Arsenal (The Gunners) | Special Thread

I suggest he should have ended his Gemany citizenship too..!

Every Geramany has a negative eye on ozil now..
 
Wamuache Ozili kwani alikuwa anacheza peke yake uwanjani?, mbona walipochukua kombe 2014 hawakumsifia??
 
Kwa Taarifa zisizo rasmi Sana Ila nimezipata kweny source makini ninazoziamin Sana zinasema kuwa.

Mkurugenzi WA ufundi WA arsenal Raul Sanhieli yupo Spain Sasa hivi kushughulikia dili YA dembele. Miaka miwili mkopo Na option YA kumnunua km akionesha kiwango kikubwa. Kwahiyo iyo dili ipo njian kukamilika siku za USONI. Kwahiyo arsenal itakuwa ikimlipa nusu mshahara kwa wiki 75k.

Baba WA nzonzi amesema wanaijadili ofa YA nzonzi kwenda arsenal. Mazungumzo yamefikia pazuri muafKa utapatikn soon.

Ospina kwenda Napoli kuziba nafas YA Pepe Reina. Mazungumzo yamefikia pazuri.

Bakayoko kwenda mkopo sevilla kuziba nafas YA nzonzi anayetimkia arsenal. Makubaliano tayar nzonzi tu NDIO wanamsikilizia.

KWAHIYO MJIANDAE WAKALI WOTE WA DORTMUND WANAHAMIA ARSENAL MSIMU UJAO MTAIELEWA TU ARSENAL
 
Ulikuwa ni uchaguzi wa ujerumani?
 
Arsenal Tour in Singapore


Kikosi cha Arsenal kabla hakijaanza kucheza mechi ya kirafiki na Athletico Madrid.

Nyuma kutoka kushoto: Hector Bellerin, Bernd Leno, Rob Holding, Shrokran Mustafi, Matteo Guendouzi, Emile Smith Rowe, na PierreEmerick Aubameyang.

Mbele kutoka kushoto: Reiss Nelson, Alexandra Lacazette, Sead, Kolasinac na Aaron Ramsey.





Arsenal wanacheza na Athletico Madrid na mpaka sasa kipindi cha pili goli ni 1-1

Mechi inachezwa uwanja wa taifa wa Singapore.

Athletico walianza kufunga dakika ya 36 kipindi cha kwanza goli lililofungwa na Correa baada ya kupokea mpira wa juu kutoka kwa Vietto.


Kipa wa Arsenal Leno akiwa hoi baada ya kufungwa goli la kwanza.


Mfungaji wa Athletico Madrid Correa akipongezwa na Vietto baada ya kufunga goli la kwanza.

Dakika ya 46 mchezaji mdogo wa Arsenal Smith Rowe nae akasawazisha goli hilo kwa goli safi ambalo amefunga akiwa nje ya boksi la hatari.


Mchezaji Aubameyang akijaribu mpira wa adhabu.

Picha zingine za Arsenal wakiwa ndani ya uwanja wa taifa wa Sngapore.




Vyumba vya Arsenal.



Vyumba vya Athletico Madrid.

Hali ya Wachezaji:

Wachezaji wa Arsenal wanaonekana wana furaha ya kusafiri kuwepo nchini Singapore.

Mesut Ozil na Mohamed Elneny wakiteta jambo.


Pierre-Emerick Aubameyang na Hector Bellerin wakiteta jambo.


Pierre-Emerick Aubameyang na Eddie Nketiah wakiingia uwanjani.


Mesut Ozil akiwa ametulia baada ya kusakamwa na chama cha soka cha Ujerumani.


Hali ni furaha tu ya kusafiri.
 
Last edited:
Maitland-Niles Ainsley huyu dogo yupo vizur kama ataendelea kupewa muda zaidi yeye na kipa wa atletico wamepiga penat nzur sana .
 
Mechi meisha goli 1-1

Zinapigwa penalties.

Athletico Madrid wanashida penalty 2 na Arsenal wanakosa zote.

AM wanashinda kwa goli 3-1

Jumamosi Arsenal itacheza na PSG kwenye uwanja huuhuu wa taifa wa Singapore.
 
Mechi meisha goli 1-1

Zinapigwa penalties.

Athletico Madrid wanashida penalty 2 na Arsenal wanakosa zote.

AM wanashinda kwa goli 3-1

Jumamosi Arsenal itacheza na PSG kwenye uwanja huuhuu wa taifa wa Singapore.
perfomance ya arsenal ilikuaje!?..wanakaba/press au bdo wanakaba kwa macho,wana kasi au bdo slow?
 
perfomance ya arsenal ilikuaje!?..wanakaba/press au bdo wanakaba kwa macho,wana kasi au bdo slow?

