uwe hodari
JF-Expert Member
- Dec 16, 2022
- 4,041
- 8,636
Huo mlima utauona mrefu kupanda ukipanda na makundi maalumu km
Wanawake
Wazee
Watoto
Na wenye vitambi uzembe
Wanawake
Wazee
Watoto
Na wenye vitambi uzembe
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ametoa Rai kwa Watanzania waendelee kujitokeza na kushiriki mashindano ya mbio za Baiskeli yanayofanyika ndani na nje ya nchi.
Ametoa rai hiyo leo Aprili 01, 2023 jijini Dar es Salaam alipokutana na Mwendesha Baiskeli bora Duniani Bw. Mike Leszek Mikulski kutoka nchini Poland ambaye amekuja nchini Tanzania kuweka rekodi ya kupanda Mlimani Kilimanjaro na kushuka kwa muda wa saa 24.
View attachment 2573163
Unamaanisha kuanzia getini?nakuambia nimeshapanda mara 4 ule mlima. Mara ya mwisho ni july 2022. Tulienda kiofisi na waliotuchelewesha nii mademu na vibonge. MIIMA KILIMANJARO NAPANDA NA KUSHUKA MASAA 8 YANATOSHA VIZURI.
Be careful iko siku utawekewa jiwe la kumbukumbu mahali mwili umeachana na roho!Ni mind set yako uliyoijenga
Hata sisi tuliogopeshwa mara ya kwanza
Lkn tukagundua njian ni kitu chepesi tu, Njiani tulikuwa tunawapita makundi ya watu wanatembea polepole na kushangaa chemicgemi za maji
Nilikuwa na kamanda tukaiacha crew yetu tukaenda kwa joging ila guide akawa anatukataza tutapotea na bla bla kibao
Tulifika kituo cha kwanza kile ( sikumbuki jina)
Crew yetu tuliisubiri kwa masaa mawili ndio wakafika wakadai wamechoka tupumzkie
Hali ya hewa pale kweli ilibadilika baridi na chai kwenye jiko la gesi ilitumia dkk km kumi kupata moto kutokana na maji baridi sana wakati majumbani chai dkk tano tu imechemka
Tatizo mnashindwa kutofautisha kupanda mlima kwa kutalii ukiwa umerelax kwakuwa umetenga siku zako 3+
Ila kwenda kwa lengo la kufika kileleni kuanzia asubuhi hadi saa nane saa tisa utakuwa kileleni
Waache wajifanye wajuaji! Siku wakianza kuwekewa mawe ya kumbukumbu mahali roho zao ziliacha mwili ndio watajifunza!Mimi nimeupanda mara mbili kupitia machame gate. Achana na hawa madogo wanaoongea tu bila kuwa na experience yoyote. Wanauchukulia mlima KLM kama kijilima flani hivi bila kujua changamoto za hali ya hewa zilizopo ndizo zinazofanya safari iwe ndefu.