Angalizo kwa wana JF - Lugha ya matumizi ya nguvu haina nafasi

Status
Not open for further replies.
Kwa wachangiaji wengi makini hapa JF hiki kilikuwa kipindi cha kupumzika kwa sababu kuna wengine wameigeuza forum kuwa battleground pengine kwa kujua au kutojua! Kwa kweli michango mingi humu ndani wakati wa kampeni na wakati wa matokeo ilikuwa terrible na unaweza kusema uhuru wa habari uliopitiliza kama ulioonekana humu unatia kichefu chefu. Watu tuna tofauti, lakini viwango vya ustaarabu havitofautiani sana.

Vile vile kuna watu wameamua kutumia kipindi hiki cha uchaguzi kuchafua hali ya hewa na kuifanya social media kama Jamii Forums ionekane kama kitu kisichofaa! Pengine hawa walikuwa wengi sana kipindi hiki, na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuwa-put off watu wengi wanaoiona jamii forums kama channel muhimu ya kupata habari na fikra huru zisizo-haririwa.

Mimi nashauri members wapya sana wawe wanapewa nafasi ya kuona content tu bila kupewa ruhusa ya kuchangia. Member mpya akisajiliwa awe anapewa kama One month ya kukaa kama observer kabla ya kuruhusiwa ku-post kitu chochote kwenye forum. Nahisi kuna watu humu wakiona hoja zinazowashinda hukimbilia kujisajili kwa ID mpya na kuvuruga mijadala yenye hoja hizo. Hili linawezekana kutokana na urahisi wa kujisajili upya na kuanza kuchangia. At least masharti haya yanaweza kuwekwa katika baadhi ya majamvi tu, sehemu kama mapenzi na mahusiano watu waruhusiwe kujimwaga.

Ni kweli mijadala mingi isiyokuwa na lugha za kistaarabu inavuruga sana forums na kufanya wale wanaoitegemea kuchukia na kutafuta alternative source.

Siasa ni mchezo msafi, kwani siasa hutoa viongozi wanaotakiwa kuwaongoza watu. Si ajabu kuwa nchi yetu inaendelea kuzama katika lindi la umaskini, ikiwa tunaendelea kuichukulia siasa kama ni sehemu ya kutumia hila, fitna na uzandiki kiasi cha watanzania kuaminishwa kuwa siasa ni MCHEZO MCHAFU. Mchezo mchafu, hauwezi kutoa washindi wasafi. Taifa linatakiwa kuongozwa na watu wasafi. Lazima tuseme kuwa siasa zetu tunaziendesha vibaya ndo maana matokeo yake ni mabaya kwetu wote.

Tunataka mabadiliko, lazima tutumie njia safi ili kujitenga na wanaotumia njia mbovu. Tunajua fitna na hila zitaendelea kuwepo na kwa kipindi fulani zitaonekana kushinda. Lakini dawa yake ni kuzikataa hila na fitna sehemu yoyote tunapopata nafasi ya kufanya hivyo, hatimaye ukweli utasimama. Kujaribu kumuondoa nyoka ndani ya nyumba kwa kuichoma moto inaweza isiwe uamzi wa busara sana!
 
ulichokisema mwanakijiji ni cha ukweli hatupingi,ila utambue kuwa ni matokeo ya wizi na mwenendo mbaya wa uongozi wa hii tz ndio unawafanya watu kuwa na hasira hadi kutumia hoja zenye hasira ndani yake,kwani kumbuka,ni hatari sana kumfanya mwenzako ni mjinga na akatambuwa kuwa wa mfanya yeye ni mjinga kitakachotokea ni kile ambacho baadhi wanajamii forum wanakitoa sasa,ni kweli tunahitaji kubadilika ili tuiweke JF Katika mazingira salama

MAPINDUZIIIIIIIIIIIII DAIMAAAAAAAAA
 
ahante MMKJJ, hili limekuja wakati muafaka na imezidi kunidhihirishia kuwa kimya kingi kina mshindo mkuu!

Haya tusonge mbele tena kwa busara na maarifa, hii nguvu tuliyo nayo isiishie hapa bali haya yaliyokusudiwa kutukatisha tamaa yawe chachu ya mema na makubwa zaidi!

JOY COMES WITH THE MORNING.... KUMEKUCHAAAAAAAAAAAA!!!
 
Ndugu Wana JF,

Naunga mkono hoja, mi nadhani ingewezekana kuwe na utaratibu kila Mwezi au kila wiki MOD awe anatoa list ya watu waliokiuka maadili ya uchangiaji tuwakanye na wale waliokuwa na mchango mkubwa itolewe list yao then tuwapongeze.

Utaratibu huu utatusaidia kuweza kuwa objective na kuwa na self evaluation ya jinsi tunavyotoa michango yetu humu ndani.

