Anna Mghwira: Tuendeleze mjadala wa Mikopo ya Elimu ya Juu na tuchukue hatua

Mama anzisha harambee hapa hapa JF tunatosha kufanikisha hili jambo.
Tuanze tu, maana tayari wanafunzi kadhaa waliotangazwa kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada ama sifa walikuwa zaidi ya elfu kumi (10,000) wengi sana hawa kuwapoteza bilaujuzi wala sifa za kitaaluma. Hiki kijiwe cha JF kikianza tunaweza kukusanya zaidi ya m400 kwa mchango wa elfu moja tu. Tuwaombe moderators wa jukwaa watusaidie...tuweke akaunti ya kutuma. Ili ikiwezekana mhula mpya unapoanza tuwe na kitu cha kuwapa walengwa. Itakuwa thawabu kubwa kwa nchi yetu, kumsaidia mtu kujisaidia. Asante sana kwa maoni haya.
 
Naafiki mfuko uanzishwe. Niliahidi kupendekeza ninaoamini mnalandana kimawazo kuhusu Elimu. Kabla ya kupendekeza muundo,leo nikutajie hadharani angalao wawili tu. 1. Mh. Easter Bulaya. 2. Mzee wetu Reginald Mengi. 3........,4....... Hao wengine nitakupa baadaye.
Mimi ni scientist by profession,na ni Mtafiti. Nina tabia ya kutaka ukweli,na ni result-oriented person. Hutaka kuona utafiti ukianza ili kupata ukweli, utakaoakisi hali ya matokeo tunayotarajia. Ninaomba nipendekeze yafuatayo kwa uchache
1. Jamii ikupongeze kwa Juhudi zako.
2. Pata wanasheria,wasomi na wachumi (mnaoendana) kimtizamo,muchambue wazo hili kiutafiti,ili liweze kumerge na sera ya Taifa ya Elimu.
3. As a fund, iwe revolving kama ulivyosema,na ikibidi,itengenezewe mfumo fulani wa hisa (nina mfano) wa nchi iliyofanikiwa kivile.
Kwa leo niishie hapo Mama yetu. Mungu akutangulie.
Kididimo,

Asante kwa maoni yako. Nitajaribu kuwasiliana na hao uliowataja, hata mimininaafiki mapendekezo yako. Kwa kuanzia tuna kamati ndogo Arusha inayoratibu hatua za mwanzo. Tutaendelea nayo. Kuna mapendekezo JF ianze ili hatua za mwanzo za uchangiaji zianze na wanafunzi wenye sifa kupata mkopo waanze mwezi huu mwishoni vyuo vitakapofunguliwa. Hili linatoa nafasi ya kuharakisha hatua hizi. Kamati ikamilishe majukmu yake, ...baada ya michango na kuwapa wahusika wachache , utafiti uanze ili kutoa picha pana ya tatizo. kwa sasa ninafahamu / nimetafiti kidogo na kujua kuwa zaidi ya wanafunzi laki 400 hawana mikopo. Hawa ni wa daraja la 1&2. Wanafunzi takribani wote wa daraja la 3 na 4 wameachwa nje kabisa, hawajulikani walipo na wanachofanya.

Mtaji wetu nama moja wa kufikia nchi yaviwanda niwatumishi wenye ujuzi. Ninaamini lengo la viwanda hivi nipamoja na kutoa ajira nyingi na bora kwa watanzania kwanza. Kwa hiyo tuna kila sababu ya kutaka wawe na ujuzi wa kila aina. Hili pia litaangaliwa na utafiti huu. Tuanzie hapa. Asante
 
Ninaikumbuka vema kauli ya mama Salma Kikwete kuwa nanukuu: " Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako." Leo watoto wa wenzetu wameingia tatizo la kukosa mikopo ya elimu ya juu; tuwasaidie kama watoto wetu.

Ninapenda kuwaomba akina mama wote nikianza na Mhe mama Salma Kikwete aliyeasisi usemi na hatua hii, tushirikiane kunusuru maisha ya elimu ya watoto walioko vyuoni wenye sifa ya kuwa na mikopo lakini hawakufanikiwa kupata mkopo. Tuwahamasishe vijana waliobakia mitaani na majumbani kujiunga na vyuo vikuu kuanua akili zao changa kukidhi ushindani wa sasa kimaisha.

