wewe sijui unaongea nini, hiyo design ni ya iPhone 3, walichobadili ni unene, ukubwa na material tu kuwa aluminium badala ya plastic kama kwenye 3 na 3gs! Jobs alikuwa ameshatoka huko zamani, naona Cooks amekosa ubunifu na kuanza kurudi nyuma. Na kwenye saa angalia tena facts zako, saa bora mpaka sasani Moto360 kutoka motorola, hayomengine ni maboksi tu ya vijana kuvaa mkononi. Kampuni gani iliandika 16mp na ikawa 5mp?...labda kama unaongelea simu za kichina, na ubora wa picha si wingi wa pixels, apple wana picha bora tu na camera zao za 8mp kuzidi simu nyingi zenye 13mp camera. Naongea hivyo kama mnazi wa Apple Inc. sijawahi kununua smartphone yoyote zaidi ya iPhone, kuanzia 3 mpaka 5s zote nimeshamiliki kwa zaidi ya miezi sita kila moja, hii waliyotuletea sasa hivi haina mashiko na wameshatoka nje ya identity yao, PREMIUM! Safari hii nitabaki na 5s yangu, kwenye 6 wamenikosa, nikitaka kubadili simu nitanunua Samsung kwa mara ya kwanza, tena nitanunua Note Edge.