Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Wakuu habari za usiku maana saa za Croatia ni saa 1 na dakika 52 za jioni.

Nipo hapa tunasubiri orodha ya majina ya wachezaji ambao watawakilisha timu zao uwanjani, yaani yale majina 22 na wachezaji wa akiba wa timu zote.

Mechi hii itakuwa ikifanyika kwenye uwanja wa Maksimir ambao ndio uwanja wa taifa wa Coratia na Dinamo Zagreb huwa wanautumia.
 
Arsenal wanarajiwa kuchezesha kikosi kilicho na mabadiliko huku Aaron Ramsey, Hector Berellin na Francis Coquelin waloachwa ambako wamebaki London kwa kusubiri mtanange wa Stamford Bridge siku ya jumamosi saa 6.45 za mchana kwa saa za Ulaya.

Hivyo Mathieu Debichy, Mikael Arteta na Mathieu Flamini wanaweza kuanza game.
 
Team News:

Arsenal: Kipa David Ospina, Olivier Giroud, Gibbs, Arteta, Chamberlain, Debuchy na Gabriel Paulista wanaanza.
 
Team kwa ujumla

Arsenal:

David Ospina, kulia ni Mathieu Debuchy, mabeki wa kati ni Gabriel Paulista na mkoba Laurent Koscielny, beki wa kushoto Kieran Gibbs. Namba sita ni Arteta, namba nane Cazorla, namba 11 ni Mesut Ozil, namba saba ni Alex Oxlade-Chamberlain, namab 10 ni Alexis Sanchez, na namba 9 ni Olivier Giroud.

Dinamo Zagreb: Eduardo, Ivo Pinto, Sigali, Taravel, Pivaric, Soudani, Paulo Machado, Ademi, Antolic, Fernandes, Pjaca.
 
Arsenal wamevalia jezi zao nyekundu na kaputura nyeupe pamoja na soksi nyeupe huku Dinamo Zagreb wakiwa na jazi na kaputura za rangi ya bluu iloiva.

Dakika inakwenda ya 18

Mabao ni 0-0
 
Arsenal wamevalia jezi zao nyekundu na kaputura nyeupe pamoja na soksi nyeupe huku Dinamo Zagreb wakiwa na jazi na kaputura za rangi ya bluu iloiva.

Dakika inakwenda ya 18

Mabao ni 0-0
Habari Chifu...

Msaada wa Live streaming mkuu
 
So far so good Arsenal wanakuwa wanasubiri kushambulia kwa kunuia kupata goli lakini walitakiwa wamwe na goli 3 mpaka sasa.
 
Goooooooal kwa Dinamo Zagreb goli wanfunga dakika ya 24 na Josip Piravic

Zagreb 1 Arsenal 0
 
Dakika inakwenda ya 36 na Arsenal wanajaribu lakini hawaonyeshi kutafuta goli kwa nguvu. Giroud anapoteza mipira mingi.
 
Back
Top Bottom