Anayeuza meno ya Tembo anapomlaumu Ngassa!

Anayeuza meno ya Tembo anapomlaumu Ngassa!

Eddo kucha zako zitunze maccm hayapendi kukosolewa yanapenda kusifiwa.
 
Edo said:

Ni kweli. Tumekosa dira kama taifa. Hatujui tulipo wala tunapokwenda. Kabla haujamlaumu mwenzako jiulize, wewe unaifanyia nini nchi yako. je wewe Sekta yako ina maendeleo yanayostahili kabla ya kumnyooshea kidole mwingine?
Huwa nawaza sana.

Hapana siyo Tumekosa dira kama taifa....bali viongozi walio wengi wa taifa hili hawajakosa dira( wanazo dira) ila dira wanatumia zilizo feki(fake) kuliongoza taifa.

Eee...! Ndiyo..! Ni dira feki...dira ya ubinafsi uliopitiliza kuwa uuwaji ....dira ya kutorosha/kuiba wanyamapori na mazao yake nchi za kigeni...huku jamii zinazozunguka hifadhi hazifaidi huduma za jamii....Ni dira feki baadhi ya viongozi na watoto wao kufanya biashara ya magendo, kushiriki kukwepa kodi...kuwatumia wasanii...wanafunzi wanaosoma nje ya nchi kubeba na kuuza madawa ya kulevya hapa nchini na nje ya nchi...huku wakijua wanaharibu kizazi cha sasa na kijacho...

Edo..watanzania walio wengi ambao hawapo madarakani na wachache walioko madarakani wanayo dira halisi (siyo feki). Dira halisi ya kuwakomboa watanzania walio wengi. Tatizo hao viongozi walio na dira feki hawataki kabisa dira hii halisi itumike.


Well done Edo...!!
 
C:\DOCUME~1\[COLOR=

Chanda aka Chiwa,

uwe makini unapo-upload file kutoka kwenye HDD ya computer yako...!
 
Last edited by a moderator:
Ni Andiko la maana kwa kweli siyo siri ni kweli kuwa watu hatutimizi wajibu wetu halafu tunaishia kulaumu watu wengine ambao nao pia wanatoa lawama zao kwa kundi la watu wengine, kwa misingi hiyo ni kweli kuwa badala ya kutengeneza cheni ya UWAJIBIKAJI tunatengeneza cheni ya LAWAMA.
 


Tanzania tunafahamu nini zaidi? Tumepatia wapi hadi tuseme mpira ni tatizo sana? wasomi na wananchi wa kawaida tuanze kuitafakari nchi kwa pamoja. Tusitafakari kwa mapande mapande. Tuna tatizo kila sehemu. Nani hajawahi kulaumiwa au kulaumu? Kila mtu tatizo nchi hii…


hhaah! MACC wanamajibu hapa,
wansema TUMEJARIBU, TUMEWEZA, TUNASONGA MBELE
 
Yani mods mmemsikiliza yule zezeta mmeleta uzi huku badala ubaki kule siasani au mchanganyiko?

are u mad!!!!!! mbona unamawazo mgando hivyo yale ni mawazo yake na huyu mtu aliepost hii mada ajakosea kabisa but its okay watu kama hamkosekani humu kila jema mnapinga tu
 
Thread imeenda shule sana dah...lakin n mwendelezo tu wa malalamiko next tym inabidi zije thread za nin kifanyike...
 
Eddo Kumwembe haswaa simpendi kwa ukosefu wake wa adabu, 5/julay 1982 mjili lindi mtaa wa kawawa, tuko chobingo tunasubiri wahindi watoke jamatini ili mhindi mmjawapo rafiki yetu atuonyeshe mkanda wa mechi kati ya Brazil na Argentina world cup ya mwaka 1982, mechi iliyochezwa 2Julay 1982 ambayo Brazil iliibuka mshindi kwa bao 3-1.
Enzi hizo wajanja tulikuwa tunajipendekeza kwa wahindi ambao walikuwa na video kwenye jamatini zao walikwa na kanda za world cup lizokuwa zinatoka tv of Zambia kwa kutumia yale mamikanda makubwa kama mikate
Tulikuwa mimi wakati huo nasoma chuo kikuu nilienda Lindi kufanya field work Sokoine regional Hospital pia alikuwepo Advovate Kumwembe ambae nahisi ndiye baba yake Eddo Kumwembe aliyekuwa anaishi Ligula Mtwara alikwenda Lindi kwa shughuri zake za kiuwakili na rafiki yetu Sengwaji aliyekuwa anafanya kazi Tanesco Lindi katika mechi hiyo alikuwepo Yule gwiji wa kabumbu wa kizazi cha kati Diego Maradonna
Ilikuwa hivi Sengwaji alilopoka eti Maradonna ni zaidi Pele Advocate Kumwembe aling`aka na kumwamba aache kumlinganisha pele na Maradonna kwa sababu Maradonna hamfikanii pele hata kwa nusu.
Mala nyingi nimeona katika articles zake nyingi huyu Dogo Kumwembe anamponda Pele mbele ya Maradonna wakati sisi Pele tumemwona na Maradonna tumemwona watu hawa hawalinganishiki
Kwa hiyo kuanzia hapo huwa nimwamwona dogo huyu hana nidhamu kwa hiyo kila anachosema huwa siafiki.
Sasa ndo nini hivyo?
 
Sisi tunaongoza katka sera, kilimo kwanza
Mkukuta
Mkurabita
Big result now
Division five
Ufaulu usioridhisha aaah nimechoka
 
Mods ondoa ujinga huu! This is a political forum and not otherwise!
Popote hii makala itakapowekwa ni mwafaka kabisa!Ni uchambuzi uliotukuka, anayechukia ameguswa kinamna na ndo lengo lake haswaa!Big up Edo
 
Back
Top Bottom