Wamekwisha kujibiwa. Jibu kuu kwa wasio pata no kuwa serikali haina Pesa, kwa aliyepata anamshukuru munguNatamani vijana wa mwaka wa kwanza walio appeal wangejibiwa kabla vyuo kufunguliwa kwenda semista ya pili
Wamekwisha kujibiwa. Jibu kuu kwa wasio pata no kuwa serikali haina Pesa, kwa aliyepata anamshukuru munguNatamani vijana wa mwaka wa kwanza walio appeal wangejibiwa kabla vyuo kufunguliwa kwenda semista ya pili
Habar ya asbh wana jm! Kuhusu hili suala jaman Naona kimya kimekuwa kirefu. Hili muhimu sana kwa kufanikisha ndoto za wengi, tumuunge mkono mama yetu.Ninaikumbuka vema kauli ya mama Salma Kikwete kuwa nanukuu: " Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako." Leo watoto wa wenzetu wameingia tatizo la kukosa mikopo ya elimu ya juu; tuwasaidie kama watoto wetu.
Ninapenda kuwaomba akina mama wote nikianza na Mhe mama Salma Kikwete aliyeasisi usemi na hatua hii, tushirikiane kunusuru maisha ya elimu ya watoto walioko vyuoni wenye sifa ya kuwa na mikopo lakini hawakufanikiwa kupata mkopo. Tuwahamasishe vijana waliobakia mitaani na majumbani kujiunga na vyuo vikuu kuanua akili zao changa kukidhi ushindani wa sasa kimaisha.
Naomba akina mama wote viongozi, wazazi, walezi, wafanya bishara, waajiriwa, wanaharakati bila kujali itikadi zetu za aina yoyote tusimame kama wanawake wazazi wenye nia kuejnga taifa la watu walioelimika tuunde mfuko wa kuwasiadia watoto wetu wafanikiwe kumaliza masomo yao kwa ujenzi wa taifa letu.
Nikitoka na mama Kikwete ninaomba wake za marais wote waliopita kuanzia na mama Karume (mzee marehemu na Rais aliyemaliza mda wake) mpaka mama Janet Magufuli anayenivutia sana kwa kuonesha moyo wa amani sana kwa taifa letu.
Baada ya hao nimuombe mama Anna Makinda na wabunge wanawake wote waliopo na waliomaliza tangu uhuru wa nchi yetu tuungane kumsaidia kila mtoto wa Tanzania mwenye uwezo wa kusoma asome.
Kisha kwa niaba ya wanawake wafanya bishara niombe kitengo cha wanawake cha TCCIA, Baraza la Biashara la wanawake...tukubali wito huu: Tuungane kama wazazi na walezi chini ya kauli mbiu: Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako...tuunde mfuko wa elimu kwa ajili ya vijana wetu.
Niombe vyama vya wana-taaaluma: waalimu, madaktari, wahandisi, watumishi wa umma, mabenki, makampuni yote ya ndani na ya kigeni, asasi za kiraia za ndni na za kimataifa, balozi zetu zote, tuungane kuunda chombo hiki kuwasaidia vijana wetu.
Nimeguswa sana na mahangaiko ya vijana wa vyuo vikuu. Ninawashukuru wachache waliofika kwangu kueleza changamoto zao. Mmenihamasisha kuchangia kidogo elimu yenu lakini ninaomba hili liwe suala la kitaifa.
Ninaomba wanawake wenzangu popote tulipo tuwasiliane tuunde umoja huu kuwaimarisha na kuwapa tumaini vijana na janga la kukosa elimu ya juu kama wana sifa za kuipata.
Tuweke kando siasa, dini, kabila, ukanda ama aina yoyote ya kigezo kufanikisha jambo hili. Ninawashukru sana. Kesho kuna wanafunzi watashindwa kufanya mitihani kwa kukosa ada kidogo tu ya laki kuanzia 5-8. Mfuko wa mama Salma, Mfuko wa mama Mkapa wa Fursa sawa kwa wote, Taasisi ya Benjamini mkapa, Taasisi ya Jakaya Kikwete, Taasisi ya Mwalimu Nyerere, na zingine, tusaidiane kukamilisha azima hii. Na mimi nimeanzisha Taasisi ya Mama Anna Mghwira kwa ajili ya kushughulikia masuala ya aina hii.
Nitawashukuru sana kwa niaba ya vijana wetu, tuenzi elimu yao kwa kuunganisha nguvu zetu hivi. Mnisamehe kwa kuandika mtandaoni. Nimejaribu njia za kawaida za simu sikufanikiwa sana. Hapa ninajua kila moja atapata taarifa. Mapungufu yangu yasizuie jambo hili kutendeka. Jinsi tulivyo changia madawati, sasatuchangie elimu ya juu.
Niombe wizara na Bodi ya mikopo ya wanafunzi kutoa ushirikiano tutakapouhitaji utaalamu muwe nasi bega kwa bega.
Mungu atubariki wote, aibariki Tanzania.
Asanteni tena, ni mimi mama Anna Mghwira
Ninashukuru kwa kulifanyia kazi wazo langu. Post yako imewezeshwa "kuwa sticky thread".Tutaweza kuiaccess kwa wepesi katika kutoa michango yetu. Tutaomba mrejesho wa kila hatua. UbarikiweKididimo, hiyo ndiyo roho ya nia hii...hakuna zaidi wala pungufu.!
Asante sana. Kwa sasa tunaandaa tangazo la kuweka mtandaoni. ninaomba maoni ya wadau lini tuanze kuchangia? tunawasiliana na mitandao ya simu tupate namba maalum za michango.naunga mkono mama yangu.tuendelee kupigania suala hili
Tangazo litasaidia walengwa kuleta majina yao licha ya wale tuliopokea awali. Tukianza kuchangia na kusaidia wanafunzi wachache ndipo tutaweka tarehe ya uzinduzi rasmi.Asante sana. Kwa sasa tunaandaa tangazo la kuweka mtandaoni. ninaomba maoni ya wadau lini tuanze kuchangia? tunawasiliana na mitandao ya simu tupate namba maalum za michango.
Hii ni fursa pekee kwa wanajamii forum kuonesha njia katika jambo hili kisha wengine wafuate. Asanteni sana na Karibuni sana. Nilitingwa kidogo na mukitano ndio sababu nilipotea lakini tupo vijana wanaandaa tangazo kisha mchakato uanze.Tangazo litasaidia walengwa kuleta majina yao licha ya wale tuliopokea awali. Tukianza kuchangia na kusaidia wanafunzi wachache ndipo tutaweka tarehe ya uzinduzi rasmi.
Hongera mama mungu yupo pamoja nasi kwenye hili....Hata mimi nilikuwa kimya kwa lengo la kuweka mikakati sawa, kukutana na wadau mbalimbali na kuona uwezekano wake kila eneo. Watu wengi wanaunga mkono. Tuanze mara tangazo litakapotoka wiki hii.
Kna dogo masoma y kata Tena science yupo udsm.. Conas... Hana hata v0%Mikopo inatolewa kwa watoto waliosoma shule za Kata tu, huo ndiyo msimamo wa Serikali hii na ndiyo kigezo kikuu
Habar ya asbh wana jm! Kuhusu hili suala jaman Naona kimya kimekuwa kirefu. Hili muhimu sana kwa kufanikisha ndoto za wengi, tumuunge mkono mama yetu.
Kna dogo masoma y kata Tena science yupo udsm.. Conas... Hana hata v0%
Maoni ya ziada: Baada ya kupata muda wa vipindi na Luninga za Star, Azam,Ch Ten, mwaoni ya wadau yanaomba tuangalie pia kada la kundi la chini lililo kubwa zaidi na ambalo madhara yake kwa jamii ni makubwa zaidi: Kidato cha 4, 6, na hata darasa la 7 wasio na ujuzi wowote. Wadau / wasikilizaji wa vipindi waliomba tuliangalie hili kwa jicho tofauti. Ni vizuri kuweka rekodi sawa ili tutakapoanza tusisahau jambo hili. AsanteniAsante Kitukuu. Katika kuendelea kupata mkono wa umma nimeendesha vipindi vya luninga azam, chanel ten na star tv. Mwitikio ni mzuri. Ninaomba tangazo likitoka tuanze kutoa si
Ndugu Mkwepa Kodi, naona umekwepa na maneno sasa. Sijui kama wengine wamekuelewa. Mimi nimetoka kapa.
Hata mimi nilikuwa kimya kwa lengo la kuweka mikakati sawa, kukutana na wadau mbalimbali na kuona uwezekano wake kila eneo. Watu wengi wanaunga mkono. Tuanze mara tangazo litakapotoka wiki hii.
Wazo zuri sanaa asante kwa kutoa progress, huu uzi ungekua wa kuikejelii serikali zingekua page 1000plus za replies lakini cha ajabu kitu cha msingi kwa taifa letu watu wanapita tuuMaoni ya ziada: Baada ya kupata muda wa vipindi na Luninga za Star, Azam,Ch Ten, mwaoni ya wadau yanaomba tuangalie pia kada la kundi la chini lililo kubwa zaidi na ambalo madhara yake kwa jamii ni makubwa zaidi: Kidato cha 4, 6, na hata darasa la 7 wasio na ujuzi wowote. Wadau / wasikilizaji wa vipindi waliomba tuliangalie hili kwa jicho tofauti. Ni vizuri kuweka rekodi sawa ili tutakapoanza tusisahau jambo hili. Asanteni