Naomba akina mama wote viongozi, wazazi, walezi, wafanya bishara, waajiriwa, wanaharakati bila kujali itikadi zetu za aina yoyote tusimame kama wanawake wazazi wenye nia kuejnga taifa la watu walioelimika tuunde mfuko wa kuwasiadia watoto wetu wafanikiwe kumaliza masomo yao kwa ujenzi wa taifa letu.

Nikitoka na mama Kikwete ninaomba wake za marais wote waliopita kuanzia na mama Karume (mzee marehemu na Rais aliyemaliza mda wake) mpaka mama Janet Magufuli anayenivutia sana kwa kuonesha moyo wa amani sana kwa taifa letu.

Baada ya hao nimuombe mama Anna Makinda na wabunge wanawake wote waliopo na waliomaliza tangu uhuru wa nchi yetu tuungane kumsaidia kila mtoto wa Tanzania mwenye uwezo wa kusoma asome.

Kisha kwa niaba ya wanawake wafanya bishara niombe kitengo cha wanawake cha TCCIA, Baraza la Biashara la wanawake...tukubali wito huu: Tuungane kama wazazi na walezi chini ya kauli mbiu: Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako...tuunde mfuko wa elimu kwa ajili ya vijana wetu.

Niombe vyama vya wana-taaaluma: waalimu, madaktari, wahandisi, watumishi wa umma, mabenki, makampuni yote ya ndani na ya kigeni, asasi za kiraia za ndni na za kimataifa, balozi zetu zote, tuungane kuunda chombo hiki kuwasaidia vijana wetu.

Nimeguswa sana na mahangaiko ya vijana wa vyuo vikuu. Ninawashukuru wachache waliofika kwangu kueleza changamoto zao. Mmenihamasisha kuchangia kidogo elimu yenu lakini ninaomba hili liwe suala la kitaifa.

Ninaomba wanawake wenzangu popote tulipo tuwasiliane tuunde umoja huu kuwaimarisha na kuwapa tumaini vijana na janga la kukosa elimu ya juu kama wana sifa za kuipata.

Tuweke kando siasa, dini, kabila, ukanda ama aina yoyote ya kigezo kufanikisha jambo hili. Ninawashukru sana. Kesho kuna wanafunzi watashindwa kufanya mitihani kwa kukosa ada kidogo tu ya laki kuanzia 5-8. Mfuko wa mama Salma, Mfuko wa mama Mkapa wa Fursa sawa kwa wote, Taasisi ya Benjamini mkapa, Taasisi ya Jakaya Kikwete, Taasisi ya Mwalimu Nyerere, na zingine, tusaidiane kukamilisha azima hii. Na mimi nimeanzisha Taasisi ya Mama Anna Mghwira kwa ajili ya kushughulikia masuala ya aina hii.

Nitawashukuru sana kwa niaba ya vijana wetu, tuenzi elimu yao kwa kuunganisha nguvu zetu hivi. Mnisamehe kwa kuandika mtandaoni. Nimejaribu njia za kawaida za simu sikufanikiwa sana. Hapa ninajua kila moja atapata taarifa. Mapungufu yangu yasizuie jambo hili kutendeka. Jinsi tulivyo changia madawati, sasatuchangie elimu ya juu.

Niombe wizara na Bodi ya mikopo ya wanafunzi kutoa ushirikiano tutakapouhitaji utaalamu muwe nasi bega kwa bega.

Mungu atubariki wote, aibariki Tanzania.

Asanteni tena, ni mimi mama Anna Mghwira

Mhe Lowassa katika manifesto yake ya kutaka kuingia Ikulu alikuwa na agenda yake muhimu sana kwa taifa 1. Elimu 2. Elimu 3. Elimu na kuahidi kuwa watoto wa taifa la Tanzania watasoma bure kuanzia chekechea(nursery) mpaka chuo kikuu bure na wale wote waliosomeshwa kwa mikopo watasamehewa, kwani ni kodi iliwasomesha! Watanzania walichagua mwenye faslisafa ya kuwa watoto watasoma bure kutoka nursery mpaka kidato cha nne(form four). Kule kuomba mchango kutoka kwa wahisani na wabunge kuchanga wakati Watanzania walichagua kusoma mpaka kidato cha nne unaudhi na kusumbua raia wema wakati wanafurahi walichochagua. Let them wait mpaka next election 2020 ili tuone Watanzania wanataka nini! Please tumechagua wenyewe na tunafurahia as 2020 siyo mbali.
 
Asante mama Mghwira
(1) Mfuko shughuli zake ziwe transparent, ielezwe wapi pesa inatoka, na shughuli zote za kutoa hizo pesa ziwe transparent

(2) Mfuko usiwe na upendeleo, vigezo viwekwe na wanaoqualify wapate usaidizi bila ubaguzi

(3) Mfuko ushirikiane na serikali, upatiwe msaada wa kibalozi huko nje ya nchi katika kuwatafuta wasamaria wema kuuchangia

(4)Mfuko uingie mkataba na wanufaika, kuwa hata wao baadae watakuja kusaidia kuutunisha kama wao walivyosaidiwa

(5)Mfuko uongee na viongozi wote wa dini, ziwepo sadaka maalum za waumini kuutunisha mfuko huu wa elimu

(6)Mfuko utatafute USSD code maalum kutoka TCRA ili watu waweze kuuchangia kupitia sms

(7) Mfuko utoe account yake, na uwashawishi watu walipie kwenye account hiyo kwa kukatwa asilimia 0.1 ya mshahara wao juu kwa juu na mabenki mishahara yao inapopitia na kuingizwa kwenye accont hiyo, hii inasaidia mtu asinotice makato hayo, lakini infact anakuwa anachangia!
Gamba la Nyoka,

Asante sana kwa maoni yako. Yote yatazingatiwa.

Tutakuwa na bima pia kwa mfuko mzima na kwa mikopo itakayotolewa. Wataalamu wa fedha na bima watausaidia mfuko kujua njia bora za kujiendesha.

Asante sana
 
Tuanze tu, maana tayari wanafunzi kadhaa waliotangazwa kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada ama sifa walikuwa zaidi ya elfu kumi (10,000) wengi sana hawa kuwapoteza bilaujuzi wala sifa za kitaaluma. Hiki kijiwe cha JF kikianza tunaweza kukusanya zaidi ya m400 kwa mchango wa elfu moja tu. Tuwaombe moderators wa jukwaa watusaidie...tuweke akaunti ya kutuma. Ili ikiwezekana mhula mpya unapoanza tuwe na kitu cha kuwapa walengwa. Itakuwa thawabu kubwa kwa nchi yetu, kumsaidia mtu kujisaidia. Asante sana kwa maoni haya.
Hatuwapi tunawakopesha wote wenye sifa, tutafute wanasheria wazuri waandae mkatamba ambao hauna riba, tuanze na hiyo elfu moja kuanzia April mosi. Nb nasikia na wewe ni mwanasheria hivyo tusaidie
 
Kididimo,

Asante kwa maoni yako. Nitajaribu kuwasiliana na hao uliowataja, hata mimininaafiki mapendekezo yako. Kwa kuanzia tuna kamati ndogo Arusha inayoratibu hatua za mwanzo. Tutaendelea nayo. Kuna mapendekezo JF ianze ili hatua za mwanzo za uchangiaji zianze na wanafunzi wenye sifa kupata mkopo waanze mwezi huu mwishoni vyuo vitakapofunguliwa. Hili linatoa nafasi ya kuharakisha hatua hizi. Kamati ikamilishe majukmu yake, ...baada ya michango na kuwapa wahusika wachache , utafiti uanze ili kutoa picha pana ya tatizo. kwa sasa ninafahamu / nimetafiti kidogo na kujua kuwa zaidi ya wanafunzi laki 400 hawana mikopo. Hawa ni wa daraja la 1&2. Wanafunzi takribani wote wa daraja la 3 na 4 wameachwa nje kabisa, hawajulikani walipo na wanachofanya.

Mtaji wetu nama moja wa kufikia nchi yaviwanda niwatumishi wenye ujuzi. Ninaamini lengo la viwanda hivi nipamoja na kutoa ajira nyingi na bora kwa watanzania kwanza. Kwa hiyo tuna kila sababu ya kutaka wawe na ujuzi wa kila aina. Hili pia litaangaliwa na utafiti huu. Tuanzie hapa. Asante
Asante. Naomba uwaombe Moderators waiweke hii thread kama "Sticky Thread" kwa vile ni endelevu,na tunahitaji kuchangia pia. Pia mimi,niko tayari kuanza uchangiaji,ila tuone njia nzuri ya kutumia ID zetu humu JF! Wengi siyo verified users na huenda hawatahitaji kuwa exposed publicly. Nina nia njema. Ubarikiwe mama yetu.
 
Ninaikumbuka vema kauli ya mama Salma Kikwete kuwa nanukuu: " Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako." Leo watoto wa wenzetu wameingia tatizo la kukosa mikopo ya elimu ya juu; tuwasaidie kama watoto wetu.

Ninapenda kuwaomba akina mama wote nikianza na Mhe mama Salma Kikwete aliyeasisi usemi na hatua hii, tushirikiane kunusuru maisha ya elimu ya watoto walioko vyuoni wenye sifa ya kuwa na mikopo lakini hawakufanikiwa kupata mkopo. Tuwahamasishe vijana waliobakia mitaani na majumbani kujiunga na vyuo vikuu kuanua akili zao changa kukidhi ushindani wa sasa kimaisha.

Naomba akina mama wote viongozi, wazazi, walezi, wafanya bishara, waajiriwa, wanaharakati bila kujali itikadi zetu za aina yoyote tusimame kama wanawake wazazi wenye nia kuejnga taifa la watu walioelimika tuunde mfuko wa kuwasiadia watoto wetu wafanikiwe kumaliza masomo yao kwa ujenzi wa taifa letu.

Nikitoka na mama Kikwete ninaomba wake za marais wote waliopita kuanzia na mama Karume (mzee marehemu na Rais aliyemaliza mda wake) mpaka mama Janet Magufuli anayenivutia sana kwa kuonesha moyo wa amani sana kwa taifa letu.

Baada ya hao nimuombe mama Anna Makinda na wabunge wanawake wote waliopo na waliomaliza tangu uhuru wa nchi yetu tuungane kumsaidia kila mtoto wa Tanzania mwenye uwezo wa kusoma asome.

Kisha kwa niaba ya wanawake wafanya bishara niombe kitengo cha wanawake cha TCCIA, Baraza la Biashara la wanawake...tukubali wito huu: Tuungane kama wazazi na walezi chini ya kauli mbiu: Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako...tuunde mfuko wa elimu kwa ajili ya vijana wetu.

Niombe vyama vya wana-taaaluma: waalimu, madaktari, wahandisi, watumishi wa umma, mabenki, makampuni yote ya ndani na ya kigeni, asasi za kiraia za ndni na za kimataifa, balozi zetu zote, tuungane kuunda chombo hiki kuwasaidia vijana wetu.

Nimeguswa sana na mahangaiko ya vijana wa vyuo vikuu. Ninawashukuru wachache waliofika kwangu kueleza changamoto zao. Mmenihamasisha kuchangia kidogo elimu yenu lakini ninaomba hili liwe suala la kitaifa.

Ninaomba wanawake wenzangu popote tulipo tuwasiliane tuunde umoja huu kuwaimarisha na kuwapa tumaini vijana na janga la kukosa elimu ya juu kama wana sifa za kuipata.

Tuweke kando siasa, dini, kabila, ukanda ama aina yoyote ya kigezo kufanikisha jambo hili. Ninawashukru sana. Kesho kuna wanafunzi watashindwa kufanya mitihani kwa kukosa ada kidogo tu ya laki kuanzia 5-8. Mfuko wa mama Salma, Mfuko wa mama Mkapa wa Fursa sawa kwa wote, Taasisi ya Benjamini mkapa, Taasisi ya Jakaya Kikwete, Taasisi ya Mwalimu Nyerere, na zingine, tusaidiane kukamilisha azima hii. Na mimi nimeanzisha Taasisi ya Mama Anna Mghwira kwa ajili ya kushughulikia masuala ya aina hii.

Nitawashukuru sana kwa niaba ya vijana wetu, tuenzi elimu yao kwa kuunganisha nguvu zetu hivi. Mnisamehe kwa kuandika mtandaoni. Nimejaribu njia za kawaida za simu sikufanikiwa sana. Hapa ninajua kila moja atapata taarifa. Mapungufu yangu yasizuie jambo hili kutendeka. Jinsi tulivyo changia madawati, sasatuchangie elimu ya juu.

Niombe wizara na Bodi ya mikopo ya wanafunzi kutoa ushirikiano tutakapouhitaji utaalamu muwe nasi bega kwa bega.

Mungu atubariki wote, aibariki Tanzania.

Asanteni tena, ni mimi mama Anna Mghwira
Kuna vitu vingi vya kurekebisha nchi hii ambavyo vinaingiliana. So the best approach ni kuangalia udahili, quality of education, ajira Na source of financing yaani kodi , utendaji kazi ,rushwa etc
 
Hatuwapi tunawakopesha wote wenye sifa, tutafute wanasheria wazuri waandae mkatamba ambao hauna riba, tuanze na hiyo elfu moja kuanzia April mosi. Nb nasikia na wewe ni mwanasheria hivyo tusaidie
Ndio, si kuwapa ni kuwakopesha kwa riba ndogo kwa sababu ya udhaifu wa fedha yetu...Kamati itaamua lakini asiliia 2% inaweza kufidia pengo hili na ili kuufanya uwe endelevu (revolving) kukopesha wengine kwa kipindi chote cha uhai na uhitaji wa huduma hii.
 
Asante. Naomba uwaombe Moderators waiweke hii thread kama "Sticky Thread" kwa vile ni endelevu,na tunahitaji kuchangia pia. Pia mimi,niko tayari kuanza uchangiaji,ila tuone njia nzuri ya kutumia ID zetu humu JF! Wengi siyo verified users na huenda hawatahitaji kuwa exposed publicly. Nina nia njema. Ubarikiwe mama yetu.
Asante nitaongea na uongozi wa JF. Tayari akaunt ipo lakini kuna taratibu chache za kurekebisha, tuanze.
 
Ndio, si kuwapa ni kuwakopesha kwa riba ndogo kwa sababu ya udhaifu wa fedha yetu...Kamati itaamua lakini asiliia 2% inaweza kufidia pengo hili na ili kuufanya uwe endelevu (revolving) kukopesha wengine kwa kipindi chote cha uhai na uhitaji wa huduma hii.
Mother inabidi tufanye harambee iongozwe na PM kwa ajili ya mfuko wetu, mapendekezo mkopo wa shule 5% na wa member wa JF ni 8%, anza kuandika katiba
 
Waooooh, hili wazo bonge la wazo

Maombi tuuu kisiruhusiwe chama chochote na kwa namna yoyote kulitumia hili wazo kama mtaji,

Na asitokee mtu yeyote atakayeruhusu kutumia kwa namna yeyote hili wazo kwa ubaguzi wowote
Press tayari, sasa tunapanga uzinduzi rasmi. Tayri wanafunzi waliokosa mikopo wanajitikeza na kueleza keri zao mbalimbali.
 
Kwanini umeomba radhi kwa kuandika mtandaoni ?

Kingine , Nakuhakikishia mpango wowote wa kuleta neema kwa wanafunzi nje ya mipango ya serikali hii hautakubaliwa na mamlaka kwa sababu ya uoga , lengo kuu la ccm ni kuhakikisha wanafunzi wanakosa mikopo ili waendelee kuwa mbumbumbu , wasije wakapata akili wakaanza kuongoza mapambano ya ukombozi wa nchi yao .

Elimu ni ukombozi wa mtu mmoja mmoja na jamii. sidhani na siamini serikali haitaki watu wapate elimu, lakini changamoto za uratibu zinaweza kutoa matokeo hasi. Sisi tutoe mchangowetu.
 
