Nimependa bei tuliyopata kutoka kwa Iwobi. Actually nilifikiri hana thamani ile, ingawa naamini tulitakiwa kubaki naye. Liva wamebaki na Origi kwa ajili ya kiwango alichoonyesha mechi 2 tu.
Mustafi siyo mbaya. Takwimu zake zipo vizuri kuliko Virgil, isipokua midfielder yetu haikua nzuri hivyo mpira ulikua unashinda mno kwa Mustafi.
Nina imani na Bellerin na Holding. Too bad Niles simuoni katika potential first XI yetu, ni mchezaji poa aliimprove kila mechi.
Guendouz simkubali kwakua hana stamina at the same time hana spidi. Surprisingly na control hana. Kwa m
ninavyomuona nahisi bado yupo na hizo shortages.
Kama PES player wa PS2 Lacazette inapendeza akitokea wing ya kulia Pepe ya kushoto na Aubameyang akae katikati. Pepe na Laca ni fighters, wanakaa na mpira vizuri kumzidi Auba. Auba ni scorer mzuri kuliko kua mleta mipira kwenye dimba.
Kumuweka pembeni means kupoteza mipira eneo hilo.
Msimu uliopita Laca alikua na assisst nyingi kuliko Ozil. Ni ajabu kidogo ukizingatia nafasi zao uwanjani. Ozil akiwa on fire hua inakua mara mbili ya kawaida akiwa nyoro hua inakua mara 7 ya kawaida, pia hana consistency. Ingawa siyo swala kwa kipindi hichi tulichompata Cebalos.
Xhaka na Toreira walikua poa, hope moto ni ule ule. Pia formataion ya 3 4 1 2 naona ni nzuri ila isichezwe kwa kila mechi.
Ni formation ya kukaba mno wakati mechi zingine tunataka kushinda, pia ni formation ngumu ikiwa mid yako ni Guendouz na Ozil.
Naipa striking yetu 79%
Midfield 77%
Beki 78%
Hiyo ni kwa sasa.