Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Msimu wa maandalizi kwa timu yetu ya Arsenal unaanza rasi leo ambapo timu yetu inatarajiwa kucheza na timu ya Lens ya Ufaransa.

Uwanja ni wa Lens uitwao Stade Bollaert-Delelis.

Utaratibu mzima wa mechi za kujipima nguvu za Arsenal.

vs MLS All-Stars, Thursday 28 April, 01:00 BST, mjini Dallas katika jimbo la Texas nchini Marekani.

vs Chivas, Sunday 31 July, 17:00 BST, San Jose huko Santa Clara jimboni California, Marekani.

vs Viking VK, Friday 5 August, 19:30 BST, Stavanger [Norway]

vs Manchester City, Sunday 7 August, 18:00 BST [Stockholm]
 

Ndio maana nimesema, kama Wenger akiamua kuvunja benki, lakini hiyo sera yao ya usajili haijasimamia hapo.
 
Na washua wameshaona Hawana mpango wakumwaga mapesa mengi kusajili so kwa super quality player in the market lazima umwage mzigo kwa mpango huu kina holding wanahusika Sana Wacha niwe mpole tu kwa kweli nisubir ligi haya mengine yanauzi
 
Game ya leo saa ngapi kwa masaa ya Tanzania
 
Man wameshakufa Mkono kasoro
 
Hii ndiyo timu iliyoanza mechi na Lens.

Martinez, Debuchy, Mertesacker, Chambers, Monreal, Elneny, Coquelin, Walcott, Iwobi, Reine-Adelaide na mbele Chuba Akpom
 
Uwanja wa Lens kabla mechi haijaanza.


Lens


Mtunza vifaa vya wachezaji au kitman bwana VIc Akers alipokuwa akiandaa vifaa vya wachezaji kwenye chumba cha wachezaji wa Arsenal.


Meneja Arsene Wenger akisalimiana na wapenzi wa Gunners ambao wamesafiri hadi Lens mji uliopo kaskzini mwa Urafansa, kushuhudia mtanange huo.


Kikosi cha vijana kabla ya mechi ya kirafiki na Lens.
 
Dakika imekwenda ya 76 Arsenal wanaonekana wamechoka na au bado wanawaza likizo.

Lens 1 Arsenal 0
 
Lens 1 Arsenal 1

Alex Oxlade Chamberlain anafunga goli la kusawazisha dakika ya 81


Mpira umeanzia kwa Joel Campbell na akampa pasi Serge Gnabry ambae nae akamtengenezea chumba OX nae kwa utulivu kabisa akiwa umbali wa yadi 15 akauchota mpira huo na akaukwamisha kimiani kwenye kona juu ya kipa wa Lens Douchez.
 
Mpira umeisha na timu zote zimetoa sare ya 1-1

Arsenal walionekana kutaka kuongeza magoli baada ya kusawazisha lakini meneja Arsene Wenger atakuwa ameridhika na matokeo haya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…