Dr. Chapa Kiuno
JF-Expert Member
- Sep 11, 2009
- 443
- 18
Monday, November 02, 2009 10:42 AM
MSICHANA WA kazi za ndani aliyefahamika kwa jina moja la Sakina [22] mkazi wa Mabibo Hostel amejikuta akiwa kwenye wakati mgumu wakati alipomuandalia chakula baba mwenye nyumba, alipoona mkewe amechelewa kurudi nyumbani kwake hapo.
Chanzo cha habari hii anayeishi karibu na lilipotokea tukio aliiambia NIFAHAMISHE kuwa msichana huyo alipigika kutokana na kitendo chake cha kumuandalia bosi wake wa kiume chakula.
Alidai kuwa wakati anaanza kazi kwa dada huyo miezi mitano iliyopita bosi wake wa kike alimwambia kuwa afanya kazi zote ila mambo yanayomuhusu mume wake asiyaingilie kabisa ikiwemo na kumuandalia chakula na kufua nguo za mume wake huyo.
Alidai siku ya tukio Jumamosi majira ya saa 3 usiku, msichana huyo alikuwa amepika chakula na kula na mtoto wake anayemlea mwenye umri wa miaka minne, na wakati huo bosi wake huyo wa kike alikuwa ametoka na kuchelewa kurudi na bosi wake wa kiume huyo alikuwa amerudi kwenye majira ya saa moja jioni.
Hivyo msichana huyo alipoona mama yake huyo amechelewa kurudi hadi majira ya saa 3 na nusu, aliona ni vyema amuandalie chakula bosi wake huyo kwa kuwa mama yao alikuwa amechelewa.
Alidai alimuandalia chakula hadi alipomaliza kula mama yake huyo alikuwa hajarudi na yeye aliingia ndani kulala.
Ilidaiwa kuwa mama huyo aliporudi ambapo ilidaiwa alikwenda kwenye sherehe ya Kitchen Patry aliingia nyumbani kwake hapo kwenye majira ya 4 na nusu usiku, na kuingia jikoni kumuandalia chakula mume wake ili waweze kula kwa pamoja.
Wakati alipomaliza kuandaa chakula na kumkaribisha mume wake huyo kipenzi asogee mezani wapate chakula kwa pamoja ndipo mume wake huyo alipomjibu He mbona mimi nimeshakula zamani Sakina alishaniandalia endelea tu mke wangu mi nishakula
Baada ya kupata majibu hayo kwa mume wake huyo moja kwa moja aliingia kwenye chumba alicholala msichana huyo na kumuamsha na kumuuliza baba alishakula na msichana huyo kujibu ee alishakula nilimuandalia
Bila kutarajia mama huyo alianza kipigo kwa msichana huyo na kumwambia nilikwambiaje wewe si nilikwambia kazi hiyo uniachie mwenyewe kwa nini ulimuandalia kwani yule mume wako? huku akiendelea kumpa kichapo cha nguvu
Kipigo kilivyokuwa cha nguvu ndipo msichana huyo uzalendo ukamshinda na kuanza kupiga kelele hadi baba huyo kukimbilia chumbani huko kuuliza imekuwaje ndipo msichana huyo alimwambia kuwa ananipiga kwa kuwa nilikuandalia chakula alishanikataza nisiwe ninakuandalia.
Alianza kumkemea mkewe kwa kumsihi sio kitendo kizuri na baba huyo kurudi chumbani kwake kulala, mama huyo alipooona amepata upenyo aliendelea kumpiga msichana huyo kwa hasira na msichana huyo kukimbilia nje huku akilia na ndipo majirani wa karibu walipokimbilia na kumsihi mwenzao huyo amsamehe.
NIFAHAMISHE siku iliyofuata ilitembelea eneo la tukio na kukuta msichana huyo akilalama akitaka mshahara wake ili aweze kurudi kwao na kudai anamdai dada huyo mshahara wa miezi mitatu nyuma.
Alipomwambia bosi wake huyo dhamira ya kutaka kuondoka kwao alimwambia asiondoke na kudai kuwa alikuwa na jazba na alimwambia alikuwa anamuonya kwani kuonywa ni kawaida akikosa.
Msichana huyo aliiambia nifahamishe kuwa anabaki hapo akisubiri kuandaliwa mshahara wake na akiupata ataondoka kwao.
Na Pilly Kigome, Dar