Apanda Mlima Kilimanjaro kwa Saa 24

Apanda Mlima Kilimanjaro kwa Saa 24

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,773
Reaction score
1,174
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ametoa Rai kwa Watanzania waendelee kujitokeza na kushiriki mashindano ya mbio za Baiskeli yanayofanyika ndani na nje ya nchi.

Ametoa rai hiyo leo Aprili 01, 2023 jijini Dar es Salaam alipokutana na Mwendesha Baiskeli bora Duniani Bw. Mike Leszek Mikulski kutoka nchini Poland ambaye amekuja nchini Tanzania kuweka rekodi ya kupanda Mlimani Kilimanjaro na kushuka kwa muda wa saa 24.

20230401_180047.jpg
 
🤣Hao wanaopanda siku 3 ni wagonjwa tu wa vifua pumu, visukari, vitambi na kutofanya mazoezi miguu mizito ila mimi sijawahi fika hapo ila nauhakika naupanda kwa masaa machache tu.
Ndoto hazijawahi kushindwa kitu.
Unaweza kuota unapaa juu kama tai
 
Huo mlima ukianza saa moja asubuhi saa saba mchana utakuwa kileleni

Hizi zingine huwa ni biashara za wabeba mizigo kuwachelewesha wateja au wateja wasio kuwa na haraka na wenye bajeti kubwa
Unajua Ina umbali wa km ngapi?

Usichukulie zile meta 5895 kama ndo umbali wake hizo meta ni za mwinuko kutoka usawa wa bahari na umbali kutoka chini ya mlima na kilele Cha mlima ni habari nyingine, unaweza Kuta Kuna km 60 Sasa km60 utumie masaa 2?
 
Ndugu yangu mimi sizungumzii mambo ya kufikirika

Najua unapopanda mlima huendi direct

Ni barabara yenye milima,tambarare na miteremko

Usipotaka kupoteza muda kushanga chemchem za maji na kulala njiani
Asubuhi Hadi mchana au alasiri unatoboa

Kumbuka sizungumzii wazee,na wengine wenye changamoto
Unajua Ina umbali wa km ngapi?

Usichukulie zile meta 5895 kama ndo umbali wake hizo meta ni za mwinuko kutoka usawa wa bahari na umbali kutoka chini ya mlima na kilele Cha mlima ni habari nyingine, unaweza Kuta Kuna km 60 Sasa km60 utumie masaa 2?
 
Back
Top Bottom