Nimesoma kwa Umakini mkubwa thread yako kuhusu mikopo ya Elimu ya juu. Sijafurahishwa na motive yako! Utanisamehe! Mwalimu Nyerere,Baba wa Taifa,alikusomesha kipindi pato la Taifa likitegemea Mkonge,Kahawa,Pamba,Paretonk. Kwa uwiano wa pato la Taifa na mahitaji,fedha ilitosheleza usomeshwe bure bila harambee za mama au bibi zetu!
Leo,mapato ya nchi hayategemei sana mazao hayo,bali tuna migodi ya madini,makampuni ya mawasiliano,mikopo,grants,wasomi,uvuvi na mengineyo chungu tele!
Kama mwanasiasa mahiri,na mama,dada yetu,ungeanzia hapo kuhoji kulikoni tumekwamia wapi? Ninaamini una nia njema,ila kabla wake zetu,shangazi zetu hawajaanza kuchangia wazo lako,tueleze au tuelimishe tumekwamia wapi? Ukiwa kama kipepeo kuchagua uwa la kuanzia kurukia kwa sababu tu ya rangi au upepo umekusukumia hapo,jamii haitakuelewa vizuri.
Kididimo, mkwamo wa rasilimali upo ndio maana tunaongea hivi. Kama kujadili kutawapa wanafunzi mikopo kesho kutwa vyuo vikifunguliwa,basi tuanze huomjadala, lakini kama mijadala mingi haijazaa matunda, tuchange wakati tunajadili ili michango ipungue, na kodi ya mali asiliilipie elimu yetu,
 
Vijana wa Lumumba kwenye huu Uzi huwezi kuwaona wanasubiri michango ikishakusanywa utawaona wakipanga utaratibu wa kugawa.majambazi wakubwa CCM
Waterloo,
Tumesema tusiingize siasa, lakini wewe unaingiza siasa kwa mategemeo kuwa wengine hawatafanya hivyo, itawezekana kweli? Kama hatutaki siasa kwenye jambo lolote tusishutumu mtu wala kikundi mbacho hakijaleta siasa. Anayeleta siasa, atajitoa mwenyewe kwenye kundi.
 
Nina wasiwasi na serikali hii kama kweli ina dhamira ya dhati kuinua elimu na kuwasaidia watoto wa masikini.

Nakumbuka kwenye kampeni mjini Tabora mjomba alisema hakuna mtoto atakayekosa mkopo. Sasa sijui kma mjomba anakumbuka.

Kwenye majukwaa wanasema hii ni serikali ya wanyonge na maskini, Lkn kwenye utekelezaji ni tofauti kabisa. Huu umaskini wetu ndo viongozi wanajivunia.

Kampeni ni nia mkuu. Lakini unapofika kazini mambo mengi. Tz maskini sana. Na unaposema utoe mkopo huu. Ujue na mwakani lazima utoe. Rais kazi yake ni kuonyesha dhamiri ya kufanya. Sisi ndo tumsaidie. Hawezi toa hela mfukoni. Nchi ina watu 50,mill na ushee. Embu tumia akili ukioanisha na maisha yako. Angalia kabla hujafikia stage fulani lakini ngoma yenyewe inachangamoto. Unawaza ada. Usiku nyumba inaungua. Unawaza nyumba. Mkwe anafariki. Nk. Nk so kabla ya kuandika pumba tufikirie mana sasa hata mbwa atatuzidi kwa vitu na hoja za kichekechea kisa majina ya kificho.
 
Naam, ndio lengo. Tukifanikiwa kuchangisha kwa miaka 5 mfululizo, tunaweza tusichange tena milele, ilimradi mfuko uendeshwe kwa uadilifu.

Piga kazi mother, hii issue ya wanafunzi kuhusu mikopo tutengeneze kitu ambacho kitakuwa na msaada kwa vizazi na vizazi kupitia hapa hapa JF, itapendeza kama wewe utatuongoza kwenye harambee ya kuchangia wanafunzi wetu. Mother wewe ni public figure
 
Back
Top Bottom