Chenge hana kosa lolote, mwenye makosa ni Rais Mkapa, tuanze na huyoNdugu zangu,
Nimeona jana kwenye Tv Andrew Chenge akiwa Mwenyekiti wa Kikao cha Bunge.
Katika mazingira ya sasa, kile cha jana kilipaswa kiwe kikao cha mwisho Andrew Chenge kukiongoza.
Maana, kwa mizoga hii tuliyoonyeshwa kwenye kabati la Chenge, inahitaji ujasiri wa kifisadi kuendelea kukalia kiti cha uenyekiti kuwaongoza Wabunge wa Jamhuri. ' August Session' ni moja ya vikao vya Bunge vyenye hadhi kubwa.
Haviwezi kuongozwa na mtu mwenye tuhuma nzito za ufiaadi na ni dhihaka kubwa kwa Jamhuri inayoongozwa na Rais aliyechaguliwa na aliyesema makubwa jana yenye kumhusisha Chenge pia.
Mimi nadhani, ni wakati sasa, kama Chenge hatajiuzuru mwenyewe nafasi ya uenyekiti Bungeni, Kamati ya Uongozi ya Bunge imshinikize kufanya hivyo. Kazi hiyo si lazima aifanye Kiongozi Mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni, Waziri Mkuu.
Maggid Mjengwa.
Picha: Gazeti Mtanzania.
Kwa kweli RIPKipindi hiki ndio Mwisho wa Kisiasa wa Chenge asichukulie poa kama alivyozoea kuleta dharau zake. Timing is Everything
When I'm Grown Up, Surely I want to be John Andrew Chengechama kipo nyuma yake
Hapo ndo mtapoteana, jaribuni muone.....Chenge atashtakiwa kama AG mstaafu ambaye aliandaa na kushauri serikali kuingia mikataba ya hovyo
Kweli kabisa huu ni upepo tu utapita tuView attachment 523171View attachment 523172
Chenge hili sio la kwanza kwake.Litapita tu kama mengine.Kwa wenye uzoefu wanaweza kulijua hili
Ndio mnavyojidanganyaHakuna wakumgusa Andrew John Chenge.
Hahahhh Mkulu ana mtindo wa kubadilishabadilisha kauli! Kesho anaweza akasema vinginevyo acha tuone tutaishia wapi! Amesema ni kazi ngumu lakini kama Mungu amemweka basi ataifanya kwa kumtegemea Mungu. Katiba Mpya ndio suluhu ya yote haya period!Hususan kwa sababu kapiga deal na Mkapa na Kikwete na amechukua ushahidi wote.
Na Magufuli kashaapa hatawagusa marais wastaafu.
Sasa atamgusa vipi Chenge bila kuwagusa hao marais?
Nyie watu wa ajabu kweli kweli
Kwamba ndio mmejua leo kuwa Chenge hafai?
Mlivyomchagua kuwa mwenyekiti wa Bunge kwa kura nyingi za wabunge wa CCM hamkujua?
Hebu msituchoshe na msitufanye wajinga kwa makosa yenu mnayofanya kila siku.
Waingereza walirudisha chenji ya Rada Bil 40 na ushee na SFO ikasema kabisa Chenge amehongwa...Mlifanya nini?
Msituchoshe wezi nyie CCM


hakuna wa kumgusa jemedari wa vita Chenge inabidi tumshauri aondoke mwenyewe heeee heeee kua na akili kama Chenge ni raha sana.