SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,432
- 23,754
- Thread starter
- #41
ANGA LA WASHENZI ---- 02
Simulizi za series
“Vipi, kaka kuna tatizo?” Mwanamke aliuliza. Alikuwa amevalia suruali ya jeans na tisheti nyeupe ya bia ya Serengeti. Mkono wake wa kuume alikuwa ameshikilia sahani ndefu ya plastiki iliyobebelea kinywaji cha Balimi.
.
.
.
“Hamna tatizo dada,” Jona alijibu akipangusa uso. Alinyanyua kinywaji chake akapiga mafundo mawili. Mwanamke alimtazama kwa mashaka. Ni wazi alikuwa anastaajabu kutingwa kule kwa mwanaume huyo.
.
.
.
“Samahani,” akasema. “Nilitaka kujua kama utahitaji chochote toka jikoni.”
“Ooh, kuna chakula gani?” Jona akauliza akiketi vema kitini.
“Nyama ya kukaanga, rosti, ndizi, chips na ugali.”
.
.
.
Jona akatazama saa yake ya mkononi. Muda ulikuwa umeenda, na pia alihisi uchovu. Aliona ni vema akabeba chakula moja kwa moja aende nacho nyumbani, hivyo akaagizia na kungoja.
.
.
.
Baada ya muda mfupi, chakula kikaletwa, akalipia na kuondoka.
Toka hapo bar mpaka nyumbani kwake si mbali. Mwendo wa wastani ungekufikisha kwa takribani dakika kumi. Kama ukikazana unaweza kuchukua hata dakika tano tu. Ila Jona hakuwa na haraka na nyumbani. Hakuwa na cha kuwahi, labda kama kungekuwa kuna mvua ingemkimbiza. .
.
.
Mvua ilikuwa imekata, manyunyu tu ndiyo yalikuwa yanashuka. Nyumbani hakukuwa na mtu wa kumngojea, anaishi peke yake. Miguu yake ilitembea taratibu akitazama chini. Alipokaribia nyumbani kwake, akaona kuna gari limesimama kwa mbele, shaka likampata.
Alisimama upesi, akalichambua gari hilo. Alisogea kidogo apate kuliona vema. Mara akagundua ni lile lile aliloliona kule kazini likiwa limesimama, na kisha kuondoka.
.
.
.
Lilikuwa ni Range Rover Sport, pleti namba yake ya Kenya.
Jona akajikuta anapata maswali. Akiwa hapo anaendelea kutazama, akamuona mwanamke mmoja akitokea gizani, akapanda ndani ya gari hilo upesi. Mavazi ya mwanamke huyo yalimfanya Jona aamini ndiye yule mwanamke aliyemtembelea kazini akidai mzigo wa Beatrice.
.
.
.
Ina mana amenifuata nyumbani? Alijiuliza. Kumbe ndiye yeye aliyekuwa ndani ya gari hilo kule nje ya mabanda!
.
.
.
Hakutoka hapo alipokuwa amejibanza. Macho yake yaliendelea kutazama gari akingojea liondoke. Aliminya mfuko wa chakula, akasonya.
.
.
“Chakula kinapoa.”
.
.
Punde anamuona mwanaume mmoja mrefu akiwa kando na gari. Hakujua ametokea wapi. Mwanaume huyo aliegeza mikono yake dirishani mwa gari akasimama hapo kwa muda kidogo. Bila shaka alikuwa anaongea jambo na mtu ama watu waliomo ndani ya gari. .
.
.
Alitazama huku na kule, akapanda kwenye chombo wakaondoka. Jona alisindikiza hilo gari mpaka lilipoyoyoma kisha akatoka alipokuwa na kuenenda nyumbani kwake. .
.
.
Ilikuwa ni nyumba ya wastani, sebule na vyumba viwili, yenye uzio mfupi wa tofali na geti dogo jeusi. Ilikuwa kimya na tulivu sana, pia ilikuwa giza. .
.
.
Jona alikula kisha akaelekea chumbani kwake pasipo kupoteza muda. Kilikuwa ni chumba kipana kidogo, kitanda kikubwa na kabati moja kubwa la nguo lenye kioo kipana. Pembezoni mwa kabati hilo kulikuwa kuna kitu kikubwa chenye pembe nne kikiwa kimefunikwa na shuka la kijivu.
Jona alioga, kisha akafungua kabati lake na kitoa kisanduku fulani cha mbao, kidogo kwa umbo. Alikifungua, ndani yake kulikuwa kuna brashi kadhaa za kuchorea, mirija kadhaa ya rangi na penseli za mikaa, charcoal pencils.
.
.
.
Alikiweka kisanduku hicho juu ya stuli aliyosogeza karibu na kitu kilichofunikwa na shuka, kisha akalibandua shuka hilo. Kumbe hapo kulikuwa kuna makaratasi lukuki meupe marefu, mahususi kwa ajili ya kuchorea.
.
.
.
Karatasi ya kwanza kabisa ilikuwa ina picha ya mwanamke mrembo mwenye nywele za rasta. Jona aliitazama picha hiyo kwa sekunde kadhaa akifikiria jambo.
.
.
.
Mwanamke alikuwa anatabasamu, macho yake yaliangaza. Jona naye akajikuta anatabasamu, ila macho yake yakiwa mekundu.
.
.
.
Alifungua picha nyingine, picha ya mtoto wa kiume mwenye makadirio ya miaka mitatu.
.
.
.
Alitazama picha hiyo kwa sekunde kadhaa kabla hajaigeuza na kukutana na karatasi mpya isiyo na mchoro wowote. Hapo akaanza kuchora kwa kutumia penseli.
.
.
.
Hakutazamia popote pale isipokuwa alirejea kichwani mwake. Alichora picha ya mwanamke, yule aliyekuja kumtembelea ofisini akidai mzigo wa Beatrice. Alimchora mwanamke huyo hivyo hivyo kama anavyoonekana kuanzia kichwani mpaka kifuani asisahau hata vazi.
.
.
.
Alipomaliza aliketi kando, akitazama picha hiyo kwa umakini. Alijiuliza maswali kadhaa lakini hakuyapatia majibu. Alitamani Beatrice angekuwepo karibu ili amuulize, au basi angekuwa na simu ampigie.
Mwishowe anaamua kuipuuzia, anafuata jokofu sebuleni na kutoa chupa kubwa ya whisky anayoanza kuigida akielekea chumbani. Alikunywa chupa yote, kisha akalala.
.
.
.
Hawezi kulala pasipo kufanya hivi. Hujaza jokofu lake mara kwa mara kwa vileo vikali, kwa kazi moja tu, kumsaidia alale.
.
.
.
Asipokunywa, usingizi huwa mrefu kupitiliza. Ataamka na kushtuka kila mara. Hatapata amani.
Amekuwa akifanya hivi kwa takribani miaka mitatu sasa. Tangu pale alipoacha kazi yake ya uaskari, akiwa inspekta mwadilifu. .
.
.
Ni miaka hiyo ya nyuma, mwanaume huyu alikuwa na furaha akitenda kazi yake kiufanisi. Alisuluhisha kesi kedekede zilizoonekana ngumu na zisizowezekana mbele ya macho ya wengine. Alifanikiwa kwa kiasi kikubwa kumaliza makundi ya majambazi yaliyokuwa yameweka makazi yake ndani ya jiji la Dar es salaam.
.
.
.
Alifahamika kwa jina la Joh 'the knife', moto wa kuuotea mbali. Mwanaume mwenye mateke mazito, ngumi za kasi na matumizi mazuri ya silaha, haswa kisu. Hata kivuli chake kilikuwa kinaogopesha.
.
.
.
Simulizi hiyo ya kupendeza ilikuja kuhitimishwa muda mfupi baada ya baba yake mzazi alipofariki akiwa kazini, kituo cha polisi. Babaye alikuwa ni miongoni mwa maafisa polisi waliouawa kwenye mashambulizi ya majambazi vituoni vya polisi kwa dhumuni la kupoka silaha.
.
.
.
Ilikuwa bado miezi mitatu tu mzee huyo astaafu, adha hiyo ya kifo ikamkumba. Jambo hili lilimuuma sana Jona, akaapa kutafuta wahusika wote na kuwatia nguvuni. Ilimgharimu mwezi tu kufanikisha adhma hiyo. Alipomaliza akaamua kuacha kazi papo hapo.
Maamuzi haya hakushawishiwa na yeyote yule isipokuwa akili yake. Alirudisha kila kitu cha jeshi akiandika barua ya kushindwa kuendelea na majukumu. Barua hiyo haikueleza sababu, bali tu hitaji.
.
.
.
Kiuhalisia, Jona alisononeshwa sana na namna jeshi la polisi lilivyomhudumia na kumjali marehemu baba yake. Aliona anastahili zaidi ya kile alichopewa na jeshi hilo. Alilipigania sana, alilitendea kazi kwa uadilifu na kwa uaminifu. Heshima aliyopata, haikuwa hata theluthi ya yale aliyotenda.
.
.
"Nami nikifa nitatendwa hivi hivi," alikuwa anasema Jona.
"Kama wameshindwa kumthamini baba yangu aliyewatumikia miaka nenda rudi, vipi kwangu? Familia yangu itaachwaje?"
.
.
.
Aliona kazi hiyo haimfai. Aliamua ahamishie nguvu zake kufanya mambo mengine yatakayomletea faida zaidi, ambayo ni kujihusisha na biashara. Kuwepo ndani ya jeshi la polisi kulikuwa kunamkumbusha baba yake na kifo chake. Mara kadhaa alijikuta anajiuliza endapo angekuwa katika nafasi ya baba yake, familia yake ingebakije, ingeishije? Upuuzi.
.
.
.
Alitaka kupumzisha akili yake na purukushani. Alikuwa na ndoto za kufanya biashara, atengeneze faida kisha aende mbali kabisa, ulimwengu mwingine ambapo hakutakuwa na simu za kuitwa ofisini wala kazi za kutumikishwa. Atakuwa na familia yake tu, karibu kabisa na maji ya bahari, visiwa, samaki, moto na miti.
Ila matarajio hayo yote yanakatwa ghafla kana kwamba kibatari mbele ya kimbunga. Familia yake inauawa kwenye moto mkali ulioteketeza nyumba. Biashara yake ya kusafirisha korosho nje ya nchi inakufa, mtaji unakata. .
.
.
Mambo haya yanatukia kwa haraka sana. Yanamwacha Jona katika fikirishi kali maisha yake yakigeuka juu chini, chini juu. Ni ndani ya muda mfupi anapoteza mihimili yake ya maisha. Anageuka kuwa fukara, na ombaomba.
.
.
.
Katika kipindi hicho cha ukata mnene, jeshi la polisi likatupa ndoana kwa Jona kumtaka arejee kazini kabla hajafa kibudu.
.
.
.
Lakini, ingawa Jona hakuwa na mbele wala nyuma, akakataa kata kata, wakati huo hana hata uhakika wa chakula mezani.
Lakini je nani aliyapanga mambo haya yote kwa Jona? Yalitukia tu? .
.
.
Taarifa ya kikosi cha zimamoto na uokoaji, ilisema nyumba iliungua kwa hitilafu za umeme. Sababu ambayo haikukuna kabisa kichwa cha Jona kwani aliamini aliweka makazi yake katika usalama kwa kufunga vifaa vya kuzima umeme punde tu hitilafu inapobainika.
.
.
.
Isitoshe, kama ukimuuliza leo hii kwanini biashara yake, iliyoanza kuchanua, ilikufa hatakupa jibu la kueleweka. Hajui. Ni ndani ya juma moja tu, mtandao wake wa biashara ukakata huko Vietnam, mizigo yake ikazuiliwa bandarini na kugubikwa na urasimu mkubwa.
.
.
.
Kama haikuwa kipaji chake cha kuchora, hakujua maisha yake yangeenda wapi. Angalau alipata chakula na hata nauli za kumsogeza toka eneo moja kwenda lingine. Japokuwa pesa ilikuwa finyu!
Sasa kivipi mtu huyu atalala pasipo kilevi? Kwake, haikuwezekana. Alishuka chini kama embe lidondokavyo mtini. Alikuwa kama bado yu kwenye bumbuwazi. .
.
.
Ikiwa ni kwenye komo la usiku, majira ya saa kumi na moja, gari nyeusi Mark X, inasogea mbele kidogo ya geti la Jona na kusimama. Anashuka mwanamke mmoja mrefu aliyevalia kimini kifupi cheusi na viatu vyenye kisigino kirefu.
.
.
.
Mwanamke huyo alikuwa na nywele nyingi alizozikusanya na kuzibana kwa kamba nyekundu, uso wake mnene ulikuwa una miwani ya macho yenye fremu nzito.
.
.
.
Aliegemea gari akitazama nyumba ya Jona. Punde akamwona mwanaume huyo akifungua mlango na kutoka ndani.
Ilikuwa rahisi kwake kumuona Jona kuliko Jona kumuona kwani yeye alikuwa gizani wakati Jona akiwa kwenye mwanga.
.
.
.
Jona alifika getini ndiyo akajua kuna mtu yupo kando. Alishtuka, lakini hakumpa faida hiyo mgeni. Alisogea kwa kujiamini akasimama akimtazama mwanamke aliyekuwa hapo.
.
.
.
"Wewe nani?" Aliuliza pasipo salamu. Macho yake yalikuwa mekundu. Alikunja ndita.
"Habari yako?" Mwanamke akasalimu kwa sauti tamu.
"Nzuri," Jona akajibu.
"Samahani kwa kukusumbua, Jona. Najua huu ndio muda pekee wa kukupata maana umekuwa ukishughulika na kubanwa kwa siku nzima. Kwa jina naitwa Nade, ni mtumishi wa Mheshimiwa Eliakim Mtaja, nimekuja kukufikishia wito wake binafsi kwako. Anakuhitaji.
"Ananihitaji kivipi?" Akauliza Jona.
"Nadhani ingekuwa vizuri ukaongea naye, sina majibu ya kukuridhisha. Naweza nikakupeleka?"
"Hapana, huwezi."
"Jona, sasa mheshimiwa atakupataje?"
"Sijui."
"Una simu?"
"Hapana."
.
.
.
Mwanamke alifungua gari mlango wa nyuma akatoa Nokia xperia nyeusi akamkabidhi Jona.
.
.
.
"Ina kila kitu. Bila shaka mtawasiliana kwa kutumia hiyo."
Jona akapandisha kichwa juu.
"Sawa," alijibu kiufupi.
"Naweza nikakupeleka job?" Mwanamke aliuliza.
"Hapana," akajibu Jona. "Nashukuru."
.
.
.
.
***
***
Simulizi za series
“Vipi, kaka kuna tatizo?” Mwanamke aliuliza. Alikuwa amevalia suruali ya jeans na tisheti nyeupe ya bia ya Serengeti. Mkono wake wa kuume alikuwa ameshikilia sahani ndefu ya plastiki iliyobebelea kinywaji cha Balimi.
.
.
.
“Hamna tatizo dada,” Jona alijibu akipangusa uso. Alinyanyua kinywaji chake akapiga mafundo mawili. Mwanamke alimtazama kwa mashaka. Ni wazi alikuwa anastaajabu kutingwa kule kwa mwanaume huyo.
.
.
.
“Samahani,” akasema. “Nilitaka kujua kama utahitaji chochote toka jikoni.”
“Ooh, kuna chakula gani?” Jona akauliza akiketi vema kitini.
“Nyama ya kukaanga, rosti, ndizi, chips na ugali.”
.
.
.
Jona akatazama saa yake ya mkononi. Muda ulikuwa umeenda, na pia alihisi uchovu. Aliona ni vema akabeba chakula moja kwa moja aende nacho nyumbani, hivyo akaagizia na kungoja.
.
.
.
Baada ya muda mfupi, chakula kikaletwa, akalipia na kuondoka.
Toka hapo bar mpaka nyumbani kwake si mbali. Mwendo wa wastani ungekufikisha kwa takribani dakika kumi. Kama ukikazana unaweza kuchukua hata dakika tano tu. Ila Jona hakuwa na haraka na nyumbani. Hakuwa na cha kuwahi, labda kama kungekuwa kuna mvua ingemkimbiza. .
.
.
Mvua ilikuwa imekata, manyunyu tu ndiyo yalikuwa yanashuka. Nyumbani hakukuwa na mtu wa kumngojea, anaishi peke yake. Miguu yake ilitembea taratibu akitazama chini. Alipokaribia nyumbani kwake, akaona kuna gari limesimama kwa mbele, shaka likampata.
Alisimama upesi, akalichambua gari hilo. Alisogea kidogo apate kuliona vema. Mara akagundua ni lile lile aliloliona kule kazini likiwa limesimama, na kisha kuondoka.
.
.
.
Lilikuwa ni Range Rover Sport, pleti namba yake ya Kenya.
Jona akajikuta anapata maswali. Akiwa hapo anaendelea kutazama, akamuona mwanamke mmoja akitokea gizani, akapanda ndani ya gari hilo upesi. Mavazi ya mwanamke huyo yalimfanya Jona aamini ndiye yule mwanamke aliyemtembelea kazini akidai mzigo wa Beatrice.
.
.
.
Ina mana amenifuata nyumbani? Alijiuliza. Kumbe ndiye yeye aliyekuwa ndani ya gari hilo kule nje ya mabanda!
.
.
.
Hakutoka hapo alipokuwa amejibanza. Macho yake yaliendelea kutazama gari akingojea liondoke. Aliminya mfuko wa chakula, akasonya.
.
.
“Chakula kinapoa.”
.
.
Punde anamuona mwanaume mmoja mrefu akiwa kando na gari. Hakujua ametokea wapi. Mwanaume huyo aliegeza mikono yake dirishani mwa gari akasimama hapo kwa muda kidogo. Bila shaka alikuwa anaongea jambo na mtu ama watu waliomo ndani ya gari. .
.
.
Alitazama huku na kule, akapanda kwenye chombo wakaondoka. Jona alisindikiza hilo gari mpaka lilipoyoyoma kisha akatoka alipokuwa na kuenenda nyumbani kwake. .
.
.
Ilikuwa ni nyumba ya wastani, sebule na vyumba viwili, yenye uzio mfupi wa tofali na geti dogo jeusi. Ilikuwa kimya na tulivu sana, pia ilikuwa giza. .
.
.
Jona alikula kisha akaelekea chumbani kwake pasipo kupoteza muda. Kilikuwa ni chumba kipana kidogo, kitanda kikubwa na kabati moja kubwa la nguo lenye kioo kipana. Pembezoni mwa kabati hilo kulikuwa kuna kitu kikubwa chenye pembe nne kikiwa kimefunikwa na shuka la kijivu.
Jona alioga, kisha akafungua kabati lake na kitoa kisanduku fulani cha mbao, kidogo kwa umbo. Alikifungua, ndani yake kulikuwa kuna brashi kadhaa za kuchorea, mirija kadhaa ya rangi na penseli za mikaa, charcoal pencils.
.
.
.
Alikiweka kisanduku hicho juu ya stuli aliyosogeza karibu na kitu kilichofunikwa na shuka, kisha akalibandua shuka hilo. Kumbe hapo kulikuwa kuna makaratasi lukuki meupe marefu, mahususi kwa ajili ya kuchorea.
.
.
.
Karatasi ya kwanza kabisa ilikuwa ina picha ya mwanamke mrembo mwenye nywele za rasta. Jona aliitazama picha hiyo kwa sekunde kadhaa akifikiria jambo.
.
.
.
Mwanamke alikuwa anatabasamu, macho yake yaliangaza. Jona naye akajikuta anatabasamu, ila macho yake yakiwa mekundu.
.
.
.
Alifungua picha nyingine, picha ya mtoto wa kiume mwenye makadirio ya miaka mitatu.
.
.
.
Alitazama picha hiyo kwa sekunde kadhaa kabla hajaigeuza na kukutana na karatasi mpya isiyo na mchoro wowote. Hapo akaanza kuchora kwa kutumia penseli.
.
.
.
Hakutazamia popote pale isipokuwa alirejea kichwani mwake. Alichora picha ya mwanamke, yule aliyekuja kumtembelea ofisini akidai mzigo wa Beatrice. Alimchora mwanamke huyo hivyo hivyo kama anavyoonekana kuanzia kichwani mpaka kifuani asisahau hata vazi.
.
.
.
Alipomaliza aliketi kando, akitazama picha hiyo kwa umakini. Alijiuliza maswali kadhaa lakini hakuyapatia majibu. Alitamani Beatrice angekuwepo karibu ili amuulize, au basi angekuwa na simu ampigie.
Mwishowe anaamua kuipuuzia, anafuata jokofu sebuleni na kutoa chupa kubwa ya whisky anayoanza kuigida akielekea chumbani. Alikunywa chupa yote, kisha akalala.
.
.
.
Hawezi kulala pasipo kufanya hivi. Hujaza jokofu lake mara kwa mara kwa vileo vikali, kwa kazi moja tu, kumsaidia alale.
.
.
.
Asipokunywa, usingizi huwa mrefu kupitiliza. Ataamka na kushtuka kila mara. Hatapata amani.
Amekuwa akifanya hivi kwa takribani miaka mitatu sasa. Tangu pale alipoacha kazi yake ya uaskari, akiwa inspekta mwadilifu. .
.
.
Ni miaka hiyo ya nyuma, mwanaume huyu alikuwa na furaha akitenda kazi yake kiufanisi. Alisuluhisha kesi kedekede zilizoonekana ngumu na zisizowezekana mbele ya macho ya wengine. Alifanikiwa kwa kiasi kikubwa kumaliza makundi ya majambazi yaliyokuwa yameweka makazi yake ndani ya jiji la Dar es salaam.
.
.
.
Alifahamika kwa jina la Joh 'the knife', moto wa kuuotea mbali. Mwanaume mwenye mateke mazito, ngumi za kasi na matumizi mazuri ya silaha, haswa kisu. Hata kivuli chake kilikuwa kinaogopesha.
.
.
.
Simulizi hiyo ya kupendeza ilikuja kuhitimishwa muda mfupi baada ya baba yake mzazi alipofariki akiwa kazini, kituo cha polisi. Babaye alikuwa ni miongoni mwa maafisa polisi waliouawa kwenye mashambulizi ya majambazi vituoni vya polisi kwa dhumuni la kupoka silaha.
.
.
.
Ilikuwa bado miezi mitatu tu mzee huyo astaafu, adha hiyo ya kifo ikamkumba. Jambo hili lilimuuma sana Jona, akaapa kutafuta wahusika wote na kuwatia nguvuni. Ilimgharimu mwezi tu kufanikisha adhma hiyo. Alipomaliza akaamua kuacha kazi papo hapo.
Maamuzi haya hakushawishiwa na yeyote yule isipokuwa akili yake. Alirudisha kila kitu cha jeshi akiandika barua ya kushindwa kuendelea na majukumu. Barua hiyo haikueleza sababu, bali tu hitaji.
.
.
.
Kiuhalisia, Jona alisononeshwa sana na namna jeshi la polisi lilivyomhudumia na kumjali marehemu baba yake. Aliona anastahili zaidi ya kile alichopewa na jeshi hilo. Alilipigania sana, alilitendea kazi kwa uadilifu na kwa uaminifu. Heshima aliyopata, haikuwa hata theluthi ya yale aliyotenda.
.
.
"Nami nikifa nitatendwa hivi hivi," alikuwa anasema Jona.
"Kama wameshindwa kumthamini baba yangu aliyewatumikia miaka nenda rudi, vipi kwangu? Familia yangu itaachwaje?"
.
.
.
Aliona kazi hiyo haimfai. Aliamua ahamishie nguvu zake kufanya mambo mengine yatakayomletea faida zaidi, ambayo ni kujihusisha na biashara. Kuwepo ndani ya jeshi la polisi kulikuwa kunamkumbusha baba yake na kifo chake. Mara kadhaa alijikuta anajiuliza endapo angekuwa katika nafasi ya baba yake, familia yake ingebakije, ingeishije? Upuuzi.
.
.
.
Alitaka kupumzisha akili yake na purukushani. Alikuwa na ndoto za kufanya biashara, atengeneze faida kisha aende mbali kabisa, ulimwengu mwingine ambapo hakutakuwa na simu za kuitwa ofisini wala kazi za kutumikishwa. Atakuwa na familia yake tu, karibu kabisa na maji ya bahari, visiwa, samaki, moto na miti.
Ila matarajio hayo yote yanakatwa ghafla kana kwamba kibatari mbele ya kimbunga. Familia yake inauawa kwenye moto mkali ulioteketeza nyumba. Biashara yake ya kusafirisha korosho nje ya nchi inakufa, mtaji unakata. .
.
.
Mambo haya yanatukia kwa haraka sana. Yanamwacha Jona katika fikirishi kali maisha yake yakigeuka juu chini, chini juu. Ni ndani ya muda mfupi anapoteza mihimili yake ya maisha. Anageuka kuwa fukara, na ombaomba.
.
.
.
Katika kipindi hicho cha ukata mnene, jeshi la polisi likatupa ndoana kwa Jona kumtaka arejee kazini kabla hajafa kibudu.
.
.
.
Lakini, ingawa Jona hakuwa na mbele wala nyuma, akakataa kata kata, wakati huo hana hata uhakika wa chakula mezani.
Lakini je nani aliyapanga mambo haya yote kwa Jona? Yalitukia tu? .
.
.
Taarifa ya kikosi cha zimamoto na uokoaji, ilisema nyumba iliungua kwa hitilafu za umeme. Sababu ambayo haikukuna kabisa kichwa cha Jona kwani aliamini aliweka makazi yake katika usalama kwa kufunga vifaa vya kuzima umeme punde tu hitilafu inapobainika.
.
.
.
Isitoshe, kama ukimuuliza leo hii kwanini biashara yake, iliyoanza kuchanua, ilikufa hatakupa jibu la kueleweka. Hajui. Ni ndani ya juma moja tu, mtandao wake wa biashara ukakata huko Vietnam, mizigo yake ikazuiliwa bandarini na kugubikwa na urasimu mkubwa.
.
.
.
Kama haikuwa kipaji chake cha kuchora, hakujua maisha yake yangeenda wapi. Angalau alipata chakula na hata nauli za kumsogeza toka eneo moja kwenda lingine. Japokuwa pesa ilikuwa finyu!
Sasa kivipi mtu huyu atalala pasipo kilevi? Kwake, haikuwezekana. Alishuka chini kama embe lidondokavyo mtini. Alikuwa kama bado yu kwenye bumbuwazi. .
.
.
Ikiwa ni kwenye komo la usiku, majira ya saa kumi na moja, gari nyeusi Mark X, inasogea mbele kidogo ya geti la Jona na kusimama. Anashuka mwanamke mmoja mrefu aliyevalia kimini kifupi cheusi na viatu vyenye kisigino kirefu.
.
.
.
Mwanamke huyo alikuwa na nywele nyingi alizozikusanya na kuzibana kwa kamba nyekundu, uso wake mnene ulikuwa una miwani ya macho yenye fremu nzito.
.
.
.
Aliegemea gari akitazama nyumba ya Jona. Punde akamwona mwanaume huyo akifungua mlango na kutoka ndani.
Ilikuwa rahisi kwake kumuona Jona kuliko Jona kumuona kwani yeye alikuwa gizani wakati Jona akiwa kwenye mwanga.
.
.
.
Jona alifika getini ndiyo akajua kuna mtu yupo kando. Alishtuka, lakini hakumpa faida hiyo mgeni. Alisogea kwa kujiamini akasimama akimtazama mwanamke aliyekuwa hapo.
.
.
.
"Wewe nani?" Aliuliza pasipo salamu. Macho yake yalikuwa mekundu. Alikunja ndita.
"Habari yako?" Mwanamke akasalimu kwa sauti tamu.
"Nzuri," Jona akajibu.
"Samahani kwa kukusumbua, Jona. Najua huu ndio muda pekee wa kukupata maana umekuwa ukishughulika na kubanwa kwa siku nzima. Kwa jina naitwa Nade, ni mtumishi wa Mheshimiwa Eliakim Mtaja, nimekuja kukufikishia wito wake binafsi kwako. Anakuhitaji.
"Ananihitaji kivipi?" Akauliza Jona.
"Nadhani ingekuwa vizuri ukaongea naye, sina majibu ya kukuridhisha. Naweza nikakupeleka?"
"Hapana, huwezi."
"Jona, sasa mheshimiwa atakupataje?"
"Sijui."
"Una simu?"
"Hapana."
.
.
.
Mwanamke alifungua gari mlango wa nyuma akatoa Nokia xperia nyeusi akamkabidhi Jona.
.
.
.
"Ina kila kitu. Bila shaka mtawasiliana kwa kutumia hiyo."
Jona akapandisha kichwa juu.
"Sawa," alijibu kiufupi.
"Naweza nikakupeleka job?" Mwanamke aliuliza.
"Hapana," akajibu Jona. "Nashukuru."
.
.
.
.
***
***