Kipindi hicho magazeti ya musiba ya kutukania wastaafu na viongozi wa dini yanapewa ruzuku leo musiba anaumwa msongo wa mawazo mlipaji mkuu wake hayupo tena, wafanyakazi wake wanamburuza mahakamani miezi 4 awajalipwa.Kiufupi, utawala uliopita umewashikisha adabu watu wengi sana. Angalau Diallo katoka hadharani na kusema ya Moyoni. Imagine wamiliki wa magazeti ya Mtanzania, Dimba na Rai ambao magazeti yao yamekufa, imagine Mawio, Mwanahalisi na Tanzania Daima, nao wameonja joto ya jiwe ya mwendazake. Acha watu waseme, wapumue, watoe ya moyoni. Kila mtu ana namna yake ya kumkumbuka mwendazake, msiwapangie watu cha kuongea.