Nipo hapa nasikia tu Makelele kipindi cha mwanzo. Nimeamua kuitafuta mechi kwenye TV kumbe iko tv ya TVN Warszawa (TVN Warsaw). Mwanzo nilifikiri itakuwa kwenye Station yao ya HD ya N ambayo inabidi uwe na Decoder yao.
Sasa kaingia kijana kutoka Zimbabwe ambaye mwaka jana na juzi alitesa sana kwenye ligi za Poland, anaitwa Chinyama.
Huu ni uwanja ambao umejengwa na kupanuliwa. Miaka ya karibuni, kampuni ya ITI ambayo ni moja ya kampuni kubwa sana hapa Poland, walinunua hii timu. Kwa sasa wanaleta mabadiliko makubwa sana huku tukiona wachezaji walionunuliwa kwa Euro karibu milioni 1.
Ningelitamani sana kijana wetu Ngasa walau acheze kwenye timu kama hizi. Siku zinavyokwenda, itakuwa ngumu sana maana nina imani watakuwa wanazidi kupanda BEI na kudata.