Mimi sikubaliani na hoja hii.
Kanisani ni sehemu mwafaka kwa mkristo kuongea na Mungu. Kuongea na Mungu ni pamoja na kuabudu, kusali, kutukuza, kusifu, kuomba n.k. Kama mke mwema anatoka kwa Mungu, inabidi mkristo aongee na Mungu ili Mungu ampe huyo mke mwema. Moja ya njia ya kuongea na Mungu ni kuomba. Hivyo mkristo anayehitaji mke humwomba Mungu. Kwa hiyo kanisani ni sehemu maalumu iliyokubalika kufanya maombi ingawaje mkristo anaweza kufanya maombi yake nje/mbali na kanisa.
Hakuna haja ya kuwa na shaka maadamu mke mweka hutoka kwa Mungu hakuna sababu ya kuhofu kupata kitu kibaya kutoka kwake. Kwa kuwa kanisani kuna wabaya na wema kwa jinsi ilivyo hakana haja ya kuhofu kuwa mwombaji atapata 'watembeza ngoma', 'wanaopigana mijeledi', vijana wazinzi, 'wapigaji mizinga', matapeli wa kupindukia n.k.
Lakini pia ni vizuri kujihoji. Je, kama mimi ninataka/ninapenda mke mwema, mimi ni mwema? Ni vizuri huyo mke mwema ninayemuomba nimtayarishie mazingira ya wema. Inawezekana sipato mke mwema kwa sababu mimi si mwema.