Anayesupply samaki popote Golden, akae akijua anafanyiwa fitina

ephen_

JF-Expert Member
Oct 28, 2022
3,625
14,793
Habari Wanajf!

Leo Nikasema nijitoe out nikaenda Zangu Msasani kwenye hotel ya Golden. Nilipofika kama kawaida akaja Muhudumu akanipa Menu ya vinywaji nikachagua, Nikapewa menu ya chakula nikawa naperuzi ipi nichukue.

Macho yangu yakatua kwenye Grilled Fish! Basi nikamwambia niletee hii pamoja na Extra chips. Cha kushangaza huyu muhudumu akanambia " Sista nakushauri uchukue tu kuku! Yaani samaki wa hapa wanakaa hata wiki kwenye friji mpaka aje kupikwa radha yote ishaisha".

NIkachuja yale maneno nikamwambia ebu niletee hivyohivyo nihakikishe mwenyewe mimi sipendi maneno ya kuambiwa.

Baada ya muda samaki kaja, kumla hivi Uwiiii! Samaki ni mtamu balaaa! Nikaona hapa kuna bifu kati ya muhudumu na mtu anayesupply samaki.

Nikapanga nimwite kijana wakati wa kulipa nimpe vipande vyake yeye mwenyewe, kaja nikamwambia nataka kuswipe sina cash! Akanijibu ety mashine hatuna tunatumia lipa namba, nikaona huyu ana masihara Hotel ya kimataifa haina mashine ya kuswipe?

Nikamwambia nenda uje na manager wako, katoka kaja na mashine, nikamwambia SITAKI NAMTAKA MANAGER!!😂 akaja na mkaka nikamwambia wewe ndo manager akasema hapana Mimi ni supervisor.

Nikamuelezea jinsi huyu muhudumu anavyoharibu biashara kwa kukataza watu kula samaki, imagine ni watu wangapi wanaghairi kula samaki kwa sababu yake?

INSHORT nikawapa vipande vyao, Anayesupply samaki popote alipo akae akijua anafanyiwa FITINA!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom