Anthony Diallo anazeeka vibaya

Kiufupi, utawala uliopita umewashikisha adabu watu wengi sana. Angalau Diallo katoka hadharani na kusema ya Moyoni. Imagine wamiliki wa magazeti ya Mtanzania, Dimba na Rai ambao magazeti yao yamekufa, imagine Mawio, Mwanahalisi na Tanzania Daima, nao wameonja joto ya jiwe ya mwendazake. Acha watu waseme, wapumue, watoe ya moyoni. Kila mtu ana namna yake ya kumkumbuka mwendazake, msiwapangie watu cha kuongea.
Kipindi hicho magazeti ya musiba ya kutukania wastaafu na viongozi wa dini yanapewa ruzuku leo musiba anaumwa msongo wa mawazo mlipaji mkuu wake hayupo tena, wafanyakazi wake wanamburuza mahakamani miezi 4 awajalipwa.
 
Kiufupi, utawala uliopita umewashikisha adabu watu wengi sana. Angalau Diallo katoka hadharani na kusema ya Moyoni. Imagine wamiliki wa magazeti ya Mtanzania, Dimba na Rai ambao magazeti yao yamekufa, imagine Mawio, Mwanahalisi na Tanzania Daima, nao wameonja joto ya jiwe ya mwendazake. Acha watu waseme, wapumue, watoe ya moyoni. Kila mtu ana namna yake ya kumkumbuka mwendazake, msiwapangie watu cha kuongea.

Sawa waongee ila watoe sababu kwanini walishikishwa adabu...wasiseme mtu ni kichaa wakati alikuwa anatekeleza wajibu wake
 
ANTONY DIALLO ANAZEEKA VIBAYA

Kwanza kabisa nianze kwa dhati ya moyo wangu kumpongeza katibu wetu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tanzania (UVCCM) ndugu yetu, na kaka yetu Kenani Labani Kihongosi kwa jinsi anavofanya kazi kwa weledi mkubwa kama kijana mwenye maono na anaonesha kwa namna gani ni kiongozi bora kabisa ndani ya jumuiya yetu kwa muda mfupi ametuonesha dira kama vijana wa UVCCM tunatakiwa kuenenda kwa namna gani.

Katibu Kenani Labani Kihongosi anafahamika kwa uimara wake na misimamo thabiti isiyoyumba hasa linapokuja swala la kutetea masilahi ya watanzania wote hii tumeona maeneo mengi alipokuwa mkuu wa wilaya ya Arusha katika utumishi wake wote alisimama na wananchi vilevile kusimama kama kiongozi wa umoja wa vijana wa CCM Tanzania ndo maana hata tumeshuhudia amethubutu kumpa onyo bila woga mwenyekiti wa CHADEMA F. A. Mbowe kuwa awakanye na kuwafundisha adabu vijana wake maana wanakosa heshima kwa kiongozi mkuu wa nchi kiufupi vijana wa mzee Mbowe wanavuka mipaka yao na kuona wanauwezo wa kuamua au kuropoka chochote kitakachowajia akilini mwao,

Lakini ni katibu wa UVCCM Taifa ambaye ameinuka na kukemea kauli mbovu na za kejeli zilizotolewa na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza ndugu Antony Diallo katika moja ya mahojiano yake na kituo cha runinga cha Star TV hapo Nyuma, kauli za mwenyekiti huyo zimekikashifu Chama Cha Mapinduzi (CCM) Chama ambacho yeye mwenyewe ni kiongozi wake tena wa ngazi kubwa kabisa ya mkoa. Hapo Kenani Labani Kihongosi kama kijana wa nchi hii na jasiri, kijana mwenye uzalendo haswa ameshindwa kuvumilia nakuamua kutoka hadharani na kutoa onyo kali kwa waziri huyo wa zamani aliyehudumu zaidi ya wizara mbili ambaye ni kiongozi wa CCM mkoa wa Mwanza

Hivyo nimtie shime katibu wetu wa UVCCM Tanzania kwamba asonge mbele akaze buti sisi vijana tunamuunga mkono kwa asilimia zote tutamlinda, tutamshauli, tutamkosoa, lakini zaidi tutamtetea kwa nguvu zetu zote na kwa maarifa yetu yote kwasababu yeye ni jasiri mwongoza njia na tumeona kazi yake ameanza vizuri na kauli mbiu yake maridhawa kabisa ya Mtumishi wa wote hivyo hata mimi naungana na katibu wangu na kusapoti onyo lake kwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza kwamba aache mara moja hicho anachokisema maana anakikosea Chama na serikali ambayo ameitumikia na bado anaisimamia kwa cheo chake

Katika vitu ambavyo vimeshangaza wengi sana ni hiki kituko alichokifanya mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza bwana Antony Diallo, ambaye kimsingi yeye ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa lakini zaidi yeye ni mjumbe wa NEC ya CCM kwa cheo chake. Antony Diallo inawezekana uzee unamnyemelea kwa kasi tunaweza kusema hivo labda pengine ana truck record mbaya ya biashara zake ndo maana anaonesha chuki ya moja kwa moja kwa serikali ya awamu iliyopita, hebu tuangalia mambo yake kadhaa huko nyuma yanayozalisha chuki kubwa dhidi ya viongozi wa CCM

Antony Diallo akiwa hivo hivo mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza lakini ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Sahara Media Group (SMG) inayomiliki kituo cha televisheni cha Star TV, kituo cha radio cha Radio Free Afrika (RFA) na kituo cha radio cha Kiss FM, na king'amuzi cha Continental decoder katika utendaji wake wa hizo kampuni mwaka wa 2017 alikutwa na makosa makubwa mawili ambayo yalimwondolea kabisa Legacy yake kama kiongozi wa CCM ndani ya mkoa wa Mwanza ambao ni moja kati ya Majiji makubwa ndani ya nchi yetu na Afrika Mashariki kwa ujumla lakini makosa hayo yalimshushia heshima yeye kama mkurugenzi mtendaji wa vituo vikubwa vya kurusha matangazo ndani ya Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.

Antony Diallo alikabiliwa na kosa la ulimbikizaji wa kodi kutoka katika mamlaka za mapato Tanzania (TRA) kiasi cha shilingi za kitanzania Bilioni 4.5 na vituo vyake vikafungiwa ndo maana leo anaanza kutoa maneno ya chuki dhidi ya serikali ya Chama anachokiongoza yeye mwenyewe (CCM) lakini bado serikali anayoikejeli leo kupitia TRA wakampunguzia masharti wakamwambia ili vituo vyake vifunguliwe alipe Billion 2 kutoka katika zile 4.5 anazodaiwa na akafanya hivyo na mambo yakaendelea vizuri kwake. Hivyo unaweza ukaona ukosefu wa uadilifu katika uongozi wa Antony Diallo ulisababisha hasara kwa Taifa na kupoteza mapato yake mengi sana ambayo alikuwa anayakalia ndani ya taasisi anazozisimamia pale Mwanza.

Pia ni huyu Antony Diallo aliburuzwa katika Mahakama Kuu ya Kanda ya Mwanza kwa kushindwa kulipa mishahara wafanyakazi wake 20 kwa muda wa miezi 6 mfululizo na alikuwa anadaiwa kiasi cha shilingi milioni 100 kwa wafanyakazi hao, halafu leo anasimama kuwasema vibaya viongozi wa Serikali baada ya serikali kukagua madudu yake ambayo alikuwa anajificha kwa mwamvuli wa kuwa mwenyekiti wa CCM huku akifanya ubadhilifu mkubwa na kuingizia hasara Serikali na kukwamisha shughuli za maendeleo kwa watanzania. Atuachie Chama Chetu kama anaona amechoka milango ipo wazi aende huko akachague viongozi anaowafahamu yeye lakini hatutakubali kejeli kama hizi kwa Serikali yetu tutasimama imara na kueleza kwanini anaichukia Serikali huku sababu kubwa ikiwa ni kuweka mazoea ya kukwepa kodi alipobanwa ndo anaanza kuona serikali ya CCM na viongozi wake ni wabaya kwake.

Kwa nafasi ya Antony Diallo kama mwenyekiti wa CCM mkoa yeye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa hivyo ana maamuzi makubwa ya kuchagua viongozi kama aliyaona hayo kwanini hakufunguka tangu awali? kitu anachokifanya kwasasa ni uchochezi usiokuwa na faida ndani na nje ya CCM.

Kiongozi yoyote yeye ni mbeba maono sasa inapotokea anakiuka taratibu ni lazima tumueleze ukweli kuwa njia anayopita si sahihi. Antony Diallo bado alishutumiwa kutokupeleka stahiki za wafanyakazi wake katika mifuko ya hifadhi za kijamii PPF/NSSF huko alipobanwa tayari akaanza kuiona serikali kama haipo upande wake kwasababu inafichua maovu yake na kuyaweka wazi na hapo ndipo chuki yake na viongozi wa serikali ilipoanzia na kuota ndani ya moyo wake.

Antony Diallo huyu huyu amewahi kuwa waziri wa Maji na umwagiliaji ni nini alikifanya katika wizara hiyo pia akaja kuwa waziri wa Maliasili na Utalii hivi hata leo najua kabisa hapa kati yenu mnae soma andiko hili kuna uwezekano mkubwa ulikuwa hufahamu kama huyo Diallo alishawahi kuwa waziri katika nchi yetu hii

Sasa leo hii anaanza kuongea mambo yanayokikashifu Chama chetu kana kwamba anaongea maswala ya wafanyakazi wake, amesahau kabisa kuwa CCM ni taasisi kubwa inayotoa viongozi wakuu wa nchi ambao wanaongoza watanzania zaidi ya milioni 60 halafu leo anaanza kuzungumza vitu ambavyo vinaleta mkanganyiko mkubwa na kejeli nyingi kwa viongozi wetu hatutakubali yeye kama anazeeka basi azeeke kwa amani atuache akae kwa kutulia asitake kuanzisha malumbano yasiyokuwa na tija ndani ya CCM yetu.

Uongozi ni dhamana huwezi kujificha ndani ya CCM kwa kufanya mambo yako mabaya kwa jamii halafu yanapokuja kufichuka basi unaanza kuiona Serikali mbaya inaongozwa na viongozi wa tofauti nadhani Mwenyekiti huyu Diallo kuna vitu alitarajia atavipata kutoka katika awamu iliyopita lakini baada ya kuvikosa ndo mambo yalipoharibikia hapo sasa aache asianze kuamsha tena haya yamepita viongozi wetu ambao wamekwisha kufanya kazi katika taifa hili wanapaswa kuheshimiwa na siyo kukurupuka na kuanza kutoa kejeli ambazo kwanza jamii inayokuzunguka inakuona kama umechanganyikiwa kwasababu unaanza kusema kitu ambacho wewe mwenyewe umekifanyia maamuzi huyu mwenyekiti katukosea sana ingawa ni mtazamo wake lakini yeye kama kiongozi amevuka mipaka jambo ambalo CCM wanatakiwa kuliangalia mara mbili.

Ahsante.
Lakini Mkuu yeye au kampuni zake zililemewa au zilishindwa kulipa kodi,nae akajiongeza kulipa kwa awamu hadi akamaliza deni,hakukwepa kulipa kodi bali alilemewa kulipa kodi.
Diallo anadai mazingira ya biashara wakati wa Raisi Magufuli yaligeuka kuwa magumu,labda ndizo zababu zilizofanya biashara zake ziyumbe.Ugumu wa kufanya biashara tumeusikia sio tu kwake,hata Raisi SSH kasema hayo hayo.Wabunge akina Msukuma wamesema hayo hayo,sioni kama ametenda dhambi bali ameepuka dhambi kwa kuwa mkweli.
 
Sawa waongee ila watoe sababu kwanini walishikishwa adabu...wasiseme mtu ni kichaa wakati alikuwa anatekeleza wajibu wake
Siku zote, wafanyabiashara na wanasiasa wapo kwa maslahi yao, wala sio ya wananchi. Diallo alidhani kumpigia kampeni JPM kwa kutumia TV yake kungemfanya asilipe kodi, alipelekewa bili na TRA mpaka akataka kufunga ofisi zake. ALishika adabu, kwa kifupi.
 
Lakini Mkuu yeye au kampuni zake zililemewa au zilishindwa kulipa kodi,nae akajiongeza kulipa kwa awamu hadi akamaliza deni,hakukwepa kulipa kodi bali alilemewa kulipa kodi.
Diallo anadai mazingira ya biashara wakati wa Raisi Magufuli yaligeuka kuwa magumu,labda ndizo zababu zilizofanya biashara zake ziyumbe.Ugumu wa kufanya biashara tumeusikia sio tu kwake,hata Raisi SSH kasema hayo hayo.Wabunge akina Msukuma wamesema hayo hayo,sioni kama ametenda dhambi bali ameepuka dhambi kwa kuwa mkweli.
Lakini kwa nini hakuachia ngazi kama anajua yupo kwenye serikali ya kichaa
 
Siku zote, wafanyabiashara na wanasiasa wapo kwa maslahi yao, wala sio ya wananchi. Diallo alidhani kumpigia kampeni JPM kwa kutumia TV yake kungemfanya asilipe kodi, alipelekewa bili na TRA mpaka akataka kufunga ofisi zake. ALishika adabu, kwa kifupi.
Hakika umeeleza vyema mwenye upeo amekuelewa
 
Kiufupi, utawala uliopita umewashikisha adabu watu wengi sana. Angalau Diallo katoka hadharani na kusema ya Moyoni. Imagine wamiliki wa magazeti ya Mtanzania, Dimba na Rai ambao magazeti yao yamekufa, imagine Mawio, Mwanahalisi na Tanzania Daima, nao wameonja joto ya jiwe ya mwendazake. Acha watu waseme, wapumue, watoe ya moyoni. Kila mtu ana namna yake ya kumkumbuka mwendazake, msiwapangie watu cha kuongea.
Pole sana

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
 
Kwa ufupisho ni kwamba bwana Antony Diallo anazeeka vibaya
Napinga hoja hiyo.Katiba yetu pamoja na mapungufu yake inatoa haki ya kutoa maoni kwa kila mmoja wetu.
Pili kila mtu alijua kuwa kulikiwa na ubambikiaji watu wa kesi mbali mbali ambazo mama yetu hataki hayo mambo yaendelee.
 
Napinga hoja hiyo.Katiba yetu pamoja na mapungufu yake inatoa haki ya kutoa maoni kwa kila mmoja wetu.
Pili kila mtu alijua kuwa kulikiwa na ubambikiaji watu wa kesi mbali mbali ambazo mama yetu hataki hayo mambo yaendelee.
Ila uliisikia kauri ya Diallo?
 
ANTONY DIALLO ANAZEEKA VIBAYA

Kwanza kabisa nianze kwa dhati ya moyo wangu kumpongeza katibu wetu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tanzania (UVCCM) ndugu yetu, na kaka yetu Kenani Labani Kihongosi kwa jinsi anavofanya kazi kwa weledi mkubwa kama kijana mwenye maono na anaonesha kwa namna gani ni kiongozi bora kabisa ndani ya jumuiya yetu kwa muda mfupi ametuonesha dira kama vijana wa UVCCM tunatakiwa kuenenda kwa namna gani.

Katibu Kenani Labani Kihongosi anafahamika kwa uimara wake na misimamo thabiti isiyoyumba hasa linapokuja swala la kutetea masilahi ya watanzania wote hii tumeona maeneo mengi alipokuwa mkuu wa wilaya ya Arusha katika utumishi wake wote alisimama na wananchi vilevile kusimama kama kiongozi wa umoja wa vijana wa CCM Tanzania ndo maana hata tumeshuhudia amethubutu kumpa onyo bila woga mwenyekiti wa CHADEMA F. A. Mbowe kuwa awakanye na kuwafundisha adabu vijana wake maana wanakosa heshima kwa kiongozi mkuu wa nchi kiufupi vijana wa mzee Mbowe wanavuka mipaka yao na kuona wanauwezo wa kuamua au kuropoka chochote kitakachowajia akilini mwao,

Lakini ni katibu wa UVCCM Taifa ambaye ameinuka na kukemea kauli mbovu na za kejeli zilizotolewa na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza ndugu Antony Diallo katika moja ya mahojiano yake na kituo cha runinga cha Star TV hapo Nyuma, kauli za mwenyekiti huyo zimekikashifu Chama Cha Mapinduzi (CCM) Chama ambacho yeye mwenyewe ni kiongozi wake tena wa ngazi kubwa kabisa ya mkoa. Hapo Kenani Labani Kihongosi kama kijana wa nchi hii na jasiri, kijana mwenye uzalendo haswa ameshindwa kuvumilia nakuamua kutoka hadharani na kutoa onyo kali kwa waziri huyo wa zamani aliyehudumu zaidi ya wizara mbili ambaye ni kiongozi wa CCM mkoa wa Mwanza

Hivyo nimtie shime katibu wetu wa UVCCM Tanzania kwamba asonge mbele akaze buti sisi vijana tunamuunga mkono kwa asilimia zote tutamlinda, tutamshauli, tutamkosoa, lakini zaidi tutamtetea kwa nguvu zetu zote na kwa maarifa yetu yote kwasababu yeye ni jasiri mwongoza njia na tumeona kazi yake ameanza vizuri na kauli mbiu yake maridhawa kabisa ya Mtumishi wa wote hivyo hata mimi naungana na katibu wangu na kusapoti onyo lake kwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza kwamba aache mara moja hicho anachokisema maana anakikosea Chama na serikali ambayo ameitumikia na bado anaisimamia kwa cheo chake

Katika vitu ambavyo vimeshangaza wengi sana ni hiki kituko alichokifanya mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza bwana Antony Diallo, ambaye kimsingi yeye ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa lakini zaidi yeye ni mjumbe wa NEC ya CCM kwa cheo chake. Antony Diallo inawezekana uzee unamnyemelea kwa kasi tunaweza kusema hivo labda pengine ana truck record mbaya ya biashara zake ndo maana anaonesha chuki ya moja kwa moja kwa serikali ya awamu iliyopita, hebu tuangalia mambo yake kadhaa huko nyuma yanayozalisha chuki kubwa dhidi ya viongozi wa CCM

Antony Diallo akiwa hivo hivo mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza lakini ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Sahara Media Group (SMG) inayomiliki kituo cha televisheni cha Star TV, kituo cha radio cha Radio Free Afrika (RFA) na kituo cha radio cha Kiss FM, na king'amuzi cha Continental decoder katika utendaji wake wa hizo kampuni mwaka wa 2017 alikutwa na makosa makubwa mawili ambayo yalimwondolea kabisa Legacy yake kama kiongozi wa CCM ndani ya mkoa wa Mwanza ambao ni moja kati ya Majiji makubwa ndani ya nchi yetu na Afrika Mashariki kwa ujumla lakini makosa hayo yalimshushia heshima yeye kama mkurugenzi mtendaji wa vituo vikubwa vya kurusha matangazo ndani ya Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.

Antony Diallo alikabiliwa na kosa la ulimbikizaji wa kodi kutoka katika mamlaka za mapato Tanzania (TRA) kiasi cha shilingi za kitanzania Bilioni 4.5 na vituo vyake vikafungiwa ndo maana leo anaanza kutoa maneno ya chuki dhidi ya serikali ya Chama anachokiongoza yeye mwenyewe (CCM) lakini bado serikali anayoikejeli leo kupitia TRA wakampunguzia masharti wakamwambia ili vituo vyake vifunguliwe alipe Billion 2 kutoka katika zile 4.5 anazodaiwa na akafanya hivyo na mambo yakaendelea vizuri kwake. Hivyo unaweza ukaona ukosefu wa uadilifu katika uongozi wa Antony Diallo ulisababisha hasara kwa Taifa na kupoteza mapato yake mengi sana ambayo alikuwa anayakalia ndani ya taasisi anazozisimamia pale Mwanza.

Pia ni huyu Antony Diallo aliburuzwa katika Mahakama Kuu ya Kanda ya Mwanza kwa kushindwa kulipa mishahara wafanyakazi wake 20 kwa muda wa miezi 6 mfululizo na alikuwa anadaiwa kiasi cha shilingi milioni 100 kwa wafanyakazi hao, halafu leo anasimama kuwasema vibaya viongozi wa Serikali baada ya serikali kukagua madudu yake ambayo alikuwa anajificha kwa mwamvuli wa kuwa mwenyekiti wa CCM huku akifanya ubadhilifu mkubwa na kuingizia hasara Serikali na kukwamisha shughuli za maendeleo kwa watanzania. Atuachie Chama Chetu kama anaona amechoka milango ipo wazi aende huko akachague viongozi anaowafahamu yeye lakini hatutakubali kejeli kama hizi kwa Serikali yetu tutasimama imara na kueleza kwanini anaichukia Serikali huku sababu kubwa ikiwa ni kuweka mazoea ya kukwepa kodi alipobanwa ndo anaanza kuona serikali ya CCM na viongozi wake ni wabaya kwake.

Kwa nafasi ya Antony Diallo kama mwenyekiti wa CCM mkoa yeye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa hivyo ana maamuzi makubwa ya kuchagua viongozi kama aliyaona hayo kwanini hakufunguka tangu awali? kitu anachokifanya kwasasa ni uchochezi usiokuwa na faida ndani na nje ya CCM.

Kiongozi yoyote yeye ni mbeba maono sasa inapotokea anakiuka taratibu ni lazima tumueleze ukweli kuwa njia anayopita si sahihi. Antony Diallo bado alishutumiwa kutokupeleka stahiki za wafanyakazi wake katika mifuko ya hifadhi za kijamii PPF/NSSF huko alipobanwa tayari akaanza kuiona serikali kama haipo upande wake kwasababu inafichua maovu yake na kuyaweka wazi na hapo ndipo chuki yake na viongozi wa serikali ilipoanzia na kuota ndani ya moyo wake.

Antony Diallo huyu huyu amewahi kuwa waziri wa Maji na umwagiliaji ni nini alikifanya katika wizara hiyo pia akaja kuwa waziri wa Maliasili na Utalii hivi hata leo najua kabisa hapa kati yenu mnae soma andiko hili kuna uwezekano mkubwa ulikuwa hufahamu kama huyo Diallo alishawahi kuwa waziri katika nchi yetu hii

Sasa leo hii anaanza kuongea mambo yanayokikashifu Chama chetu kana kwamba anaongea maswala ya wafanyakazi wake, amesahau kabisa kuwa CCM ni taasisi kubwa inayotoa viongozi wakuu wa nchi ambao wanaongoza watanzania zaidi ya milioni 60 halafu leo anaanza kuzungumza vitu ambavyo vinaleta mkanganyiko mkubwa na kejeli nyingi kwa viongozi wetu hatutakubali yeye kama anazeeka basi azeeke kwa amani atuache akae kwa kutulia asitake kuanzisha malumbano yasiyokuwa na tija ndani ya CCM yetu.

Uongozi ni dhamana huwezi kujificha ndani ya CCM kwa kufanya mambo yako mabaya kwa jamii halafu yanapokuja kufichuka basi unaanza kuiona Serikali mbaya inaongozwa na viongozi wa tofauti nadhani Mwenyekiti huyu Diallo kuna vitu alitarajia atavipata kutoka katika awamu iliyopita lakini baada ya kuvikosa ndo mambo yalipoharibikia hapo sasa aache asianze kuamsha tena haya yamepita viongozi wetu ambao wamekwisha kufanya kazi katika taifa hili wanapaswa kuheshimiwa na siyo kukurupuka na kuanza kutoa kejeli ambazo kwanza jamii inayokuzunguka inakuona kama umechanganyikiwa kwasababu unaanza kusema kitu ambacho wewe mwenyewe umekifanyia maamuzi huyu mwenyekiti katukosea sana ingawa ni mtazamo wake lakini yeye kama kiongozi amevuka mipaka jambo ambalo CCM wanatakiwa kuliangalia mara mbili.

Ahsante.
Magufuli kwa nyakati tofauti, akiwa mzima wa afya alifanya mengi mazuri.
Lakini siyo siri kuwa dalili mbaya ya mambo mabaya aliyofanya , zinazothibitisha kuwa na faili Mirembe ndio zimemuondolea yote mazuri aliyofanya.
 
Back
Top Bottom