Nashukuru sana
 

Utaratibu huu utatusaidia kuweza kuwa objective na kuwa na self evaluation ya jinsi tunavyotoa michango yetu humu ndani.
Naunga hoja ya MMKJ 100%.

Na pia hapo kwenye Red hakuna haja ya kumpa MOD kazi hiyo. Kazi hii ya kuchambua wote waliopitiwa/kuzidiwa na jazba na kutoa matusi na lugha za uchochezi inaweza kufanywa na sisi Members bila kupoteza muda wa MOD.
 
Napinga hoja!

Mabadiliko ya Uongozi wa Siasa katika nchi yetu hautapatikana kupitia "Ballot Boxes"...PERIOD!

Lazim itumike njia mubadala kurudisha heshima katika jamii
 
Ucmtishe ndugu Melo, hakuna mtu atakayeishi kwa tabu mimi naunga mkono hoja zote za wachangiaji wa maneno ya busara ya mwanakijiji, ukweli ni kuwa ktk forum hii tulijikita zaidi kiupnzani tukasahau kuwa hii ni part ya media, na ilitakiwa isiwe na bias sas sisi tukawa biased, anyway whatever happened in the electin months happened with reasons aliye na masikio na asikie na mwenye macho atazame.

Tulio great thinkers tuendelee kutoa na kuchangia hoja, tupunguze jazba, kufungiwa ndugu notradamme tutafungiwa wengi tu kama hutuleti habari zenye ushahidi
 
MMKJ,
asante kwa kuni-quote.
Nilichosema nimekimaanisha. Unajua vema kwamba wewe na institution yako inaweza kutengeneza taswira ya mambo lakini inaweza kupenya kwenye vichwa vya watu wachache sana. "thanks" za jf zisikutie kiburi.
We know you better.........support yako ya kifiki kwa wana-mageuzi wa nchi hii tunaijua vyema. Wewe si ndio ulikuwa muasisiwa CCJ katika dakika za mwisho za kueleka uchaguzi mkuu? kiliposambaratika ulikuja na hoja gani? CHEAP.

Taarifa zako za Meremeta ulizoleta hapa zilikuwa zinamsaidia nani? ulijaribu kuonyesha kuwa Meremeta ni swala kubwa kuliko tunavyoweza kufikiri, point yako ni kwamba, it is a global issue, na inahusisha watu amabo kimsingi hatuwezi kuwafanya chochote. ILIKUWA NI REPORT YA KUTUKATIZA TAMAA SISI WATANZANIA tusiendelee kuhoji tena Meremeta.

Naweza kuendelea lakini, haina maana. Kama unataka nipige IP ban!
 
Huwezi kuibiwa alafu useme tujenge hoja zenye msingi! We are simply stating the facts and reflect our emotions. We speak the truth and we dare to speak openly! Hizo hoja za itikadi ya nguvu ni zipi?
 
Tayari wana mabadiliko tumefanya vizuri sana kwenye uchaguzi huu, hakuna mtu mwenye sababu ya kutembea kichwa kainamisha chini au kujaribu kujisikia vibaya; ukisukuma mlango ambao wao wanausukuma usifunguka na ukafanikiwa kuuachia, basi kumalizia ni juhudi kidogo tu. Malango yametikisika, na mlango umeachia.. sasa tusije tukajikuta tunapoteza muda wakati wao wanaubamiza tena dhidi yetu.
 
Tayari wana mabadiliko tumefanya vizuri sana kwenye uchaguzi huu, hakuna mtu mwenye sababu ya kutembea kichwa kainamisha chini au kujaribu kujisikia vibaya; ukisukuma mlango ambao wao wanausukuma usifunguka na ukafanikiwa kuuachia, basi kumalizia ni juhudi kidogo tu. Malango yametikisika, na mlango umeachia.. sasa tusije tukajikuta tunapoteza muda wakati wao wanaubamiza tena dhidi yetu.

wabunge 20 ndo success?
 
Mzee, Mwana wa Kijiji, nakuunga mkono. Utamu wa mjadala ni kujadili HOJA ya mtu bila JAZBA, bali kuzingatia mantiki, mtiririko na ufinyu (weakness) katika hoja inayojadiliwa, bila kuwa na uharaka wa kutumia NGUVU za mwili kwa kutumia maneno. Napenda kuwaomba wachangiaji wenzangu kujenga hoja katika kupinga hoja! nakushukuruni.
 
MMKJ,
asante kwa kuni-quote.
Nilichosema nimekimaanisha. Unajua vema kwamba wewe na institution yako inaweza kutengeneza taswira ya mambo lakini inaweza kupenya kwenye vichwa vya watu wachache sana. "thanks" za jf zisikutie kiburi.
We know you better.........support yako ya kifiki kwa wana-mageuzi wa nchi hii tunaijua vyema. Wewe si ndio ulikuwa muasisiwa CCJ katika dakika za mwisho za kueleka uchaguzi mkuu? kiliposambaratika ulikuja na hoja gani? CHEAP.

Taarifa zako za Meremeta ulizoleta hapa zilikuwa zinamsaidia nani? ulijaribu kuonyesha kuwa Meremeta ni swala kubwa kuliko tunavyoweza kufikiri, point yako ni kwamba, it is a global issue, na inahusisha watu amabo kimsingi hatuwezi kuwafanya chochote. ILIKUWA NI REPORT YA KUTUKATIZA TAMAA SISI WATANZANIA tusiendelee kuhoji tena Meremeta.

Naweza kuendelea lakini, haina maana. Kama unataka nipige IP ban!

Hivi tangu lini Mzee Mwanakijiji anatoa "ban"? Mkosoe tu kwa raha zako wala usiogope. Mbaya ni matusi na lugha za vitisho zitakazoweza kutuangamiza wote.

Amandla.......
 
mzee MKJJ umenena.

Uchaguzi huu ni wa mafanikio makubwa katika harakati za kuleta mabadiliko yenye manufaa kwa watanzania. Tumepiga hatua. Ndio. Ingeweza kuwa ni hatua kubwa zaidi lakini kwa sababu tunazozijua za upigaji kura na utangazaji matokeo, mambo yako kama yalivyo. Hatujapoteza sana. Bado tunatembea kifua mbele. Nashauri hasira zetu tuzielekeze kwenye maeneo matatu yafuatayo:

1. Vyama vya upinzani vilivyochukua majimbo na vilivyochukua Halmashauri za Wilaya/Manispaa etc wawaonyeshe watanzania kwa vitendo jinsi wanavyoitafsiri ilani za vyama vyao. Waonyeshe kuwa kuna tofauti kati ya uongozi wa sasa na utawala uliopita. Hii itajenga imani kwa umma na kuwa mifano ya mafanikio na mtaji kwenye kampeni za chaguzi zijazo.

2. Wapenda mabadiliko tutumie nguvu ya hoja na ushawishi uliokwenda shule kuwaamsha watz ili wafuatilie kwa karibu utekelezaji wa serikali inayoingia madarakani ahadi zote zilizotolewa wakati wa kampeni. Hili lianze immediately baada ya kuapishwa kwa baraza la mawaziri.

3. Wapiganaji waliofanikiwa kuingia bungeni kwa mara ya kwanza (hasa vijana) wasisinzie. Wawadhihirishie watanzania kuwa wanaweza ili kujenga imani kwa umma kuwa vijana wanahitaji kupewa nafasi zaidi. Wajue pia mjengoni kuna kanuni zake, hivyo kila mara wapate ushauri kwa wapiganaji wanaoitetea nchi ambao wana uzoefu wa shughuli za bunge ( Dr. Slaa et al)

ROME WAS NOT BUILT IN A DAY!!!!!!!!!!

TOGETHER WE CAN!
 
Mwanakijiji:

Heshima mkuu. Nilikuwa nasubiri kwa hamu posti zako. Kuna Mzee mmoja maarufu, jina kapuni, alipoandika barua wakati akiwa na hasira haikuipeleka moja kwa moja posta. Aliiweka kwenye droo ya meza na kesho yake aliisoma tena na kuandika barua nyingine. Kwa mtindo huu aliweza kuwa makini na kile alichoandika.

Uchaguzi Tanzania ni kama mitihani ya shule ambayo kazi yake ni kuchagua watakaoendelea mbele. Lakini tukichukua kuwa uchaguzi au mitihani kuwa ni kigezo cha tathmini ya maendeleo, kuna mambo mengi ya kujifunza na vyama vya upinzani vina haki zote za kujisifu na kutumia matokeo ya uchaguzi kupanga mikakati ya baadaye.

Nimetoka katika jimbo ambalo limechagua mbunge kutoka CCM. Na matokeo yalipotangazwa characterization ya kwanza ni kuwa jimbo letu ni la watu wasio soma na matusi mengine. Matusi haya yananifanya niwe na wasiwasi na mabadiliko yanayotakiwa na wanaJF.

Kwa bahati nzuri namfahamu mbunge wa jimbo letu. Kwa miaka miwili alikuwa anajiandaa kwa uchaguzi huu. Na katika kipindi cha miaka hiyo miwili kulikuwa hakuna network ya chama chochote cha upinzani. Sasa watu wanapopiga kura kumchagua mtu wanayemfahamu kwanini waitwe wajinga.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom