Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Haya mkuu tunayaongea kila siku, we usijipe presha wewe just relax tu, huyu jamaa hata wamvumilie vipi itafika muda atafukuzwa tu, uwezo wake ni mdogo hautomfikisha popote.
 
Goli la Ayew vs palace ,goli la Origi la tano vs liverpool, na goli la Raul vs Wolves leo ni magoli ya aina ileile yanafanana,
Magoli Yote yanatokana na mipira ya kross, watu katikati hawaruki kucheza mipira ya vichwa utadhani wapo peke yao pale, yeye kama kocha anadeal vipi na matatizo km hayo??

Sababu si hiyo tu, ila kwa Unai nimeona vitu vingi kila siku ni the same old story, vinajirudia utadhani hatuna kocha, unakuwa ni utoto, vitu vilevile kujirudia kila siku...Na ndio maana Evra anatuita "my babies" ...yupo sahihi kabisa na aliongea kwa uchungu sio kwamba kejeli.
 
Kama atakuwa benchi katika hii mechi tusitegemee chochote kipya
Mkuu ndio maana nasema atafukuzwa tu, hiyo mechi sioni tukishinda labda by chance.Leicester wenyewe wanajua wakitupiga wanajitengenezea mazingira mazuri ya kukaa top 4, Na huo uwezo wanao mkuu, tena na hivi wapo Home.
 
Unai hawezi kukaa Arsenal miaka mitatu kwa matokeo haya mkuu, Na ikitokea hivyo naamia Charlton Athletic ya kina Darren Bent na mdogo wake yule sijui nani Bent...
Huyu kocha anambinu mbovu sana
 
Nilikuwa tu naangalia statistics hapa kwa hisani ya #Mbweha#

Dakika 90 mmepiga mipira mitatu tu golini...
 
Unai hawezi kukaa Arsenal miaka mitatu kwa matokeo haya mkuu, Na ikitokea hivyo naamia Charlton Athletic ya kina Darren Bent na mdogo wake yule sijui nani Bent...
Wenger kakaa miaka 23 na makombe matatu na mlishindwa kumtoa, hamna uwezo wa kumtoa huyu. Kumtoa kocha inahitaji hela ndefu mazee..mtapata tabu sanaaaaaa.
 
aise uchezaji wa arsenal ni ovyo kabisa hadi selection alizofanya ni ovyo kabisaa torreira na ozil hawakucheza their natural position. kwenye subs ndio kabisaa.shukuru granit xhaka hajacheza...
 
Wenger kakaa miaka 23 na makombe matatu na mlishindwa kumtoa, hamna uwezo wa kumtoa huyu. Kumtoa kocha inahitaji hela ndefu mazee..mtapata tabu sanaaaaaa.
Hujui mpira mzee ni bora ukae kimya, we ulitaka awe na mangapi? nenda na wewe tuone utatoka na mangapi.
 
Duuh! Mkuu punguza hasira
Inaboa sana viongozi hawajui kama Mashabiki hawamtaki kocha au wanapuuzia ?nafikiri Mashabiki wa London ni wapumbavu sana ingekuwa TZ next match hakuna shabiki ambaye angeenda uwanjani uwanja ungekuwa mtupu kabisa hatutakagi ujinga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…