Ar/rb/10850/2015: Matapeli wanatumia namba yangu ya Vodacom

Ar/rb/10850/2015: Matapeli wanatumia namba yangu ya Vodacom

JC Freak

Member
Joined
Dec 4, 2013
Posts
57
Reaction score
31
Nimefungua hii Report Book (RB) katika kituo cha Police Central – Arusha hii ni baada ya simu yangu kupoteza mawasiliano siku ya jumamosi 22/08/2015, nikadhani kuwa simu imeharibika kumbe kuna mjanja/ wajanja wame swap number yangu kwa matumizi yao.

Walimpigia mke wangu simu huku kukiwa na mikwaruzo na kutosikilizana hivyo jamaa wakatumtumia wife sms na kumuuliza kwenye simu yake anashilingi ngapi? Akawajibu kiasi cha fedha alichokuwanacho kwenye simu yake. Jamaa wakamrudia kwa sms wakamwambia atume shilingi milioni moja, baada ya majibiziano mda mrefu mke wangu akaawambia hebu nipigia kwenye landline ya ofisini kwangu, hapo jamaa ndipo walipokwama jaribio lao.

Nilipopata taarifa nilienda Vodacom (mkabala na Stanbic Arusha) na kutoa ripoti na niliomba waifunge number na walifanya hivyo.

Cha kushangaza muda si mrefu simu ilirudi hewani na wakaendelea kutapeli watu wanaonipigia, hawajamaa hakuwakuwa wakipoke simu ila wanajibu kwa sms kuwa spika mbovu tuma sms. Halafu wanatuma sms kuwa ninamatatizo na hivyo kuomba kutumiwa hela kwa mpesa.

Leo nimeenda TCRA walaniambia niende Vodacom kupeleka malalamiko yangu.

Nimeenda Vodacom lakini sikupata majibu ya kuridhisha.

Je anetumia hiyo number ana nguvu kiasi gani mpaka ku override Vodacom system ambayo wao Vodacom waliifunga siku ya jumamosi?
Au ni staff wa Vodacom?
Niliomba wajaribu ku trace simu iko wapi sikupata jibu lolote
Nimeomba email kuwa nitume malamiko yangu officially wakaniambia kuwa wao ndio watakaotuma report HQ
 
Kila mahali hakukosi watumishi wasio waaminifu.

Mwambie mkeo awaarifu watu wenu wa karibu ambao na yeye ana mawasiliano nao.

Jaribu kupita kwenye mtandao wa Vodacom tz kama kuna mawasiliano fanya.

Pole sana
 
Pole sana mkuu ila tumepata shule ya kutosha.Hata wife wangu lazima nimpe shule leo.
 
Niliwahi kuisikia kesi kama hii kwa mtu wa karibu na familia yangu.
Tofauti yeye ilikuwa ni laini ya airtel.
Jamaa alikuwa anaenda airtel anafunga baada ya muda anashangaa rafiki mwingine kishatapeliwa.
Cha msingi wataarifiwe ndugu na jamaa wote.
Na wao wawataarifu jamaa wengine.
Huu mchezo upo kitambo.
Ishu ya jamaa nilomtolea mfano ni ya mwaka jana.

Pia ningeomba ubadilishe jina la topic yako ili thread ipate viewers wengi tujifunze wengi kuepukana na wizi wa namna hii.

Pole sana mkuu.
 
Pole sana mkuu..hali ya sasa imekuwa mbaya, wahalifu wamekua na mbinu nyingi sana za kuwaliza watu. Tuwe makini sana
 
Niliwahi kuisikia kesi kama hii kwa mtu wa karibu na familia yangu.
Tofauti yeye ilikuwa ni laini ya airtel.
Jamaa alikuwa anaenda airtel anafunga baada ya muda anashangaa rafiki mwingine kishatapeliwa.
Cha msingi wataarifiwe ndugu na jamaa wote.
Na wao wawataarifu jamaa wengine.
Huu mchezo upo kitambo.
Ishu ya jamaa nilomtolea mfano ni ya mwaka jana.

Pia ningeomba ubadilishe jina la topic yako ili thread ipate viewers wengi tujifunze wengi kuepukana na wizi wa namna hii.

Pole sana mkuu.



Mkubwa hapa umenena,na huu mchezo unakuwa kwa kazi sana!!!
 
Pole Kamanda lakini nilipata Taarifa polisi wanawataalamu wa IT hawezi wakakusaidia?
 
Pole sana mkuu kwani hata mimi binafsi nishakumbana na mkasa kama wako lakini ilikuwa airtel. Hadi leo sina hamu nao
Mimi ilivyokuwa ni laini yangu nikahisi labda ina tatizo, hivyo nikaenda kuitengeneza upya lakini ikagoma nikaambiwa kuwa mbona inaonekana kuna mtu anaitumia.

Kwa kuwa yule ajenti ofisi yake ilikuwa ndogo nikaenda pale ofisi za airtel J Mall pale. Kuna dada upande wa it alinijibu kirahisi hata sikuamini na utapeli uliendelea kwa siku kama nne hivi.

Ikabidi niende pale makao makuu yao karibu na makutano ya barabara ya Ali Hassan Mwinyi na Kawawa. Pale nilikuta waathirika zaidi ya 8 kila mmoja anashangaa inakuwaje namba moja itumiwe na zaidi ya mtu mmoja. Baada ya kusumbuliwa sana na mimi kuchachamaa ndo wakam-block yule jamaa siku inayofuatia.

Athari zilizopatikana
1. Watu wengi aliwatapeli kwani jamaa wengi ambao ninafanya nao biashara aliwapiga hela
2. Alikuwa anawasiliana na watu kama vile ana menu ya majina yote kama niliyokuwanayo mie katika simu yangu
3. Ajabu alikuwa anatoa pesa kutoka airtel money ilhali password sikuwahi kumpa mtu yoyote hata mke wangu, kwani hata baada ya kuiblock nilikuta kuna balance ya 35,000Tzs
Wito wangu
1. Kama ni wafanyakazi wa hizi kampuni wasio waaminifu basi wajiangalie
2. Tabia za kuajiriana kwa kujuana ndio haya madhara yake wanakosa uadilifu na uaminifu kwa kampuni na wateja
3. Kampuni za simu anzisheni vitengo vya siri vya kuwachunguza wafanyakazi wenu, hii hata wafanyakazi wa benki vilevile itafaa kwani kuna baadhi ya wafanyakazi wenu sio wema na wana tamaa sana na maisha ya hali ya juu bila kuvuja jasho
 
TCRA wamewashindwa TBCcm Mpwa dont waste your time na hawa watu
 
Last edited by a moderator:
hawahawa vodacom ndio wahusika, ishu kama hizi sio za kuchukulia mzaha.. yani mi kinachoniuma zaidi ni sababu/kisingizio watakachotumia kuomba hela kwa mtu yani wanakupakazia shida za hovyo unakuwa kama ombaomba kumbe wala huna hiyo shida...

mkuu ingia website ya voda uwasiliane nao...
 
There isnt a stupid company like Vodacom,
 
vodacomTanzania mje huku mjibu kwanza haya maswali then na sisi tueleze yetu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom