Andika mkoa na mtaa uliopo uwajue wanaJF walio karibu na wewe

Wizara ya Elimu, Sayansi na
Teknolojia leo January 12, 2018
imetoa agizo kwa shule zote
ambazo ziliwarudisha nyuma
wanafunzi madarasa, au
kuwahamisha au kuwafukuza shule
wanafunzi kwasababu hawakufikia
wastani wa ufaulu husika
kuhakikisha wamewarudisha
wanafunzi hao shule ifikapo
January 20, 2018.
Agizo hilo limeelekeza kuwa kwa
shule ambayo itakaidi agizo hili,
itafutiwa usajili wake pamoja na
usajili wa wanafunzi wake na
kuwaagiza pia wazazi wa
wanafunzi hao kuhakikisha watoto
wao wanarudi shule siku hiyo
iliyoelekezwa.
Wizara imeeleza kuwa waraka wa
elimu namba 7 wa mwaka 2004
umepiga marufuku utaratibu huo
wa shule kukaririsha, kuhamisha
au kuwafukuza shule wanafunzi
kwa kutofaulu inavyotakiwa na
kueleza kuwa kuna shule zisizo za
serikali zimekuwa zikifanya
makosa hayo
 
Back
Top Bottom