Elections 2010 Anna Kilango kutorudi bungeni...?

MtazamoWangu

JF-Expert Member
Apr 25, 2009
313
7
kweli nguvu ya mafisadi imeonekana jimbo Same mashariki, na ukiona Mama Ana kilango analalamika kiasi kile bungeni basi AMINI ni masikitiko kutoka moyoni kwake....hali yake jimboni ni mbaya sana na hata watu wake wa karibu wamemshauri hali ni ngumu sana, fitina zilizopandwa ndani ya jimbo na pesa zilizomwaga basi zimefanya hata wale wananchi waliokuwa wakimpenda kujenga chuki nae.....
Utafiti uliofanywa unaonyesha Mama Ana kilango huenda asirudi tena bungeni kwani upinzani ni mkubwa ssana, na kutokana na muda muwa mfupi kazi itakuwa kubwa kubadilisha matokeo....
 
Kwani yeye amemilikishwa?Mwambie aache unyerere kwamba same mali yake!
 
hiyoo ni demokrasia, tena wabunge wa sasa (ukiondoa wale wa upinzani) hawastahili kurejeaa bungeni kuendelezaa majunguu na unafikii wao...
 
Wananchi wa Same wasipomchagua(kama ni kweli hajawafanyia chochote)basi wananchi hao hawana haki ya uduma ya uongozi wa mama huyo and vice versa.
 
Jamani kwani Anne kilango alizaliwa awe mbunge!!!! na kama anahujumiwa yeye anashindwa nini kuhujumu hajui hiyo ndio siasa. Ukijengewa jungu na wewe pika lako it is the survival of the jungle. Mie nauliza kwanini asijiwekee mikakati ya kutetea jimbo lake badala ya kutaka sympathy from the public.
 
Aaache uvuvuzela kama Same Mashariki wanamkubali atapeta tu.....ila ajue hakuna mwenye hatimiliki ya jimbo ?
 
Wanajamii, kama kuna mtu anamfahamu Anne Kilango au watu wake wa karibu, basi wamshauri asome (kama hajawahi kusoma) the damned book "Lo Prince" by Machiavelli ili ajuwe siri ya politik! That book gave the politcian an advice about what he/she should do to persevere and to promote in his/her position badala ya kulialia. Alitakiwa kujua by now kwamba politiks is a dirty game. There is no definite rules. Siasa ni kama ile PRO-WRESTLING ya zamani (late 80s); you can use everything near you: kick, punch, slap, na ukiweza ua kabisa.
Laiti kama hayawezi haya, basi jibu lake ni rahisi; leave the dirty game to the dirty players and stop crying!:A S 20:
 
Wakuu mmenena, si kawaida kwa siasa za ushindani kuendeshwa bila mikakati yenye hujuma. Mzigo ni kwa mshindani kuwa macho. Penye jinai basi achukue hatua stahili. Penye ujanja naye ajitahidi kuzidisha kete. Hulka ya wananchi wenzetu kununulika kwa vijisenti imejengeka sana nchini jambo ambalo kwa namna moja au nyingine limepewa promosheni nzito kinyemela na chama chake. Pengine hiki ndio kitakuwa kichocheo cha kurekebisha uozo humo ndani ya chama.
 
Wanajamii, kama kuna mtu anamfahamu Anne Kilango au watu wake wa karibu, basi wamshauri asome (kama hajawahi kusoma) the damned book "Lo Prince" by Machiavelli ili ajuwe siri ya politik! That book gave the politcian an advice about what he/she should do to persevere and to promote in his/her position badala ya kulialia. Alitakiwa kujua by now kwamba politiks is a dirty game. There is no definite rules. Siasa ni kama ile PRO-WRESTLING ya zamani (late 80s); you can use everything near you: kick, punch, slap, na ukiweza ua kabisa.
Laiti kama hayawezi haya, basi jibu lake ni rahisi; leave the dirty game to the dirty players and stop crying!:A S 20:

Kizazi kilichokwisha kata tamaa... kizazi kinachohalalisha ufirauni uwe ushujaa... kizazi kilichojaa ubinafsi.... kizazi kilichopotoka...... nani wa kukinusuru? Inashangaza watu tumefikia hatua ya kufurahia mbunge anapochoguliwa kitapeli na wale wanaotaka fair play tunawaona sio wajanja.... Afrika tuna kazi
 
Wananchi wa Same wasipomchagua(kama ni kweli hajawafanyia chochote)basi wananchi hao hawana haki ya uduma ya uongozi wa mama huyo and vice versa.

Mkuu Mafisadi bado wameshika hatamu ndani ya CCM na Serikalini hivyo watafanya kila wawezalo na kwa kutumia mabilioni yao ya kifisadi kupambana na wabaya wao na kuhakikisha hawarudi tena Bungeni baada ya uchaguzi. Bongo bila ufisadi inawezekana, mimi nakataa kauli hii umefisadi umeota mizizi kila pembe na vigumu mno kuushinda.
 
shida ni kuongozana na Simba huku una harufu ya Swala,
ni jambo gumu sana kuwa mbuzi katikati ya kundi la Chui
 
Mkuu Mafisadi bado wameshika hatamu ndani ya CCM na Serikalini hivyo watafanya kila wawezalo na kwa kutumia mabilioni yao ya kifisadi kupambana na wabaya wao na kuhakikisha hawarudi tena Bungeni baada ya uchaguzi. Bongo bila ufisadi inawezekana, mimi nakataa kauli hii umefisadi umeota mizizi kila pembe na vigumu mno kuushinda.
Bubu;Tuko all the way pamoja....Isipokuwa tuliwaambia toka nyakati zile especially mama alipodai "Hapatakalika" "Patachimbika" nk...Tulisema ondokeni humo nyie mnaojiita wapiganaji,naona bado wanabisha,sasa kama hoja zao dhidi ya ufisadi ni kwenda kinyume na matakwa ya chama watamlaumu nani zaidi yao wenyewe?Tunasikia ccj hivi wapiganaji vile lakini hakuna action.

Ok lets say wananchi hawajui umuhimu wa ufisadi nk,unataka kusema hakuna alilowafanyia kabisa hao wakazi wa same?Ndiyo maana nikasema kama kuna alichowafanyia,halafu na wao bado hawamtaki,then hawana haki ya kupata huduma ya uongozi bora wa mama huyo....Na adhabu yao itaendelea kuwa kubakia kwenye umasikini.

Hizi ni issue ambazo walitakiwa wazifikirie long time ago na wajipange,inavyoonekana hawana long term strategies...yeye pamoja na wapiganaji wengine,unless upiganaji wao ni kujipanga tu kwa maslahi yao binafsi ndani ya ccm na si wananchi.
 
Siku zote "wapambanaji" wamekuwa wakidai kwamba JK yuko upande wao, sasa kwenye hizi nominations ndiyo watajua rangi halisi ya JK. It is too late kwa kuwa watachezewa rafu na bado hakuna kitakachofanyika.

Mkuu JMUSHI1 ninakubaliana na wewe, hawa watu walikuwa wakijidanganya kwamba JK yuko upande wao, juzi nimesikia wanaomba kuonana na JK. Hata kama wataonana nae sidhani kama atawasaidia kwa kuwa JK ni uzao wa UFISADI, hawezi kucheza mbali na mafisadi wenzake.

Wameishalalamika kwa Makamba, haikusaidia. Wakahamia kwa Mkuchika akawa kimya, sasa wamehamia kwa Waziri Mkuu na kutishia kwamba damu itamwagika. Nani wa kumwaga damu? Hawa watanzania ninaowafahamu? Mbona CCM wakicheza rafu mbaya sana huwa hatusikii vitisho vya kumwaga damu?

Wapiganaji wajilaumu wenyewe, kama kweli walikuwa serious na vita ya ufisadi wangejitenga na JK na kumuwekea ngumu. Kama CCM ingewafukuza uanachama, ndio wangekuwa wamepata kete nzuri ya kurudi mjengoni maana wangekuwa wamedhihirisha kwamba ni wapambanaji wa kweli. Sasa hivi ni ngumu sana kuwaelewa.
 
wanalia nini sasa maana walikuwa na mtaji wa kuwamaliza kabisa hao mafisi ufisadi???? leo hii wangekua wanahangika na kesi zao mahakamani katu hawangekua na muda wa kusumbua majimbona. nawauliza nani aliwatuma kuondoa rich mondulu mjengoni???? wasilie na wawe wapole walipaswa kujua hilo mapema. walitegwa wakaingia king kiulaiiiiiini
 
Enzi zile wapinzani walipokuwa wakilalamika rafu za majimboni CCM walikuwa wakichekelea waliona kama ngonjera za Mjomba sasa inakula kwao wanagombana wanyewe kwa wenyewe na bado tutaona mengi wakati wa kura za maoni.

Ushauri kwa mama Anne Kilango, kama anaona mtumbwi unazama anachotakiwa ni kutoka ndani yake lakini kama ataamua kuendelea kukaa basi na avumilie mawimbi asitupigie kelele ajitahidi kuchota maji ayamwage nje hadi mawimbi yatakapotulia.
 
Kwani huyu mama ni lazima agombee kupitia ccm????
Kama kweli anakubalika kwa wapiga kura wake na anaona anazongwa na mafisadi ndani ya ccm kwa nini asihamie vyama vingine ambavyo havina mnuko wa ufisadi??????? Au alikuwa amezoea tamu ya asali na ikamlewesha kiasi kujisahau anastuka alfajiri na kugundua kuwa wenzake tayari wako juu ya mti wakiwa kwenye harakati za kurina naye kwa kujihami anapiga makelele ya mwizi akitarajia wasamaria watajitokeza kumsaidia???????????????
A LUTA CONTINUA DEMOKRASIA
 
kweli nguvu ya mafisadi imeonekana jimbo Same mashariki, na ukiona Mama Ana kilango analalamika kiasi kile bungeni basi AMINI ni masikitiko kutoka moyoni kwake....hali yake jimboni ni mbaya sana na hata watu wake wa karibu wamemshauri hali ni ngumu sana, fitina zilizopandwa ndani ya jimbo na pesa zilizomwaga basi zimefanya hata wale wananchi waliokuwa wakimpenda kujenga chuki nae.....
Utafiti uliofanywa unaonyesha Mama Ana kilango huenda asirudi tena bungeni kwani upinzani ni mkubwa ssana, na kutokana na muda muwa mfupi kazi itakuwa kubwa kubadilisha matokeo....
Hivi kwa nini baadhi ya wana JF wanajifanya wanademokrasia lakini hapo hapo itokeapo mgombea pendwa anapata mpinzani tayari huyo mpinzani atahusishwa na ufisadi??? acheni kudharau wapiga kura kwani wao ndiyo wanaejuwa nani anafaa katika mazingira yao [It up to the voters to decide] Kabla ya mama huyu kulikuwa na mbunge mbona alivyobwagwa hakupiga kelele kama hizo?????
Mimi sitoki jimbo la huyu mama hivyo basi pengine humu ndani mtuelimishe [kwa wanaotoka jimboni ] hali ikoje huko???? kwa nini mama analialia na kupakaza mara damu itamwagika mara mafisadi hivi kunani huko??????
 
Abunuwasi,

ni kawaida ya anna kilango kutoa matamshi ya vitisho, kwa wanaomfahamu wala hawashangazwi na kauli za hivi karibuni. kama anna kilango ametishiwa kuuwawa kama anavyodai, kwanini haendi kushtaki polisi, badala yake anakwenda kushitaki kwa yussufu makamba? anna kilango alitumia mbinu chafu katika uchaguzi wa 2005, kwa kuanza kampeni za ubunge tangu mwaka 2000, na pia kumwaga fedha wakati wa kura za maoni za maoni na uchaguzi mkuu.

kinachomtatiza anna kilango sasa hivi ni rekodi yake kama mbunge wa same mashariki. anna kilango ameshindwa kufuatilia ahadi ya raisi ya kujengwa kwa kiwango cha lami barabara ya mkomazi-ndungu-same. jimbo la same mashariki, na wilaya ya same, imeendelea kushika mkia mkoani kilimanjaro katika mitihani ya kitaifa na juhudi za mbunge katika suala la elimu hazionekani. kuna ufisadi wa kutisha katika uvunaji holela wa miti, na uharibifu wa vyanzo vya maji ktk jimbo la same mashariki, lakini mbunge haonyeshi kukerwa na ufisadi huo.

kazi aliyoifanya anna kilango ni ndogo na hairidhishi. ukweli huo ndiyo unaosababisha akabiliwe na upinzani jimboni kwake.tayari amejitokeza naghenjwa kaboyoka "mama maendeleo" na dr.michael kadeghe kumpinga katika kura za maoni za ccm.

soma jinsi hali ilivyokuwa tete mwaka 2005 baada ya anna kilango kumfanyia mchezo mchafu naghenjwa kaboyoka. wananchi walikuwa wanapeperusha bendera za ccm nusu mlingoti!!

Wanaomhujumu mgombea ubunge wa CCM Same waonywa

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya same, Bw. August Kessy amesema kuanzia sasa viongozi wa ngazi zote wanaomhujumu mgombea Ubunge wa Jimbo la same Mashariki kupitia Chama hicho, Bi. Anne Kilango, wataondolewa.

Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Shule ya Msingi Kambene Kata ya Miamba Bw. Kessy alisema kuna viongozi ambao wamekuwa mwiba mkali kwa kampeni hizo, kutokana na kuchochea uasi.

Bw. Kessy alisema kutokana na hali ya kampeni kudorora katika Kata nyingi, ameamua kupeleka taarifa mkoani, kuelezea tatizo hilo.

’’Nimeshapeleka taarifa mkoani wameniruhusu kumuondoa kiongozi yoyote, ambaye ataleta vurugu na mgawanyiko wa kichama wakati wa kampeni, hata kama kiogozi huyo anaondolewa na vikao kwa mujibu wa katiba, lakini mimi nitamuondoa kwa muda hadi kampeni zimalizike, ndipo vikao vikae, sasa hivi hatuna muda,’’alisema Mwenyekiti huyo.

Alisisitiza kwamba viongozi hao, ni wale ambao hawakufarahishwa na mgombea ubunge aliyeteuliwa na CCM.

Alisema viongozi hao pamoja na wananchi, wamekuwa wakisusia mikutano ya kampeni ya mgombea huyo wa CCM.


’’Jamani kura za maoni sasa hivi ni historia, lakini kwa Jimbo la Same Mashariki, bado kura za maoni ni tatizo. Matokeo yake yamesababisha kudorora kampeni zetu bila sababu za msingi,”alisema Bw. Kessy.

Mwenyekiti huyo, alitoa karipio hilo, baada ya kupita kwa maandamano na kukuta bendera za CCM zinapeperushwa nusu mlingoni, kama ishara ya maombolezo.

Alisema kwa vyovyote hatua hiyo, ina mkono wa viongozi, jambo ambalo lilipingwa vikali kwa kiapo na Mweneykiti wa Kata hiyo Bw. Pagu Mkulu.

Tangu kuanza kwa kampeni za mgombea huyo, wananchi wamekuwa wakisusia mikutano yake, kuzomea na kurusha mawe kwa sababu zinazoelezwa kwamba chanzo chake ni kura za maoni, ambapo mgombea anayekubalika na wananchi wengi Bi. Naggy Kaboyoka alitemwa.

Hata hivyo, Bw. Kessy alisema hata kama wananchi hawampendi Bi. Kilango ni vema wakaja kumsikiliza, badala ya kususia mikutano yake.

’’Pale Mjema na Bombo Kata nzima walikuja watu saba kwenye mkutano, hapa kuna tatizo, pia kuna kukosa uungwana kwa viongozi na wanachama wa CCM,’’alisema.
 
Back
Top Bottom