana? Na hakuna aliyejibu.
 
Yeah... Always you must force your luck,

Mfano huwezi shinda milioni 200 za sport pesa BILA KUCHEZA, though ukishinda bado ni bahati

Nilichokuwa nafanya hapa ni kumkumbusha Castr kile alichosema (Server za Melo hazidanganyi)
Kuna msemo wa "Fortune favors the brave".

Bahati haiji tu bila mipango.
 
Nimekuelewa baba. Siku njema
 
Kwa ule mpira na makosa mliofanya jana.basi ombeni sana fainal mkutane na chelsea na sio united
 
Arteta anaijenga timu na naamini endapo atapewa wachezaji wenye quality anayoitaka tutakuwa vema, kila jambo kwa hatua
 
Mkuu mimi nimekupata, na pia nakubaliana na wewe kuwa jana mlitengeneza nafasi zaidi na magoli mliyopata yalitokana na ubora wenu kuliko uzembe wa mpinzani

Lakini haimaanishi timu ambazo huwa zinapaki basi huwa hazitengenezi nafasi, timu zinazopaki basi huwa zinatengeneza nafasi japo chache (hasa za kushtukiza/counter attack) na kwenye kumalizia wanakuwa clinical zaidi

Kiukweli kwa kikosi chenu dhidi ya City jana ile ndio ilikuwa best option, kucheza na City kama wanavyocheza wao ni kujitafutia mauaji ya bure, next season mkiimarisha kikosi mnaweza kujaribu kucheza nao hivyo japo bado quality ya City ni kubwa sana


 

''OLIVER HOLT AT WEMBLEY STADIUM: Manchester City earned a momentous reprieve in one competition last week but in the FA Cup semi-final at Wembley with only 90,000 empty seats as judge and jury, they could not escape their sentence. The Court of Arbitration for Sport might have allowed them back into the Champions League for the next two seasons but Arsenal showed them no mercy here. Their shock 2-0 victory was a triumph of uncharacteristic resilience in defence, led by a brilliant display from David Luiz, and of clinical finishing from Pierre-Emerick Aubameyang, who scored goals in each half to dump City out of the competition they won last year by trouncing Watford in the final.
 
Tuwe serious. Hivi wewe haushiki nafasi yoyote ya kisiasa hapa nchini?
😂😂😂😂Kwanini mkuu? dah umenifanya nicheke Sana, Sina Hata interest na siasa ndugu yangu,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…