Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

Status
Not open for further replies.
Well said, well spoken mkuu, umetusaidia sana kushusha hasira tulizonazo kutokana na huu uchaguzi. Maisha yaendelee.
 
exactly mkuu, ur right, mm nauchunguuuuuuuuuu sana na hawa CCM wameiba our votes, this is a huge vote rigging ever, Watu mil 19.6 wamejiandikisha , eti watu mil 8 tu ndi wamepiga kura, kisha JK kawin 5 mil, mm i strongly reject the results, i am sayin loud and clear, RAIS WANGU DR SLAAAAAAAAAAAAAA u can not take away that from me, juzi,jana, leo, kesho na hata milele
 
Mh.mwanakijiji,asante. Ila kumbuka icho kilikuwa kipindi cha kampeni. Nakuhakikishia kuwa baada ya kuapishwa watawala pamoja na rais mteule ataheshiwa kwa asilimia mia! JF inakubari ushauri huo,mkuu akishauri ni amri,sio tena ombi! Tunashukuru!
 
Mzee Mwanakijiji mi nimekuelewa sana, lakini nasikitika kuwa sijaunga mkono hoja yako.

Mzee, upole wetu siku zote ndo umekuwa ukituponza na ndio maana utawala wa hawa mafisadi unatuonea, bila nguvu ya ziada mzee mi nafikiri tutakuwa tunacheza tu. MFANO, kwenye uchaguzi wa mwaka huu hasira na jazba za watu ndo zimepelekea upinzani kupata matokeo haya waliyoyapata, kumbuka uma ulikesha, uma ulipiga kelele uma ulichoma nyumba na magari kushinikiza waliyemchagua apite.

Vinginevyo tungedhurumiwa sana mwaka huu, hivyo basi mi naamini njia hii ni njia sahii kudai haki, yaani leo watu tuamue tu kikwete hatumtaki twendeni maandamanoni, tulale barabarani wafanyakazi wasiende kazini na wanafunzi wagome kusoma hapo jamaa atatoka hata kama hataki ila tukijifanya wastaraabu rasirimali zetu tunazopigania kwa manufaa yetu zitaliwa zote huku sisi tukibaki kwenye lindi la umaskini. ni hayo tu
 
heshima zako mwanakijiji!ilikua too much ubarikiwe na mawazo yako mazuri maana hata kama tuna tofauti za kisiasa bado tunaendelea kuwa watanzania
 
Mwanakijiji pamoja na kwamba wazo lako linaweza kuwa zuri naomba nitofautiane nawe kidogo. Wengine tuliwahi kusema kuwa ni rahisi ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko kuiondoa CCM madarakani kwa njia ya kura. Kama kuna wakati hili lingewezekana ni katika huu uchaguzi unaomalizika kwani Watanzania walikuwa na sababu, nia na uwezo wa kuipumzisha CCM. Hata hivyo CCM kwa kutambua hilo kwa muda mfupi wameweza kuizima hiyo ndoto ya Watanzania kwa kutumia njia mbali mbali nyingi zikiwa si za halali.

Kwanza katiba tuliyo nayo sasa inakilinda chama kilicho madarakani na haitoi uwanja sawa kwa siasa ya ushindani na kama haitaandikwa upya, hoja yako Mwanakijiji inakosa nguvu kabisa. Swali kubwa la kujiuliza ni je, katika hii miaka mitano kuna dalili yoyote ya kupata katiba mpya chini ya serikali ya CCM. Naamini ni hofu ya katiba mpya iliyoilazimisha CCM kutumia nguvu na udanganyifu mkubwa kwenye huu uchaguzi - kuhakikisha wanaendelea kupata mteremko kwenye chaguzi zitakazofuatia.