Mambo makuu matatu lakini kabla ya kuyasema hayo nisisitize kwamba Pre-season kwa Arsenal inamaanisha Practice yaani kujifunza mbinu mpya.

Jambo la kwanza ni kwamba bado Arsenal wakikutana na timu inayocheza mtindo wa kujihami kama Athletico, basi wanakosa mbinu za kufatuta kupata nafasi za kufunga.

Mateo Guandouzi leo alikuwa kila mara akipoteza mipira kwa wachezaji wa kiungo wa AM.

Hili ni eneo ambalo kochaEmery ataliangalia khasa kwa kuzingatia bado Mesut Ozil na Lucas Torreira bado hawajaanza kucheza rasmi. Torreira ana uwezo wa kuuchukua tena mpira unapopotezwa na Ozil atasaidia kutafuta vyumba zaidi huku akisaidwa na Torreira endapo atapoteza mipira.

Jambo la pili ni kwamba kipa wa Arsenal atakuwa ni Leno na Cech atakuwa namba 2 huku Aubameyang akiwa mshambuliaji wa pembeni na Lacazette akiwa ni namba 9 wa Arsenal.

Pia Arsenal wamecheza mtindo wa 3-4-3 badala ya ule wa 4-3-3 huku Emery akiwa anatoa maekelezo kwa sauti kila mara jambo litalosaidia timu kucheza na kufuta maelekezo, huku wachezaji wakionekana wapo fit na wenye nguvu.

Jamb la tatu na mwisho ni kwamba Arsenal bado safu yake ya ulinzi inatia shaka khasa pale Rob Holding alipojikuta akipitwa na mchezaji wa AM Angel Correra kufunga goli lao la kwanza.

Matteo Guendouzi na Aaron Ramsey nao wakiwa wanachanganywa katikati hivyo kusababisha timu kushambuliwa kila mara.

Lakini kama nilivyosema hapo juu Lucas Torreira na Mesut Ozli watakaporudi wataziba nafasi za hawa wawili na sehemu ya katikati itakuwa sawa.
Sead Kilasinac nae alikuwa kilaa mara akipitisha watu upande wake wa kulia.
 
Last edited:
mkuu jana jamaa wamecheza 4-2-3-1 ambapo safu ya walinzi wanne ilichezwa na hector,kolasenac,mustaphi na holding wakati ramsey na matteo walipiga hapo chini juu akacheza smith rowe mfungaji wa goli la jana wings zilishikwa na auba upande wa kusoto na dogo nelson upande wa kulia huku mbele kabisa akasimama lacca .....huyu dogo manywele yeye alikuwa akipoteza sana mipira na shida kubwa ni kuwa hana nguvu za kutosha ingawa anaonekana kujiamini sana na anaweza kumiliki mpira vizuri na kutoa pasi zinazofika alikuwa anadondokadondoka mno kila akiguswa kidogo........mustaphi nae bado anaonekana hajawa vizuri,holding huyu ndiye aliyetoa boko la jana.....naamini zile pacha mbili za ugiriki zikianza itapendeza zaidi pale kati
 
Emile Rowe Smith baada ya kuonyesha kiwango kizuri Pre-season tayar arsenal wamekaa naye chini na tayar amekubaliana na Arsenal baadhi ya vitu vingi vya mkataba mpya..inaweza kuwa very close next week.
 
Habari nilizozipata kwa sasa ni kwamba

Nzonzi hatumuhitaji tena na ni kwasababu kumbe Nzonzi alikuwa kaandaliwa coz kuna muda dili la ramsey lilikuwa halieleweki lakn kwa sasa Ramsey karibia kila kitu kipo sawa atasaini muda si mrefu kwahyo Nzonzi hatumwitaji labda itokee pancha mbaya kabla ya msimu kuanza ya midfielder then ndo Nzonzi kama option.

Ospina anaondoka besktas wanamaliziana na arsenal na ataondoka ospina anataka kuwa namba 1 kwahyo klabu iko tayar kumwachia

Osman Dembele kuna mtu aliuliza huyu ndo mchezaji ambaye timu inapambana kufa kupona aje arsenal kabla ya tar.9/8 Sven ndo anayeliendesha hili na Raul mazungumzo yanaendelea kati ya Barcelona Na Arsenal so until next week tutajua tumefikia wapi ila tupo very very serious...
 

Honestly namkubali sana Ospina jamaa ni royal sana kwetu ila sio mbaya namtakia kila la heri aendako.
Kama hawa wazee wa ku-negotiate kweli wanaongea na Barca basi hili dirisha litaenda safi kwangu wakimleta uyu dogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…