Ansbert Ngurumo: Kikao cha siri ofisini kwa DCI kiliamua Mbowe na Wenzake wapelekwe mahakamani Jumanne wanyimwe dhamana

Kikao cha siri ofisini kwa DCI Alhamisi kiliamua Mbowe na wenzake wapelekwe mahakamani Jumanne 17:03:2018, wanyimwe dhamana, kupima joto. Leo Jumatatu katika kikao cha Mwanza, ukumbi wa BoT, kwa maagizo kutoka juu, azimio ni "kamata, funga, poteza, ua watu hawa" kabla ya 26:04:08

Daaah yametimia asee
 
Ngurumo unaweza kudanganya watu wengi lakini sio wote. Ulichoandika hapa ni mpango unaosukwa ndani ya CHADEMA kupoteza watu ili serikali ionekane ndio imefanya. Vyombo vya usalama someni kwa makini vitu anavyoondika huyu Ansbert Ngurumo, ama kwa kudhani watu ni wajinga au kujiamini sana anajikuta anatoa mrejesho wa mipango ya ndani ya CHADEMA.
Oky na Leo ilivyotokea n chadema wamepanga??
Halafu unasema una hekima?????
 
Kwa hali ilivyo Tanzania tunaweza kupigwa n.a. kaanchi kadogo kama Malawi naomba tuwaheshimu majirani zetu sana.
 
Inauma mnadanganya watoto wadogo kama nondo wanaharibu maisha yao nyie wala hamjali ili mradi muwafurahishe wazungu!
Inasikitisha sana kuona nchi ambayo iliitwa kisiwa cha amani hivi sasa inabadilika kuwa bonde la uvuli wa mauti.
 
Shetani mkubwa wewe Siri. Afu we ungejuaje. Hiyo ni logical tu. Wamevunja sheria. Wameandamana. Sasa ashikwe nani. Mbona mko fake hivyo. Mtu kakimbia eti huku hatari sasa mkimbizi. Mbona haoti kabla ya Watu kufa. Angemwambia mbowe ahairishe
Shida sio kukamatwa?? Shida ni kwanni mnawanyima dhamana wakati kesi zao zinaruhusu wapewe dhamana..... Mnawanyima kwa faida ya nani na hiyo ndio concern ya Ansbert
... Sio kukamatwa maana hilo lilitegemewa lakini kuwanyima dhamana ni kuwanyima haki zao kama tofauti huioni basi unahaki ya kumuita mwenzio shetani!!!
 
Ni anahisi kuwa ni raisi wa Tanzania, anataka kutuletea maendeleo - Kama viongozi wa nchi zilizo endelea ambao hawakuishi milele. Hivyo usitumie kuishi milele kumkatisha tamaa raisi wetu. Je maraisi Amerika wameishi milele? ni raisi gani mzuri aliye wahi kuishi milele? Je wewe utaishi milele? Kwa hiyo unataka aiuze nchi yetu kwa sababu hataishi milele!
Anamaanisha madaraka yanapita tu na kwamba ipo siku atakufa na atalipia mabaya yote aliyoyafanya sababu kwa vitendo vyake hivi anaanzaje kuepuka HUKUMU ya Mungu ya moto wa milele

Magufuli ataenda kuzimu tu na atajutia machafu yote aliofanya
 
Mungu sikuhizi anawajali wapinzani tu! Serikali mungu haioni? Mbona ndiyo inafanikiwa tu?
Serikali imefanikiwa kwenye nini??? Au hujui hata mchawi anaweza kukufanya upande cheo?? Sio kila mafanikio ni mkono wa Mungu mengine ni akili za kibinadamu tu ndio maana bado maskini kama Mungu angekua upande wetu tusingekuwa tunawatanzania zaidi ya million 35 wanaosurvive chini ya dola moja kwa siku poa tusingekuwa na wananchi million 30 wasiokuwa na access kwa maji safi na salama!!
 
Ansbert Ngurumu ulichosema jana kimetimia. Unabii umetimia. Kweli hii serekali inavuja kama alivyopata kusema Dr Slaa. Kila mnachopanga kukifanya mkimaliza kikao tu siri inavuja.
 
Kuna watu utafikiri wenyewe wana sehemu nyingine ya kukimbilia. Kumbe watakaoteseka hasa ni mama zetu, dada zetu na watoto wetu. Nilikuwa Congo mwaka juzi. Niliyoyaona kule yanatisha. Ee Mungu kikombe hiki na kiipite nchi yangu niipendayo. Mungu Ibariki Tanzania
Mkuu hili la kuomba kwa waamini ni jema sana lakini kuna wanaoamini mitutu zaidi katika kuleta amani.
Kikubwa kutenda haki kwa hivi tujiulize haki ikoje Tz
 
Back
Top Bottom