Nina hakika kuwa mwaka 2015, CCM itakuwa na kila sababu ya kuhakikisha inabaki madarakani kwani sababu za kujihami zitakuwa zimeongezeka. Kwanza Kikwete kama alivyofanya Mkapa atahakikisha anapatikana mrithi atakayeweza kumlinda kama yeye alivyomlinda Mkapa. Pili tofauti na mwaka huu baada ya CCM kushuhudia upepo wa mabadiliko unavyohatarisha usalama wao, wana miaka mitano ya kupambana na wanawaona wakorofi kwa kujaribu kuwaziba mdomo.

Hivi karibuni tu tumeshuhudia mbinu mpya kabisa ya kuwatumia wanajeshi wetu na Usalama wa Taifa kwa kuwatisha wananchi wasijaribu kudai haki zao na kutoa onyo kuwa havitasita kupambana na wananchi. Hivi sasa ni vigumu kutofautisha kati ya msemaji wa serikali na msemaji wa CCM kwani ukiikosoa serikali si ajabu akakujibu Tambwe Hiza, abdulrahman Kinana au Makamba na ukiikosoa CCM si ajabu akajibu Tendwa, Saidi Mwema au Jackie Zoka.

Hapana Mwanakiji kwenye huu uchaguzi, CCM imedhihirisha kuwa itatumia kila hila kubaki madarakani kwani CCM bila dola haiwezei kudumu hata kwa dakika. Mwaka 2015 watakuwa wanatimiza miaka 54 ukiongezea na za Tanu lakini taifa bado litakuwa halijaweza hata kutambaa kama kichanga kilichozaliwa juzi juzi. Kuking'oa hiki kisiki kunahitaji zaidi ya lugha laini na mwalimu mzuri ni historia - Mwai Kibaki na Robert Mugabe ni mifano ya karibuni ya kutafakari.
 
Nakuunga mkono 100%. Wabongo wengi waoga. Wakati umefika, "enough is enough". Nchi zilizofika zilipo hazikufanya hivyo kwa mwendo huu wa kibongo wa kumchekea nyani. Najiuliza hao watu 5m ni akina nani?
 
Moto uliokuwepo JF wakati wa kampeni ulikuwa unapendwa na wanaopenda mabadiliko. Kauli za MMJ za sasa zinapendwa na CCM. Binafsi sipendi kuona nci ikiingia katika machafuko. Hata hivyo sijasahau harakati za akina Mkwawa, Mzee Karume, Akina Dedan Kimathi etc. Misimamo ya akina Mzee Mwanakijiji haisaidii chochote kwa kuwa inatugeuza sisi mazezeta kiasi kwamba tunakuwa na haki moja ya kupiga kura halafu hatuna haki ya kudai haki ya matokeo halali. MMJ anategemea tutapewa haki yetu na akina Chenge kwa kujadiliana nao.

Niulize tu simply, hivi kuna haja gani ya kupiga kura ikiwa matokeo yanachakachuliwa halafu busara inakuwa "Kuacha tu."? This is nonsence. Heshima iliyopo Zanzibar si matokeo ya "Acha tu" bali pressure (Physical) ya CUF. Amani iliyopo Kenya, Zimbabwe etc ni matokeo ya physical Pressure. South Africa etc etc.

CCM inajua wazi, wakati wa kampeni tumia magazeti kuchafua watu halafu baada ya uchaguzi yatumie "Kuponya vidonda" vya uchaguzi. Mi ni msomi na niko tayari kutukanwa kuwa sijaelimika kwa kutoona logic ya kupiga kura ambazo masharti ya ke ni kukubaliana na matokeo yoyote hata kama nimeibiwa.

Ukipiga kura halafu ukawa tayari kupokea matokeo hata yaliyoibiwa maana yake ulienda kuloanisha kidole katika wino wa kura tu, basi.
 
Nakubaliana na hoja yako MMKJJ.

Hata hivyo siwezi kuacha kutoa maoni yangu ambayo yana sura yangu. Kutumia nguvu kudai haki ni lazima na ni jambo muhimu, nguvu za kiwango gani hilo ndilo swali la msingi.

Kulinda kura yako maana yake nini? Kulinda au kuto cheza mbali na kituo cha kupigia kuara baada ya kupiga kura maana yake nini?
Kumsimamisha mtu tunaye mtuhumu na kumfikisha kituo cha Usalama maana yake nini?
jamaa akitutole panga? bastola au hata wembe je?

Tunatumia nguvu kwa kiwango fulani katika kudai haki zetu kwa sababu ni muhimu kufanya hivyo. Kwa sababu kama sisi tungekuwa ni watu wa maneno tu tunapiga kura na kurudi nyumbani kulala kwa sababu hatutaki shari. Mgombea wetu Dr slaa angeibiwa kura zote ikiwa ni pamoja na aliyoipiga mwenyewe. Nashukuru kwamba watu walitumia nguvu kuhakikisha kwamba kura nyingi haziibiwi na CCM.

Kitendo cha kuendelea kuwa macho na hata kufikia hatua ya kumsimamisha mtu na kumpekua au kumweka chini ya ulinzi hadi wana usalama wafike ni kitendo cha kutumia nguvu. Mtu hawezi kuwekwa chini ya ulinzi na kundi au mtu asiyetumia nguvu au kwa kumpiga jicho na kumpa karipio. KAA CHINI MPAKA RIPORISI RIJE UMESIKIA?

Au kwa kumkuda kwa kabali ya mwana koma mpaka alegee na kusalimu amri.

Je ni nguvu za kuua mtu? Hapana.

Je mtu anaweza kufa chini ya ulinzi wetu Raia kabla wana usalama hawajafika? Ndiyo?

Kama tunadai haki yetu kisha tunalimit kutumia nguvu sidhani kama tutafika. Tunadai haki iliyopokwa na watu wasioogopa Sheria na Taratibu, watu washenzi Babarian. Tunapambana na mijitu ianayovunja sheria kwa kutumia nafasi zao katika serikali. Ni mijitu mioga kabisa lakini vyeo vyao serikali vinapiga pazio uoga wao.

Napunguza jazba.Watu hawa wasiojari taratibu ni lazima wajue "We mean Business and not other wise". Ni lazima wajue sasa tumechora mipaka wasiyotakiwa kuvuka na wakivuka ni songombingo tu.

Jazba tena. Hii mijitu ikiwa kwenye kikao na mashati yao ya kijani bila kaptula inadai kwamba sisi ni makondoo fulani.
Good point. Kondoo wana pembe, wana pembe by design for areason, mara kadhaa katika maisha yao pamoja na ukondoo wao hulazimika kuzitumia pembe.

Kwa hiyo wanatuita Mikondoo sasa tutawapa pembe meno na kwato.

Wote tunapambana hapa kudai haki. Idadi yetu ni naamini ni zaidi ya millioni 7. Sidhani kundi la watu millioni 7 linaweza kukubaliana kupambana bila kutumia nguvu.

Wale wapambanao rasmi kupitia katika safu za vyama vyao watafuata utaratibu wa vyamam vyao. Wengine wataunda vikundi vyao kupigana wakitoa misituni na mijini. Wengine wataunda vikundi vyao ndani ya himaya ya CCM UWT na NEC yenyewe na kupambana kutoka ndanimo ya vyombo hivyo kwa mtindo wa" Which is eating you is within your body". Wengine tutabeba box kwa sana na kutoa sehemu ya kipato cha kubeba Box kusaidia juhudi hizi.

Watu wapiganao kutoka ndani ya vyombo vya serikali ni watu wanao Risk maisha yao. Kwa naman nyingine ni watu walio tayari kufa. Fikiria kwamba mtu anatoa siri kutoka ndani kabisa ya moyo wa Usalama wa taifa. It the same as counting yourself dead. Kwani wakikujua wanakudunga Risasi kisha wanasema majambani wamekuua baada ya kukupoka fedha yako.

Kama watu wanarisk kiasi hicho sioni haja ya kuweka zuio la kutumia nguvu kwa wale wanaojisikia kufanya hivyo. Tunapambana na adui asiyejua kanuni.

Kuna watu hapa tunaandika maneno mazito sana juu ya Mahabithi wa CCM, tunafanya hivyo kutoa jazba zetu mtandaoni kwa sababu tukizitolea mitaani kwa semina za siri, Green guard itakuwa sawa na mtoto atambaaye. Kuna mambo mengi tunayajua kwa taaluma zetu na ufahamu wetu hata hivyo tunaona ni vema kumwaga hisia hapa mtandaooni ili zipozwe na wana JF.

Ieleweke wazi.Hatujaanza kutoa jzba hizi hapa JF eti kwa sababu shujaa wetu asiye ogopa mtu yeyote Dr Slaa kaibiwa kura tulizo mpa. La hasha. Angalia historia ya maoni yetu miaka 2 iliyopita, tulikuwa na Jazba ya kumtwanga mtu Risasi kwa maudhi mengi kutoka kila Sekta. Tuliwashutumu na kuwakazia macho UWT. Mimi binafsi nilisha wanyea UWT siku nyingi hata kabla Dr Slaa hajasema wamehusika moja kwa moja kuiba kura. Niliwaita vivuli wategemeao mwanga wa kuishi pia wanatumiwa kama ya ndani. Maneno hayo siwezi kuyafuta kwani ni ukweli mtupu.

Matamshi ya namna hii kwa vyombo vya serikali si matamshi yapokelewayo kwa mikono miwili. Ni matamshi yanayowapa hasira na kuwajaza kisasi.maneno kama haya si maneno ya Nguvu ya hoja ni maneno ya Hoja ya nguvu yenye lengo la kuwachokoza ili waweke ushenzi wao hadharani.

Watu waandike hisia zao zote hapa. Pia watu wenye kushauri namna nyingine nao walete ushauri wao hapa. Mwafaka wa nini kila mtu afanye utapatikana hapahapa kwa kuchanganya mawazo yote yale yenye Nguvu ya hoja na yale yenye Hoja ya Nguvu.

Sijutii hata neno moja nililolisema kwa mcheche wangu wa kupokwa HAKI na Maharamia na wazandiki wa KiCCM.

THE LEGEND HAS JUST BORN
 
Haya maneno si yako Mwaanakiji

Kwa kufanya hivyo, tunaweka mtandao wetu tuupendao hatarini kwani kikiwa ni chombo kilichoandikishwa na licha ya watu kutumia majina mbadala endapo jambo fulani linatokea mtandao huu una wajibu wa kushirikiana na vyombo vya kiusalama kutekeleza amri halali ya mahakama kuweza kuwapata wahusika. Sasa tusichukulie kimzaha tunapotoa kauli zenye mfanano wa vitisho, kauli hizo hazilindwi na "uhuru wa maoni" kwani ni kama ilivyosema "kupiga kelele moto, kwenye ukumbi uliojaa".

Haya ni maneno ya kutisha watu yenye harufu ya CCM. Hapa umeamua kuwatia jambajamba watu bila sababu yeyote. Unatja Mahakama , kusaidia polisi. Hii ndo lugha ya kila siku kule ushwazi kwetu wakikubambika msokoto wa bangi.

Internet siyo siri na haijawahi kuwa siri. Hilo linajulikana wazi. Kama wanatataka kufunga mtandao eti kwa sababu sisi tunawatishia maisha yao wafunge tu.

Mtu akifa kwa kudundwa risasi kisha wakakimbilia kuishitaki JF huo utakuwa ni uamuzi wao. Kwani hata sasa wanaweza kuishitaki kwa uchochezi wakitaka. Kwa nini hawafanyi hivyo kwa sababu wana Guilty conscious.

Kama wana taka kujua sisi ni akina nani hiyo siyo taabu ni rahisi kama kuweka maji katani. Hawana haja ya kusubiri jambo litokee waanze sasa hivi.

Hakukuwa na haja ya kutaja Mahakama au vyombo vya kiusalama. Hivyo vyombo vya kiusalama ndivyo vitunyimvyo haki kwa ushirika mchafu na wanasiasa wa CCM.

Kwanza kuna mtu mwenye hamu ya kwenda Mahakamani kutoka CCM, UWT au NEC?
 
Nilishawahi kusema humu ndani kwamba great thinkers ni wachache sana humu ndani. na sikuficha hisia zangu kuwa MZEE MWANAKIJIJI ni mmoja wao. Mwanakijiji, hili swala uliloliongelea ni zito,kubwa na lina ukweli uliopitiliza. ukweli ambao unaweza usiingie akilini kwa baadhi ya wana JF. humu kuna watu ambao hawauoni ukweli,wakiuona hawataki kuukubali na wakiukubali wanaupindisha kwa makusudi.

Swala la kuiweka hatarini JF pamoja na MOD nililiona muda mrefu sana, binafsi nililiongelea kwa mtazamo wangu MOD akanisimamisha


uanachama na mwisho nikaamua kuachana na hii forum mpaka hivi punde nimejiunga upya.

Mwenye akili timamu atakuwa amekuelewa kwani article yako imejitosheleza sana na imekuja katika kipindi ambacho tunaelekea kuapishwa kwa raisi.Sina haja ya kusema ila nliwahi kusikia hivi karibuni kuwa MOD wa hii forum bwana MELLO ni miongoni mwa watu watakaoishi kwa shida sana katika kipindi cha miaka mitano ijayo. na hii ni kutokana na kuruhusu matusi, kejeli na uchochezi katika JF wakati akiwa MOD.

Nakuunga mkono kaka, bado tunaihitaji sana hii FORUM na hakika bila watu kujirekebisha kutumia jazba na matusi dhidi ya mamlaka zilizoshika mpini, ni wazi makali tuliyoshika katika huu mvutano yatatukata na kutuacha na majeraha.
Mkuu ulisema lini wakati umejiunga juzi?na una post 7!wote wageni naona!lol
MMJ umesema kweli,tuilinde JF isije ikawa kama ule mtandao flani uliofungiwa!
 
Heshima mbele...naungana na hoja yako MMJ kwani hoja za nguvu hazina nafasi katika nchi yetu. Tukianza pandikiza chuki za kutumia nguvu tutaifikisha jamii pabaya na wananchi wakawaida ndio tutakaoumia. Nadhani ni wakati wa upinzani kujiimalisha na kwenda kusimamia sera zao bungeni na kisha uchaguzi unaofuata wananchi wanaweza kuwapa ridhaa ya kuchukua nafasi ya uraisi. Kweli asiyekubali kushindwa si mshindani.
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki Afrika
 
Nadhani watu wengine wamenielewa vibaya kwamba namaanisha "tukubali yapite". La hasha! Ninachosema ni kuwa katika nchi ya kidemokrasia ni lazima tutumie mbinu za kidemokrasia kuwalazimisha watawala wetu watusikilize: Baadhi ya mbinu ambazo zina uwezo mkubwa sana ni pamoja na:

a. Maandamano
b. Kuwajulisha watu udhalimu/uovu uliotokea
c. Kukaa na kupinga (sit ins)
d. Mikutano mikubwa ya kupinga (Protest Rallies)
e. Kugoma kutoka mahali n.k

Hizi ni mbinu zinazotumiwa. Kwa mfano, wale vijana walioamua kukesha kulinda kura walipoona hawasikilizwi kwanini waliamua (wengine) kuanza kurusha mawe, kuchomo matairi na hata kuchoma majengo? Kwanini wasingeamua kujipanga na kuzunguka jengo au kukaa mlangoni kuwagombea kuwa hakuna mtu anaingia au kutoka hadi matokeo yatolewe?

Kwa mfano, binafsi nitaunga mkono kabisa kama Dr. Slaa na viongozi wenzake wakisema wanafanya rally au maandamano ya kuipinga Tume ya Uchaguzi na kutaka Jaji Makame ajiuzulu na iundwe tume mpya kusimamia chaguzi ndogo zijazo. Hizi ni njia za kidemokrasia. Lakini, ati tusimame na kuunga mkono mtu anataka kuwa sniper amtungue Mwenyekiti wa Tume kwa jina la "kutaka mabadiliko" mimi siko na kwa kweli mtu huyo naamini hana nafasi katika jukwaa kama hili.

Jamani, kinyume na wengine mnavyosema mmeumia mimi naamini tumefanya vizuri zaidi kuliko inavyofkirika. We have used the power of the ballot box to force change! We should not forget that.. jamani hata tukiassume kuwa wamejitahidi kweli kuchakachua wameshindwa kufikia ahadi yao ya asilimi 80-89!! Hata asilimia 62 kwa urais hawakupata, na kwa ubunge hawakupata asilimia 80!! Sasa, labda watu hawaoni hili lakini ujumbe ni kuwa tukiwa na mgombea mzuri, ujumbe mzuri (kama wa mwaka huu) na tukajipanga vizuri (kwa kweli natamani kufanya ukosoaji hapa lakini najizuia kwa wakati huu) nina uhakika tungeweza kufanya makubwa zaidi.

Naomba mrejee ule waraka wa "Chadema kutoka Hapa mpaka Kule".. mtaona kuwa uchaguzi huu ulikuwa ni wa Chadema kupoteza siyo CCM kupoteza. Kwa hiyo tusidharau nguvu ya njia za kidemokrasia kuleta mabadiliko!!!
 
Mwanakijiji una hopes za ajabu sana wakati mwingine hadu huwa nadhania hauishi kwenye dunia tuishiyo wengi.....(simaanishi kiubaya hata kidogo...ni kwamba nashangazwa na matumaini uliyonanyo)
 
Mwanakijiji una hopes za ajabu sana wakati mwingine hadu huwa nadhania hauishi kwenye dunia tuishiyo wengi.....(simaanishi kiubaya hata kidogo...ni kwamba nashangazwa na matumaini uliyonanyo)

hahahah I am a perpetual optimist..!
 
Maneno kama haya ndio haswa mafisadi wote wanapenda kuyasikia mara baada ya kufanikisha walilopanga. Ni maneno ya kuwatuliza Watanzania ili wao waendelee kula kwa raha mustarehe bila bugudha for another 5 years. Tujiulize wakati wa kampeni na kutoa matokeo ya kura ni kina nani waliozungumzia udini, kutoa kashfa kwa CHADEMA na Slaa, uzushi nk. ni hao hao.

Leo hii wamefanikiwa kila mmoja anasema nini, tulinde amani na utulivu... Watanzania tutasikiliza na kutulia, watagonga tano na kuendelea kula.

Haya mafanikio ambayo watu wanafurahia, kuna watu baadhi ya majimbo wako ndani kwa kuwa walijitolea kupambana kulinda matokeo na kuzuia wizi wa hizo kura, hivi kuna mtu kati yetu anawakumbuka hawa hata kuwasaidia kwenye hizo kesi?

Ninachojua mimi kwa utaratibu tulio nao wa maneno matupu... hali itaendelea kuwa hivi forever, hivi jamani lets be serious, mnadhani hawa jamaa watakuja kukubali tu kirahisi kuachia hiyo keki?

Watoto na vizazi vyetu watakuja kutuhukumu!!

Bila kuungana vyama vya upinzani na kuamua kwa uhakika kwamba sasa basi, hakika tutabaki kuishi kwenye nchi hii ya amani na utulivu wa kufikirika.
 
Kama umekerwa na matokeo na hukupiga kura, tatizo ni nini...... uongozi si chakula kwamba wamwambia mkeo au mumeo akubadilishie ni ujumla wa mawazo ya walio wengu kwa tumaili la pamoja, kidumu chama cha mapinduzi
 
kwa wanachama wa chadema jiandaeni vizuri maana upinzani ni nyie tuuuuu tlp, nccr, cuf na wengine wamekufa.... Heheeeee kidimu chama tawala
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom