Tetesi
Mchezaji anayelengwa na Arsenal na Everton Steven N'Zonzi amedaiwa kuonekana katika uwanja wa ndege wa Gatwick.
Mchezaji huyo wa zamani wa Stoke na Blackburn 29, ameambia Sevilla kwamba anataka kuondoka.. (Sun)
Tetesi
Arsenal na Manchester City zinamkagua beki wa Burnley James Tarkowski, 25, kwa lengo la kumvutia katika dirisha la uhamisho la mwezi ujao.(Times - subscription required)
Tetesi
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger anasema kuwa kuna uwezekano mkubwa wa asilimia 90 kwamba hataongeza mchezaji mpya katika kikosi chake mnamo mwezi Januari. (BeInSports - via London Evening Standard)
Tetesi
Sanchez atasalia Arsenal mwisho wa msimu na baadaye ajiunge na Manchester City katika uhamisho wa bure , mpango ambao utampatia kipato cha £400,000 kwa wiki. (Daily Mirror)
Tetesi
Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 29, anakaribia kuhamia Paris St-Germain baada ya ajenti wake kuelekea katika mji mkuu wa Ufaransa kwa mazungumzo(Canal Plus - via Metro)