Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Jamani eeh tusianze kumsifia huyu dogo kabla hatujaona anachezaje. Wengi wetu tumemsikia juzi juzi na clips za youtube haziwezi kuwa proof ya kuwa jamaa ni mzuri kama Patrick Vieira au sijui nani. Wapenzi wengi wa Arsenal navyowajua hamkawii kulalamika kuwa Wenger kaingia mkenge kwa kununua mchezaji huyu au yule. Miaka yote tunasikia jinsi watu wanavyowatukana kina Flamini, Arteta, Giroud etc, muda Fulani ilikuwa kina Ramsey, Wilshere. Msimu huu sijasikia mkimtukana Giroud sababu anafunga magoli karibia kila mechi. Tusubiri tuone itakavyokuwa baada ya mechi kama 6 au 10 atakazocheza ndio tutoe verdict.
 
Jamani eeh tusianze kumsifia huyu dogo kabla hatujaona anachezaje. Wengi wetu tumemsikia juzi juzi na clips za youtube haziwezi kuwa proof ya kuwa jamaa ni mzuri kama Patrick Vieira au sijui nani. Wapenzi wengi wa Arsenal navyowajua hamkawii kulalamika kuwa Wenger kaingia mkenge kwa kununua mchezaji huyu au yule. Miaka yote tunasikia jinsi watu wanavyowatukana kina Flamini, Arteta, Giroud etc, muda Fulani ilikuwa kina Ramsey, Wilshere. Msimu huu sijasikia mkimtukana Giroud sababu anafunga magoli karibia kila mechi. Tusubiri tuone itakavyokuwa baada ya mechi kama 6 au 10 atakazocheza ndio tutoe verdict.
Mchezaji hanunuliwi kama huyu bila kuwa wamemfuatilia muda mrefu....ulaya scouts wanawajua talents zote na details zao zinawafikia makocha kila kukicha

Sio bure kuna kitu wamekiona pale, la msingi hasizingua na apewe time ya adaptation maana EPL sio ligi ya Uswizi

Mashabiki kutoa verdict kwa players ina base na Emotions ambayo ni aidha furaha au stress dhidi ya perfomance ya mchezaji husika....

ila naamini Dogo kipaji anacho na kwa maelezo ya Kocha ni BOX TO BOX

kitu kingine naombea hasiwe Injury prone
 
Mchezaji hanunuliwi kama huyu bila kuwa wamemfuatilia muda mrefu....ulaya scouts wanawajua talents zote na details zao zinawafikia makocha kila kukicha

Sio bure kuna kitu wamekiona pale, la msingi hasizingua na apewe time ya adaptation maana EPL sio ligi ya Uswizi

Mashabiki kutoa verdict kwa players ina base na Emotions ambayo ni aidha furaha au stress dhidi ya perfomance ya mchezaji husika....

ila naamini Dogo kipaji anacho na kwa maelezo ya Kocha ni BOX TO BOX

kitu kingine naombea hasiwe Injury prone


Wachezaji wengi wa ulaya wanakuwa scouted kwa muda mrefu kabla ya kununuliwa na bado tunaona wachezaji wasio na viwango vya kuridhisha. Nachosema tusubiri muda tuone atakachofanya.
 
Wakuu mambos!

Haya basi, Arsenal wametangaza rasmi kumsajili Mohamed Elneny kutoka Basel ya Uswiss. Kama mtankumbuka habari hii ilikuwa ni ya kitambo tu maana dogo alikuwa akifuatiliwa kwa zaidi ya mwaka.

Elneny amefanya mazoezi jana na huenda akajumuishwa kwenye kikosi cha kucheza jumapili na Stoke City pale uwanja wa Brittania.

Meneja Arsene Wenger leo amesema huenda akampa dakika kadhaa kipindi cha pili.

Kama mtakumbuka ni katika uwanja huuhuu yule beki wa Stoke Ryan Showcross alimfunja mguu Aaron Ramsey na kusababisha Ramsey akae nje zaidi ya mwaka mmoja.
ramsey_2677742a.jpg

Ramsey akilia kwa uchungu kufuatia kukanyagwa mguu wake ulopinda na Ryan Showcross (hayupo pichani) huku wachezajiu wenzie wakiwa hawaamini wanachokiona. Kutoka kushoto ni Gael Clichy, Thomas Vermaelen, Nicklas Bendtner na Ces Fabregas.

Pia Danny Welbeck anarudi ndani ya wiki mbili hadi tatu.

Alexis Sanchez huenda akacheza jumapili kizingatia yupo fit asilimia 100.

COYGs!!
 
Last edited:
Hapo ndo tushafunga usajiri...tuombee wale majeruh sugu wapone na viwango vyao virudi katika ubora
 
503183116.jpg


Mesut Ozil
German national team player of the year

Arsenal’s Mesut Ozil has been voted as the German national team’s player of the year for 2015. The 27-year-old claimed 45.9% of the vote, with over 51,000 fans naming him as their top player over the 12 months. Bayern Munich’s Thomas Muller and Cologne’s Jonas Hector came second and third with 15.9% and 13.6% of the vote respectively. Ozil featured in eight of Die Mannschaft’s nine games during the year, managing eight assists. He has continued this form for his club, acquiring 16 assists for the Gunners in the Premier League this season. This is the fourth time that the former Real Madrid man has won the award, winning it three times in a row before Toni Kroos took it last year.
 
OG ananyatia top goal scorer, yupo magoli matatu nyuma .... na kwa speed anayoendelea nayo tunamtakia mafanikio. Kwa mtazamo wangu kijana Elneny atakuwa provider kama Ozil na kuweza kufunga vile vile. Ma-shoot yake ya mbali ni moto wa kuotea mbali. Atapewa ubatizo kule Brittania Stadium J2 nyumbani kwa The Potters chini ya Mark Hughes ambaye ameibadili ile timu icheze mpira wa kueleweka sio mieleka.
 
gun__1452954410_elneny_training.jpg


Elneny akiwa mazoezini leo ..... ....

zp_599311257SM002_Arsenal_Trai_8660.jpg


Alexis .... ... ..

zp_599311257SM008_Arsenal_Trai_8731.jpg


Ox alikuwepo ... ... ..

zp_599311257SM009_Arsenal_Trai_3003.jpg


Ramsey wa kwanza kushoto akiingia kwenye mazoezi na wenzake leo Colney.
Anarudi katika uwanja aliovunjika mguu akiwa kwenye mission ya kuonyesha kwamba
yupo anatandaza kabumbu ya uhakika na panapo majaliwa ataendelea na mission yake.

zp_599311257SM025_Arsenal_Trai_8540.jpg


zp_599311257SM040_Arsenal_Trai_9895.jpg


Cech mate anategemea kuwa makini kesho ... .

zp_599311257SM028_Arsenal_Trai_4745.jpg


zp_599311257SM031_Arsenal_Trai_5270.jpg


zp_599311257SM034_Arsenal_Trai_7188.jpg


zp_599311257SM048_Arsenal_Trai_9784.jpg


zp_599311257SM058_Arsenal_Trai_9112.jpg


zp_599311257SM060_Arsenal_Trai_9742.jpg


Le prof kama kawa akiandaa mikakati ya kesho
 
Mkuu Wacha 1, mimi nipo na kesho ntakuwepo hapa kuleta burudani kutokea uwanja wa Britannia maana Arsenal kesho tena wana nafasi ya kurudi kileleni na kuongoza ligi kwa 2 points kwa Leicester na 3 points kwa Man City.

Kesho mzee Wenger anaweza akaanza na Elneny na Alexis mwanzo maana Flamini na Ramsey uchezaji wao ni wa kuchanganyana sana na utoaji pasi baina yao unakuwa hafifu sana. Lakini ni rekodi yao ndio itakayowafanya waanze mchezo huo.

Stoke City wao wana wachezaji wawili muhimu ambao wana matatizo ya musuli na hawatacheza kabisa mechi hio nao ni Xherdan Shaqiri na Marco Anarutovic ambao waliwasumbua sana Chelsea na Man Utd.

Hivyo Arsenal wanaweza kabisa kuanza na wachezaji wafuatao:

Kipa Cech, beki kushoto Nacho Monreal ambae alimdhibiti vizuri Jordan Ibe kwa kipindi kirefu, kesho atakuwa na kazi ya kumchunga Ibrahim Afellay- beki wa kulia ni Hector Bellerin.

Mabeki wa kati ni Boss na Petr Mertesacker hawa jamaa uzoefu wa kucheza pamoja ndio ufunguo.

Sehemu ya kiungo:

DM - Mathieu Flamini ingawa mzee Wenger angependa kijana Elneny nae ashiriki mchezo huo. Mathieu Flamini ameanza karibu mechi zote tatu ambazo Arsenal imecheza hapo uwanja wa Britannia.

Kiungo wa kati CM ni Aaron Ramsey. Ramsey itabidi awe anarudi haraka kuzuia mashambulizi kwasababu Ozila hataweza kurudi nyuma hivyo Ramsey anapaswa kuwa makini sana anapofanya mashambulizi mbele.

AM ni Ozila ambae jumatano hakufaidi sana mchezo ingawa kesho anapewa nafasi hio kwa vile Arsenal inayarajiwa kuumiliki mchezo, hasa sehemu ya kati.

Washambuliaji:

Mshambuliaji pembeni namba 7 ni Joel Campbell ambae ameendelea kukuza uwezo wake wa kufanya mashambulizi anayoyatayarisha kutokea upande wake wa kulia kumtafutia vyumba Olivier Giroud na pia kurudi nyuma kulinda. Bado ataendelea kucheza nafasi hio hadi Alexis Sanchez atakapokuwa tayari na wakacheza pamoja.

Mshambuliaji wa pembeni namba 11 ni Theo Walcott. Kwenye mechi ya jumatano Walcott ndie aliesababisha goli la kwanza la Liverpool kwa kujaribu kutaka kupiga danadana na ndipo alipoupoteza mpira na Jordan Henderson akauchukua.

Tatizo la Walcott ni kufanya maamuzi decision making anapokuwa na mpira na hii huwa inatokea kwa baadhi ya mechi tu. Lakini Alexis Sanchez atakapopona vizuri atachukua nafasi hio na Sanchez atacheza upande wa kushoto na Campbell atakuwa upande wa kulia.

Pia Walcott atatumiwa kama back up ya Giroud.

Mshambuliaji wa kati namba 9 ni Olivier Giroud. Anayo magoli 12 katika mechi zote 15 alozianza na jumatano alicheza vizuri sana na hasa goli lake la pili ambalo kwanza alimzungusha beki wetu mshahara wa zamani Kolo Toure.

Giroud anatazamiwa kufanikisha ushindi wa kesho ambao ni muhimu sana kuliko ushindi wowote ule.

Mtindo wa Arsenal ni uleule wa 4-3-3 ambao hubadilika na kuwa 4-3-2-1 kulingana na mchezo.

Tukutane hapa kesho mchana.

COYGs!!!!
 
Mechi ya kesho ni muhimu katika kuthibitisha kua tunahitaji kunyanyua ndoo msimu huu itaonyesha kiasi gani tuko siriasi na jambo hili maana nafasi iko mikononi mwetu ni sisi tu kuitumia
Kila la heri Arsenal kama tusemavyo:-For the brave nothing is too difficult....COYG
 
Kama leo tutashinda mchezo huu, basi nitazidisha imani ya kushinda EPL hadi 65%. Stoke sio timu ya kuifunga hovyo hasa kwa arsenal, ila km Sanchez atarudi na kufanya vzr basi atakuwa na hali na hamasa ambayo itamfanya ozil awe na imani zaidi na pass zake, kwakuwa Walcott anapoteza nyingi sana...! COYG
 
Kama leo tutashinda mchezo huu, basi nitazidisha imani ya kushinda EPL hadi 65%. Stoke sio timu ya kuifunga hovyo hasa kwa arsenal, ila km Sanchez atarudi na kufanya vzr basi atakuwa na hali na hamasa ambayo itamfanya ozil awe na imani zaidi na pass zake, kwakuwa Walcott anapoteza nyingi sana...! COYG
Leo tunashinda.
Ila game hadi half time itakuwa ngumu sana na matokeo yatakuwa 1-1 au 0-0.
Ila second half watakuwa kama Watford magoli matatu ya haraka haraka yatatuhakikishia ushindi.

Game itaisha kwa 0-3 or 1-4.

Ushindi ni lazima and we cant afford to have a diffderent result out of 3 points.
 
Leo tunashinda.
Ila game hadi half time itakuwa ngumu sana na matokeo yatakuwa 1-1 au 0-0.
Ila second half watakuwa kama Watford magoli matatu ya haraka haraka yatatuhakikishia ushindi.

Game itaisha kwa 0-3 or 1-4.

Ushindi ni lazima and we cant afford to have a diffderent result out of 3 points.
Keep it up now you are becoming positive ....though a bit teh teh teh

game ngumu lakini sio masikhara
 
Wakuu wa Gunners mpo?

Leo ndio leo uwanja wa Britannia kayika mji wa Stoke.

Tunasubiria team news kwa sasa ntashusha hapa, inawezekana ikawa ni ile niliyoishusha jana usiku.
 
Arsenal ina 43 points baada ya mechi 21, ikiwa ni 7 points zaidi ya zile tulozipata msimu ulopita.

Lakini tumekosa 6 points kuliko msimu ambao tulinyakua ubingwa kwa mara ya mwisho mwaka 2004 ambapo hadi wakati huu tulikuwa na 49 points.
 
Back
Top Bottom